Friday, June 7, 2013

Wakulima 940,800 wafaidi mbolea ya ruzuku

Katika mwaka wa fedha 2012/13, Serikali ilitoa ruzuku ya tani 126,117 za mbolea ambapo jumla ya wakulima 940,783 walinufaika na tani 8,278 za mbegu bora za mahindi huku wakipata mbegu bora za mpunga tani 1,694.

Kauli hiyo ilitolewa jana bungeni na Waziri wa Kilimo,Chakula na Ushirika Christopher Chiza ambaye alisema kuwa mipango hiyo imetokana na kukubalika kwa baadhi ya mazao ya chakula kuruhusiwa na kuwa mazao ya biashara.

Alikuwa akijibu swali la Martha Mosesi Mlata (Viti Maalumu-CCM), ambaye alitaka kujua kama Serikali inatambua kwamba kuna baadhi ya mazao ambayo ni chakula lakini yanatumika kama mazao ya biashara hivyo kuna sababu ya kuyapa ruzuku.

Mlata alihoji pia sababu za wakulima wa Mkoa wa Singida kuzuiwa wasilime zao la mahindi licha ya kuwa zao hilo linastawi vizuri mkoani humo.

Waziri alisema Serikali ilijikita katika kutoa mbolea ya ruzuku na pembejeo ili kuboresha uzalishaji wa mazao hayo na kuhakikisha wakulima wanapata chakula cha kutosha na kuwaongezea kipato.

Alisema kuanzia mwaka 2013/14 hadi 2015/16, Wizara kupitia mfumo wa matokeo makubwa imejiwekea malengo ya kuongeza uzalishaji kwa kiasi cha mahindi tani 100,000 na mchele tani 290,000 katika mashamba mapya ya wakulima wakubwa na wadogo.

Kwa mujibu Chiza, katika miradi hiyo Serikali inatarajia kutumia Sh 91.5 bilioni kugharimia ruzuku ya pembejeo za mazao zikiwamo mbolea.

Thursday, June 6, 2013

Teknolojia kuandaa miche ; Mbinu mpya ya kuongeza uzalishaji wa korosho

Wakulima wakitumia teknolojia ya kisasa kubebesha mikorosho katika Kituo cha Utafiti wa Kilimo Naliendele mkoani Mtwara hivi karibuni.

Wednesday, June 5, 2013

Wafugaji, wawindaji nchini waridhishwa Rasimu Katiba

Arusha
Mtandao wa Jamii za pembezoni za Wafugaji, Wawindaji wa Asili na Waokota Matunda, umeeleza kuridhishwa na rasimu ya Katiba Mpya iliyotambua uwapo wao na kulindwa rasilimali na tamaduni wao.
Mratibu wa Taasisi ya Katiba-Initiative iliyoundwa na mashirika yanayotetea jamii hizo, William Ole Nasha alisema mapendekezo yao mengi yamechukuliwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba.
“Kimsingi tumeridhishwa na rasimu hii, maombi yetu mengi yameingizwa na sasa haki za jamii hizi, ambazo ni ndogondogo zitalindwa,” alisema Ole Nasha.
Pia, alisema haki za wafugaji ambao wamekuwa wakikabiliwa na matatizo mengi zimeingizwa na kwamba, sehemu nyingi ya rasimu itakuwa ikijulikana kuwa Tanzania kuna wakulima, wafugaji na wavuvi.
“Siyo kutambuliwa tu bali mifugo imetambuliwa kama zao la uchumi la wafugaji, pia ni maisha na mila,” alisema Ole Nasha.
Naye Mwanasheria wa Mtandao wa Mashirika ya Wafugaji wa Asili na Waokota Matunda (Pingo’s Forum), Emmanuel Saringe alisema wanaunga mkono rasimu hiyo, lakini walitaka wafugaji kuondolewa kwenye kundi dogo katika jamii.
“Wafugaji ni wengi hasa hawa wa asili, tungependa watajwe kama kundi kubwa ambalo linahitaji kutambulika ingawa kwa sasa linatajwa katika rasimu kama sehemu ya makundi madogomadogo,” alisema Saringe.
Alisema wafugaji ni kundi kubwa katika jamii, ambalo lipo nyuma kwa maendeleo, hivyo linapaswa kupewa kipaumbele na katiba.
“Wafugaji ni kundi maalumu, hivyo linapaswa kulindwa katika katiba na kuendelezwa kwani lipo nyuma,” alisema Saringe.

Tuesday, June 4, 2013

Wakulima miwa wataka kulipwa fidia ya hasara


Mvomero. 
Serikali imeshauriwa kuwalipa fidia wakulima wa miwa waliopata hasara na umaskini wa kipato kutokana na soko la miwa lisilo na tija.
Soko hilo linadaiwa kuwafanya wakulima hao kushindwa kuendelea na kilimo hicho, kinachoonekana kukosa msisimko wilayani Mvomero, mkoani Morogoro.
Akizungumza kwenye mkutano wa wanachama, Mwenyekiti wa Chama cha Msingi cha Wakulima wa Miwa na Mazao Mengine Turiani (Tucopricos) Wilaya ya Mvomero, Majaliwa Kayanda alisema sheria zinazohusu miwa zinaonekana kumbeba zaidi mwekezaji na kumsahau mkulima mdogo.
Kayanda alishauri Serikali kufanyia kazi haraka mapendekezo yaliyofikiwa kwenye kikao na wakulima, kilichoitishwa na Wizara ya Viwanda na Biashara Machi mwaka huu.
Katika kikao hicho viwanda vinavyonunua miwa ya wakulima nchini vilihudhuria na kukubaliana na kwamba, kila mkulima anafahamu kiwango cha sukari kinachotoka katika muwa wake kabla ya kupelekwa kiwandani. Kwa upande wao, wakulima wa chama hicho walibainisha kuwapo kwa changamoto mbalimbali zinazohitajika kutatuliwa ili kumnusuru mkulima.
Changamoto hizo ni wafugaji kuvamia mashamba, huku Serikali ikishauriwa kuruhusu kuwapo kiwanda kingine cha sukari kuweka ushindani wa bei, badala ya soko kuhodhiwa na kiwanda kimoja.

Saturday, June 1, 2013

Tanzania kuongeza uzalisha wa kahawa ifikapo 2016

Morogoro. Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Christopher Chiza amesema kuwa Tanzania inatarajia kuzalisha tani 80,000 za kahawa ifikapo mwaka 2016 nia ikiwa ni kuongeza uzalishaji wa zao hilo na kukidhi masoko ya ndani na nje ya nchi.
Chiza pia alisema kuwa Tanzania imekuwa ikizalisha wastani wa tani 35,000 na 50,000 za aina mbalimbali za kahawa kwa mwaka ikiwa ni pamoja na aina ya Arabica, Robusta zenye soko kubwa katika soko la dunia.
Akizungumza katika ufunguzi wa mkutano wa wadau wa kahawa unaofanyika mjini Morogoro, Waziri Chiza alisema wizara yake imeweka mikakati mbalimbali ya kuboresha zao hilo ikiwa ni pamoja na kuongeza mikoa minane ya ulimaji wa zao hilo ambayo ni pamoja na Morogoro, Iringa, Njombe, Katavi, Geita na Manyara huku Serikali ikiendelea kujenga mazingira mazuri zaidi ya kilimo cha zao hilo.
Alisema hakuna sababu ya kilimo cha zao hilo kushuka, kwa kuwa zao hilo lina bei nzuri katika soko la dunia, akiwataka Watanzania kuzalisha kwa wingi hata pale bei ya zao hilo inaposhuka katika soko la dunia kwa kuwa imekuwa na mtindo wa kupanda na kushuka mara kwa mara.
“Zao la kahawa ni muhimu sana na ni lazima kuwapo na utaratibu wa kuwa na bei moja yenye manufaa kwa mkulima na nchi yetu kwani mkulima amekuwa na mahitaji makubwa ya kimaisha na anatakiwa kukuza uchumi wake,” alisema waziri huyo.
Waziri Chiiza alisema, umefika wakati wa kuanza kutafuta masoko mapya ndani na nje ya nchi badala ya kung’ang’ania soko moja na kujikita katika kulalamika na kuongeza kuwa ili kuweza kufanikiwa katika kutafuta masoko hayo, ni lazima balozi zitumike kusaidia ili wakulima waweze kunufaika.
Alisema Serikali itaendelea kushirikiana na wadau na bodi ya kahawa kusaidia kupitia ruzuku kila mwaka na kuzitaka halmashauri kutenga maeneo ya kilimo cha kahawa na kuweka bustani za miche ya zao hilo ili wakulima waweze kupata miche hiyo kwa bei nafuu.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa mkutano huo, Seleman Chambo mapema akimkaribisha Waziri Chiza alisema kuwa, uzalishaji wa zao la kahawa nchini umeshuka kutokana na sababu mbalimbali ikiwa ni pamoja na baadhi ya mashamba ya kahawa kulimwa mazao mengine huko mkoani Kilimanjaro wakati baadhi ya wadau wa kahawa nchini wakilalamikia kutofuatwa kwa bei elekezi ya kahawa.

Thursday, May 30, 2013

Stakabadhi ghalani yaongeza gharama kwa wakulima


Utaratibu ulioanzishwa na serikali wa kuuza bidhaa za mkulima kwa mfumo wa stakabadhi ghalani (WRS) katika baadhi ya maeneo yenye uzalishaji mkubwa, umeelezwa kuongeza gharama kwa mkulima, licha ya kuwapo kwa faida katika mfumo huo.
Kitendo cha wakulima kulipa tozo kwa kilo moja ya mazao inayonunuliwa kwa mfumo huo ni mzigo mzito kwa wakulima. Utafiti mpya unaonyesha kwamba
dawa ya kuondokana na gharama hizo ni wakulima kujiunga katika ushirika na kujiendesha wenyewe.
Imeelezwa kwamba ushirika huo utawasaidia wakulima kutumia vyema fursa za kiuchumi katika kuzalisha, kuhifadhi na kupata soko la uhakika.
Tunalipa Sh2 milioni
Ofisa Mtendaji wa Taasisi ya RUDI ambayo kazi yake ni kuongeza thamani ya bidhaa zinazozalishwa nchini, Abel Lyimo akizungumzia utafiti mpya unaohusu mfumo wa stakabadhi ghalani unaojulikana ‘Tanzania Warehouse Legal Framework and its Impact on Sesame and Rice Farmers,’amesema wakulima wanalazimika kumwajiri Meneja Dhamana wa kushughulikia mfumo huo na kwamba wanamlipa Sh2 milioni kwa mwezi.

Lyimo anasema utafiti huo uliangalia athari za
kisheria na kiutendaji wa mfumo wa stakabadhi ghalani kwa mazao ya ufuta na mpunga.
“Hii ni gharama kubwa kwa wakulima, kwanini wamwajiri Meneja Dhamana wa kuangalia ghala?” anahoji Lyimo. Anafikiri kwamba ni vyema wakulima
waachwe wachague namna nzuri ya kuhifadhi na kuuza bidhaa zao kupitia ushirika.
Kwa mujibu wa utafiti huo kitendo cha kumwajiri Meneja Dhamana ni kigumu kwa kuwa wataalamu wa aina hiyo wana gharama kubwa na inakuwa ngumu zaidi wanapotaka kulipwa kwa dola za Marekani, yaani fedha za kigeni.
Kwa mtazamo mwingine endapo wakulima wanapatiwa mafunzo na kwa kuzingatia teknolojia ya asili, wanaweza kabisa kuhifadhi mazao yao ghalani tena kwa ufanisi zaidi kuliko Meneja Dhamana.
“Mameneja dhamana wengi  hawana uzoefu na mazingira ya eneo husika,” anasema Lyimo. Anasema kupitia vyama vya ushirika gharama nyingi zisizokuwa na maana zitapungua kwa upande wa wakulima.
Kwa mujibu wa Chama Kikuu cha Ushirika cha Wakulima wa Mpunga cha Kilombero(AKIGIRO), shughuli ya hifadhi na masoko wao wanafanya vyema.
Kwa mujibu wa taarifa ya utafiti huo kuna tatizo la  maghala hivi sasa na yaliyopo yanaonekana kutumika kibinafsi zaidi,
na kusababisha wakulima kutokuwa na uwezo wa kudhibiti. Wakati mwingine wakulima wanalazimishwa kutumia mfumo wa stakabadhi ghalani hata kama
hawautaki mfumo huo.
Pia imebainika kwamba ni vigumu kwa wakulima kuteta na bodi yenye dhamana na masuala ya maghala kutokana na kuwapo kwa urasimu.
Kwa mujibu wa utafiti huo, wakulima hasa wale wa ufuta wa Mkoa wa Lindi wamekuwa katika mgogoro na serikali ya mkoa kwa sababu serikali hiyo iliwataka wauze ufuta kupitia mfumo wa stakabadhi ghalani na si vinginevyo.
Wakulima wa mpunga wa Kilombero wamesema bodi ya stakabadhi ghalani katika  eneo lao imekuwa na sheria kali ikiwa ni pamoja na kuwazuia wakulima wadogo kujenga na kumiliki maghala yao.
“Kwa mfano ili ghala litambulike katika mfumo wa malipo ya stakabadhi ghalani iwe na uwezo wa kuchukua si chini ya tani 200 na masharti mengine ambayo ni magumu,” inasema taarifa hiyo.


Kanuni zilizowekwa zinawazua watu binafsi na wakulima wadogo na wale
wa makundi kumiliki maghala yao katika maeneo yao,”inasema sehemu ya taarifa ya utafiti huo.
Kwa mujibu wa utafiti huo Halmashauri ya Kilwa mwaka 2012/13 iliamua
kujitoa katika mfumo wa Stakabadhi ghalani baada ya kubaini
kwamba wanapoteza fedha nyingi kwa kukumbatia mfumo huo.
“Sababu kubwa ni kwamba bei iliyokuwa inatolewa na chama cha ushirika
cha ILULU ilikuwa ndogo kuliko zile zinazotolewa katika mikoa ya Dar es Salaam na Mkoa wa Pwani zinazopakana na wilaya ya Kilwa,” inasema
taarifa hiyo.
Kuhakikisha kwamba mkulima, vyama vya msingi na serikali za mitaa zinafaidika, halmashauri ilitengeneza muundo mwingine wa soko la ufuta na pia mfumo wa soko la wazi ulidhibitiwa. Imeelezwa kwamba faida kubwa ya mfumo huo katika Wilaya ya Kilwa, gharama nyingi zilizopo katika mfumo wa stakabadhi ghalani, ziliondolewa.
“Wafanyabiashara walielekezwa kwenda katika vijiji kadhaa, kuamsha ushindani wa kibiashara,bei ya juu ilipatikana na hivyo kuongeza kipato kwa mkulima, vyama vya ushirika vya msingi na kwenye serikali za mitaa,” inasema taarifa hiyo iliyodhaminiwa na BEST AC.

Taarifa ya utafiti huo inaonyesha kwamba tofauti na mifumo mingine na  gharama za usafirishaji zinamezwa na mkulima. Katika mfumo huo mnunuzi
anabeba gharama za usafirishaji kwa kiwango kikubwa.
Mnunuzi alikuwa ananunua gunia la kuhifadhia mazao na kulipia riba za benki.

Kutokana na mfumo huo Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa iliingiza kama kodi katika mfuko wake Sh395 milioni katika msimu wa mwaka 2012/2013 kutoka Sh70 milioni katika miaka iliyopita,huku vyama vya msingi vikiwa vimevikusanya Sh250 milioni  na Sh7 bilioni.
Kwa upande wake mwanzilishi wa shirikisho la wakulima waliohitimu vyuo vikuu Stephano Kingazi anasema wakulima hawana nongwa na mfumo wa stakabadhi ghalani, lakini hawataki serikali kuwalazimisha kuuza au kutouza mazao yao.
“Wakulima wengi wanakubaliana na ukweli kwamba mfumo wa stakabadhi ghalani ni mzuri kwao, lakini wanasema kuna makato mengi kwa kilo
na kusababisha mzigo mzito kwa mkulima,” anasema Dk Kinganzi katika mahojiano hivi karibuni mkoani Morogoro.

Kwa mujibu wa utafiti huo, wakulima wa mpunga walikuwa wanakatwa asilimia
15 katika Wilaya ya Kilombero katika mfumo wa stakabadhi ghalani, asilimia 29 wilayani Lindi na asilimia 8 Kilwa kutokana na mfumo wake.
Wakulima wawe huru
“Kinachoonekana hapa, kuna watu wengi wanachukua fedha kwa mkulima hata kabla mazao yake hayajafikia mwisho wa safari.
“Itakuwa vyema kama wakulima watafanya shughuli za kuuza mazao yao
bila kuingiliwa na mtu,” inasema taarifa ya utafiti huo.
Kwa mujibu wa utafiti, stakabadhi ghalani inakuwa na faida zaidi kwa wakazi wa vijijini. Dk Elibariki Msuya, miongoni mwa watu walioandaa taarifa ya utafiti huo amesaema ingawa Tanzania inasheria nzuri zinazowezesha mfumo wa
stakabadhi ghalani ukilinganisha na majirani zake, bado serikali haijaufikisha mfumo huo mahali pa zuri.

“Wadau mbalimbali wameonyesha matatizo hapa na pale katika mifumo tofauti inayofanyakazi nchini kwa lengo la kusaidia wakulima; mfumo wa Mkoa wa Lindi unaonekana kuwa kikwazo,kwani una sheria nyingi zinazobana katika soko la wazi na unaonekana ni dhaifu.
Katika mfumo wa Kilwa unaonekana kuwa na nafuu zaidi na mzuri kwa wakulima kwani ulifanikiwa kupunguza tozo mbalimbali,” anabainisha Dk Msuya.
Mfumo wa Kilombero unawezesha mfumo wa stakabadhi ghalani kufanyakazi huku pia watu binafsi wakiendelea kufanyakazi na kumpa fursa mkulima kuchagua soko lenye bei nzuri.
 Habari zaidi:
Kuna maghala 60 katika mikoa 19.
Biashara ya maghala nchini inasimamiwa na Bodi ya kutoa leseni ya Maghala ambayo inafanyakazi chini ya sheria namba 10 ya mwaka 2005 ya stakabadhi ghalani na kanuni zake za mwaka 2006.
 Tangu kuanzishwa kwa bodi hiyo imetoa leseni kwa maghala 60 katika mikoa 19 yenye uwezo wa kuhifadhi tani 267,000.

Wednesday, May 29, 2013

Spika Makinda azima hoja ya Mdee kuhusu umiliki wa mashamba makubwa

Dar es Salaam. Spika wa Bunge, Anne Makinda jana aliizima hoja ya Mbunge wa Kawe (Chadema), Halima Mdee kuhusu umiliki wa mashamba makubwa yasiyoendelezwa wakati wa kujadili hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi ambayo ilihitimishwa bungeni jana.

Mdee alivutana na Spika Makinda wakati wa kujadili bajeti hiyo kifungu kwa kifungu, Mdee alipotaka kufahamu kauli ya Serikali kuhusu kampuni zinazomiliki ardhi bila kuziendeleza na hatua zinazochukua kuhakikisha zinarudishwa kwa wananchi.
Baada ya kuuliza swali hilo huku akisisitiza kutoa shilingi, Spika Makinda alimtaka kukaa chini kwa kuwa hoja yake haina mashiko ya kufanya hivyo na kwamba kama anataka aiwasilishe kama hoja binafsi.
“Kaa chini, nakwambia kaa chini,” alisema Makinda huku Mdee akionekana kuendelea kuzungumza... “Nasema kaa chini,” alirudia na Mdee kukaa huku akikipeperusha karatasi hewani kuonyesha kutokubaliana naye.
Awali, Mdee alisema shamba la Simanjiro ambalo Halmashauri ya wilaya hiyo ilipendekeza mwekezaji kupewa ekari 500 lakini Wizara ya Ardhi iliidhinisha ekari 25,000 ambazo mwekezaji hajaziendeleza zote wakati mashamba ya Kisarawe na mashamba ya mkonge Tanga ambayo wawekezaji wameyakopea fedha nayo hadi sasa hayajaendelezwa.
Alitaka kauli ya Serikali kuhusiana na hali hiyo na jinsi ya kurudisha mashamba hayo katika miliki ya umma. Mbunge mwingine aliyetishia kutoa shilingi ni Dk Faustine Ndungulile wa Kigamboni (CCM), akijikita katika suala la ujenzi wa mji mpya wa Kigamboni akisema wananchi wake hawakushirikishwa katika mipango ya ujenzi huo.
Akijibu hoja hizo, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka alisema wananchi wameshirikishwa kikamilifu katika mchakato mzima na kuahidi kukaa na mbunge huyo pamoja na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Fredrick Werema kuzungumzia suala la Kigamboni.
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Goodluck ole Medeye alisema kila mkazi atalipwa Sh35,000 kwa kila mita moja ya mraba na mwenye ekari moja atapata Sh141 milioni na kuwataka wananchi kutoa ushirikiano kwa kuwa mradi huo utakuwa wa maendeleo kwa kila mmoja.
Baada ya majibu hayo, Dk Ndungulile alisimama na kusema kuwa anakubali kurejesha shilingi hasa baada ya Waziri Tibaijuka kutamka kuwa wananchi wameshirikishwa na watashirikishwa katika kutatua mgogoro wa Kigamboni.
Spika Makinda aliwataka kushirikiana kutatua mgogoro wa Kigamboni ili mradi uanze.    

Plot For Sale


Tuesday, May 28, 2013

Starlet for sale

3.3 m pungufu unaongea
FOR MORE INFO CALL +255 713 615365
+255 765 615365, +255 784 615365

Maandilizi ya kilimo cha Mpunga Sengerema


Watoto  wa kijiji cha Luchili wilayani Sengerema wakiandaa shamba kwa ajili ya kupanda Mpunga. Zao la Mpunga  hivi sasa linalimwa na wananchi wengi wa mikoa ya Mwanza na Shinyanga kwa ajili ya chakula na Biashara. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).

Saturday, May 25, 2013

Mkulima mbaroni kwa kukutwa na kobe 70

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, David Misime akionyesha kobe hai wapatao 70 waliokamatwa. Kulia kwake ni Afisa Mnadhimu wa Jeshi hilo mkoani humo, Suzan Kaganda akiwa ameshika Ngozi ya DigiDigi.
 Mkulima Moses Nyawage (42), Mkazi wa Kijiji cha Ng’hongona Manispaa ya Dodoma anashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kukutwa na kobe 70 wenye thamani ya zaidi ya Sh. milioni 7.8.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, David Misime alisema kuwa mtuhumiwa huyo alikamatwa na kobe hao Mei 22 mwaka huu saa 10.30 jioni katika  maeneo ya Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom).

Alisema alipohojiwa mtuhumiwa huyo, aliwaeleza kuwa aliwapata  kobe hao katika maeneo ya Mwitikila na kuwahifadhi kwenye viroba.

Naye Elias Mathias  (45), Mkazi wa Pwaga Wilaya ya Mpwapwa anashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kupatikana na ngozi mbili za mnyama aina ya digidigi.

Mtuhumiwa huyo alikamatwa Mei 22, mwaka huu saa 10.30 usiku katika Kijiji cha Pwaga akiwa na ngozi hizo zenye thamani ya Sh.800,00 kwa mujibu wa sheria.

Watuhumiwa hao watafikishwa mahakamani baada ya upelelezi kukamilika.Mkulima Moses Nyawage (42), Mkazi wa Kijiji cha Ng’hongona Manispaa ya Dodoma anashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kukutwa na kobe 70 wenye thamani ya zaidi ya Sh. milioni 7.8.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, David Misime alisema kuwa mtuhumiwa huyo alikamatwa na kobe hao Mei 22 mwaka huu saa 10.30 jioni katika  maeneo ya Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom).

Alisema alipohojiwa mtuhumiwa huyo, aliwaeleza kuwa aliwapata  kobe hao katika maeneo ya Mwitikila na kuwahifadhi kwenye viroba.

Naye Elias Mathias  (45), Mkazi wa Pwaga Wilaya ya Mpwapwa anashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kupatikana na ngozi mbili za mnyama aina ya digidigi.

Mtuhumiwa huyo alikamatwa Mei 22, mwaka huu saa 10.30 usiku katika Kijiji cha Pwaga akiwa na ngozi hizo zenye thamani ya Sh.800,00 kwa mujibu wa sheria.

Watuhumiwa hao watafikishwa mahakamani baada ya upelelezi kukamilika.

Mkulima Moses Nyawage (42), Mkazi wa Kijiji cha Ng’hongona Manispaa ya Dodoma anashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kukutwa na kobe 70 wenye thamani ya zaidi ya Sh. milioni 7.8.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, David Misime alisema kuwa mtuhumiwa huyo alikamatwa na kobe hao Mei 22 mwaka huu saa 10.30 jioni katika  maeneo ya Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom).


Alisema alipohojiwa mtuhumiwa huyo, aliwaeleza kuwa aliwapata  kobe hao katika maeneo ya Mwitikila na kuwahifadhi kwenye viroba.


Naye Elias Mathias  (45), Mkazi wa Pwaga Wilaya ya Mpwapwa anashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kupatikana na ngozi mbili za mnyama aina ya digidigi.


Mtuhumiwa huyo alikamatwa Mei 22, mwaka huu saa 10.30 usiku katika Kijiji cha Pwaga akiwa na ngozi hizo zenye thamani ya Sh.800,00 kwa mujibu wa sheria.


Watuhumiwa hao watafikishwa mahakamani baada ya upelelezi kukamilika.

Friday, May 24, 2013

Waziri akiri kuhusu mbolea feki nchini

Naibu Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Adam Malima 

Dodoma
 Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika, imekiri kuwa inakabiliwa na changamoto ya kuwapo kwa mbolea isiyokuwa na viwango vinavyokubalika na inayoathiri uzalishaji wa mazao.
Kauli hiyo ilitolewa bungeni na Naibu Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Adam Malima, alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Peramiho, Jenister Mhagama (CCM).
Mbunge huyo alitaka kujua kauli ya Serikali kuhusu tatizo la ubora wa mbolea, linalowakabili wakulima katika kila msimu wa kilimo.
Naibu Waziri alisema Serikali kwa kutambua hilo, imeweka udihibiti wa mbolea isiyokuwa na viwango kwa kupitia sheria ya mbolea ya mwaka 2009, kifungu cha 7 (1).
“Pamoja na hayo, lakini pia Serikali imeunda Mamlaka ya Usimamizi wa Mbolea ambayo kazi yake ni kuthibitisha ubora wa mbolea viwandani,” alisema Malima.
Alisema katika kukabiliana na tatizo hilo katika ngazi ya halmashauri na wakulima, Serikali imeanza kutoa mafunzo kwa wakaguzi wa mbolea na kwamba hadi Mei mwaka jana kulikuwa na wakaguzi 44 kutoka katika halmashauri mbalimbali.
Kwa upande mwingine kiongozi huyo alisema tayari wizara imeweka utaratibu mzuri wa kuhakikisha kuwa mbolea inawafikia wananchi kila ifikapo Agosti mosi.


Thursday, May 23, 2013

Bajeti ya kilimo mwaka huu yawaacha wadau njiapanda

Bajeti ya Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika inapita kwa mbinde katika kikao cha Bunge la bajeti 2013 mjini Dodoma hivi karibuni.
Taarifa zinabainisha kwamba haikuwa rahisi kupita kwa bajeti hiyo kutokana na sababu nyingi, lakini kubwa ni mfumo wa stakabadhi ghalani na utaratibu wa ruzuku ya pembejeo, ushirika na sintofahamu iliyopo kwa wakulima wa pamba, miwa na tumbaku.
Mazao hayo ingawa ni roho ya uchumi wa mataifa mengi ulimwenguni, nchini wakulima wake wapo njia panda na mbaya zaidi hata fedha zizozotengwa kwa ajili ya shughuli mbalimbali za kilimo hazieleweki zinaenda wapi na zinafanya nini?
Hata hivyo bajeti ya serikali 2012/2013 haijaonyesha kutoa nafuu yoyote kwa wenye viwanda vidogo na wakulima na hali hiyo kuwaweka njiapanda watendaji katika sekta hizo kwani kilichotokea katika bajeti iliyopita haikuakisi nuru kwa bajeti ijayo.
Kulingana na Waziri wa Fedha na Uchumi, William Mgimwa, Sh17.7 trilioni, zimetengwa kwa ajili ya bajeti ya mwaka 2012/2013 na bajeti  ya sasa inatenga fedha za matumizi makubwa katika mafungu matano.
Mafungu hayo ni pamoja na kulipa deni la Taifa ambalo limetengewa Sh2.7 trilioni wakati Wizara ya Ujenzi Sh1 trilioni, ulinzi Sh920 bilioni, elimu Sh721  Bilioni na nishati na madini Sh641 bilioni. Jumla ya fedha zote ambazo zitatumika kama mafungu ya juu ni Sh5.982 Trilioni.
Serikali katika bajeti ijayo katika kile ilichoelezwa kuwa ni kukabiliana na changamoto ya upatikanaji wa mikopo ya muda mrefu, kilimo kisichokuwa na tija na ukosefu wa ajira,  imetenga fedha katika maeneo tofauti kwa ajili ya la kuhuisha sekta ya kilimo.
Kulingana na bajeti ya sasa, Sh30 bilioni zimetengwa kwa ajili ya Benki ya Rasilimali (TIB) Sh40 bilioni kwa Benki ya Maendeleo ya Kilimo, fedha ambazo zinaifanya benki hiyo mpya kuwa na mtaji wa Sh100 bilioni.
Waziri Mgimwa anasema bajeti imelenga kuboresha mazingira ya biashara na kutenga maeneo maalum ya uwekezaji mijini na vijijini.
Anasema lengo lingine ni kukuza ubia kati ya sekta ya umma na sekta binafsi na hatua hiyo inaenda sanjari na kuboresha viwanda vidogo vidogo nchini na kwamba  Sh128.4 bilioni, zimetengwa katika eneo hilo.
Bajeti ya serikali katika sekta ya kilimo inatajwa Sh328.1 bilioni kwa ajili ya maendeleo ya kilimo, na Sh130.5 bilioni kwa ajili ya ruzuku ya pembejeo  na Sh5.7 kwa ajili ya ushirika ambao unalalamikiwa kuwa ni kama umekufa.

Tuesday, May 21, 2013

Mbaroni akidaiwa kuuza mbolea feki

WIKI mbili baada ya blog hii kufichua uwepo wa dawa feki, mbegu na uchakachuaji wa mbolea kukithiri mkoani Mbeya, Jeshi la Polisi limefanikiwa kumnasa mmoja wa wanaodhaniwa kuwa ni wahusika wa mchezo huo mchafu.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Diwani Athumani, alisema kuwa walimkamata Jofrey Mbago, mkazi wa Chimala wilayani Mbarali akiwa na mifuko 100 ya mbolea aina ya CAN ikiwa ndani ya mifuko yenye nembo ya Premium Agro Chem Ltd.
“Tulipata taarifa kutoka kwa Adjurist Edward Ngezi ambaye ni Ofisa Mauzo wa kampuni ya kusambaza mbolea iitwayo Premium Agro Chem Ltd yenye makao makuu jijini Dar es Salaam, akimlalamikia wakala wao Jofrey Mbago kuwa anasambaza mbolea isiyo halali kwa kutumia mifuko ya kampuni yao,’’ alisema.
Alisema uchunguzi wa awali uliofanywa na bwana shamba wa mji mdogo wa Chimala, Ezbon Michael, umebaini kuwa ndani ya mifuko hiyo kulikuwa na mbolea inayosadikiwa kuwa ni aina ya Minjingu.
“Mtuhumiwa alipohojiwa alikiri kuwa mbolea hiyo alipelekewa na Samwel Mhavile na Abson Sanga wakazi wa Makambako na kwamba mbolea hiyo inauzwa sh 50,000 kwa kila mfuko wa kilo 50 na hadi anakamatwa alikuwa ameshauza mifuko mingi,’’ alisema Kamanda Diwani.
Alisema kutokana na tukio hilo, taratibu zinafanywa sampuli ya mbolea hiyo ipelekwe kwa mkemia mkuu wa serikali jijini Dar es Salaam ili kuthibitisha mifuko hiyo ina mbolea aina gani.

Monday, May 20, 2013

How to Grow Mushrooms Indoors


 Grow Mushrooms Indoors

Growing mushrooms at home is a task that any gardener interested in growing their own food should attempt. Mushrooms are a healthy addition to any diet, as they are low in calories and fat, high in fiber, and contain high amounts of potassium. In addition, they are very easy to grow at home. Mushrooms are best grown indoors where the temperature and light conditions can be more readily managed. Learning how to grow mushrooms indoors is a matter of managing their growing conditions carefully. 

Steps
 Decide what type of mushroom you want to grow. The 3 types of mushrooms that are easiest to grow at home are oyster, white button, and Shitake. The method for growing each mushroom is similar, but the ideal growing medium differs.
  • Oyster mushrooms grow best in straw; Shitakes grow best on hardwood sawdust; button mushrooms grow best in composted manure. These different growing media reflect the different nutritional needs of each species. However, each of these 3 species can be grown readily enough in sawdust or straw.
  • Choosing a type of mushroom to grow is a matter of taste. You should grow the type you most want to eat.
    1. Purchase mushroom spawn. Mushroom spawn is sawdust permeated with mushroom mycelia - essentially the root structure of the fungus. It is used much like plant seedlings to facilitate growth. You can purchase mushroom spawn from several online retailers, some gardening supply stores, or some specialty organic living stores.
      • Make sure to buy spawn rather than spores. Some retailers will also sell spores, which are more akin to the seeds of plants (rather than seedlings). Growing mushrooms from spores takes more time and practice, and is best suited for a seasoned mushroom grower.
    2. 3
      Heat the growing medium to spread the mycelia into it. The mycelia in your mushroom spawn need to spread into the growing medium thoroughly before producing mushrooms. A warm temperature encourages this growth.
      • After choosing the growing medium suited for your mushroom species, place a few handfuls of it into a baking pan. A shallow pan with a large surface area will provide the most room for your mushrooms to grow.
      • Mix the spawn into the growing medium with your fingers. Place the baking pan on a heating pad set to 70 degrees Fahrenheit (21 degrees Celsius). This is the ideal temperature to encourage growth.
      • Leave the setup in a dark environment, such as a cabinet, for about 3 weeks. This will allow the mushroom mycelia to permeate the growing medium.
    3. 4
      Place the growing medium into the proper environment. After 3 weeks, you need to place the pan into an environment that is dark and cool (about 55 degrees Fahrenheit / 13 degrees Celsius). A basement usually works well for this, but a cabinet or drawer in an unheated room will work in winter.
      • Cover the growing medium with a handful of potting soil and spray the entire mixture with enough water to dampen it thoroughly. You can place a damp towel over the pan to prevent moisture loss if desired.
      • The mix should be kept moist and cool as the mushrooms grow. Check it periodically and spray it with water as necessary.
    4. 5
      Harvest your mushrooms when they are fully grown. In about 3 weeks, you should see small mushrooms appearing. Continue to keep their environment moist, cool, and dark to encourage their growth. When their caps separate fully from their stems, they are ready to harvest. You can simply pluck them with your fingers; it is best to rinse them before cooking or eating.

    Things You'll Need

    • Mushroom spawn
    • Sawdust, straw, or manure
    • Baking pan
    • Heating pad
    • Potting soil
    • Spray bottle
    • Water
    • Towel

Friday, May 17, 2013

Wakulima wanusurika kifo

WAKULIMA wawili wilayani Kiteto, wamenusurika kuuawa na wafugaji jamii ya Kimasai baada ya kuibuka mapigano kufuatia ng’ombe kula mazao shambani.
Wakulima hao walionusurika kuuawa ni Samweli Malima (35) na Sanagali Athumani (29), wote wakazi wa Njutaa.
Akizungumza na Mwakilishi wa Blog Yetu jana hospitalini walipolazwa majeruhi, baba mzazi wa majeruhi hao, Waziri Mtambo (55) alisema tukio hilo lilitokea Mei 15, majira ya saa 7 mchana wakati vijana hao wakiwa shambani wakivuna mahindi.
Alisema vijana hao walipofika shambani waliwakuta ng’ombe wanakula mazao ndipo walipowauliza vijana wachungaji waliokuwa wakichunga ng’ombe hao na ndipo ukatokea ubishani.
Mtambo alisema baada ya muda mfupi walitokea Wamasai sita kwenye kibanda cha shambani ambacho Malima na Athumani kipindi hicho walikuwa wamepumzika na kuomba na wao kupumzika wakidai wamechoka baada ya kutembea umbali mrefu wakichunga ng’ombe ambao hawakuwa nao.
“Baada ya muda wakaongezeka tena Wamasai wengine na kuanza kuwachoma choma na sime ubavuni huku wakihoji kwanini wanazuia ng’ombe wasile chakula,” aliongeza.Alisema kutokana na hali hiyo, vijana hao walianza kujitetea, lakini walizidiwa nguvu na Athumani alizimia ndipo walipokimbia.
Mtambo alisema vijana hao waliokolewa na wapita njia ambao walitoa taarifa kijijini na wananchi kwenda mashambani ambako waliwakuta wametapakaa damu huku wakiwa wamepoteza baadhi ya viungo vya mwili.
“Athumani ambaye hali yake ni mbaya amechanwa na sime kichwani na kupasua mfupa wa fuvu, ametobolewa kwapani na sime, paji la uso kushoto karibu na jicho, amechunwa ngozi hadi usawa wa sikio na sime na Samweli Malima amekatwa dole gumba la mkono wa kulia, amejeruhiwa kichwani kwa sime na sehemu mbalimbali mwilini,” alifafanua.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Manyara, Akili Mpwapwa alikiri kuwepo kwa tukio hilo na kwamba tayari askari wameagizwa kwenda kudhibiti hali katika eneo hilo.

Thursday, May 16, 2013

Sh4 bilioni zatumika kwa kilimo Rukwa

Katika Kipindi cha mwaka wa fedha 2007/08 hadi 2010/11, Serikali imetoa Sh4 bilioni kwa ajili ya kusaidia miradi ya umwagiliaji katika Mkoa wa Rukwa , Bunge liliambiwa jana.
Kauli hiyo ilitolewa jana na Naibu Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Adam Malima ambaye alisema kuwa fedha hizo zilipelekwa katika maeneo ya Sakalilo, Katuka, Singiwe, Maleza, Ulumi, Ng’ongo na Lwafi/ Katongo.
Malima alitoa kauli hiyo wakati akijibu swali la Abia Nyabakari (Viti Maalumu-CCM) ambaye alihoji ni kwa nini Serikali isione umuhimu wa kuupa kipaumbele Mkoa wa Rukwa katika masuala ya kilimo cha umwagiliaji.
Naibu Waziri alisema kuwa Serikali imekuwa ikiupa kipaumbele Mkoa wa Rukwa kutokana na ukweli kuwa unazalisha mazao mengi ya kutosheleza mkoa na kutoa ziada kwa mikoa mingine na ghala la Taifa.
Alisema katika kipindi hicho pia Serikali ilitoa ruzuku ya pembejeo za kilimo, mbolea na mbegu bora na kwamba jumla ya kaya 546,647 zilipata ruzuku hiyo hiyo pamoja na mbegu bora za mahindi bila matatizo.

Serikali yaahidi kugawa mbegu bora kwa wakulima nchini

Serikali kupitia Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika imeweka mkakati madhubuti wa kuwapatia wakulima mbegu na mbolea kwa utaratibu ulio bora na wenye maslahi mapana, Bunge lilielezwa jana.
Kauli hiyo ilitolewa na Naibu Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Adam Malima ambaye alisema kuwa mkakati huo utatokana na ushauri wa kitaalamu wa kutoka kwa watalaamu wa ngazi zote wakiwamo wakulima, watafiti, wagani na mawakala wa mbolea.
Alikuwa akijibu swali la Athuman Mfutakamba (Igalula-CCM) aliyehoji juu ya Serikali kuwapatia wakulima wa maeneo ya Uyui mbegu bora na kuwabadilishia kutoka mbegu za zamani na kuwapatia mbegu za mahindi aina ya DKC 8053.
Malima alisema kuwa utaratibu uliopo ni kwa wakulima wa halmashauri husika kuwasilisha wizarani mahitaji halisi ya aina ya mbegu za mahindi wanazopendelea.
Kuhusu utaratibu wa utoaji wa ruzuku ya pembejeo kwa utaratibu wa vocha, alisema wakulima hunufaika kwa kupatiwa seti ya vocha tatu za mbolea ya kupandia.
Mbali na mbegu za mahindi lakini alisema wakulima kwa baadhi ya maeneo hupewa mbegu bora za mpunga ambapo wakulima wa eneo husika huchagua mbegu wanayoihitaji baada ya kushauriwa na maofisa ugani.

Monday, May 13, 2013

Zao la korosho kuendelea kuzama kwa sera mbovu

 

Dar es Salaam. Imeelezwa kwamba wakulima wa Korosho nchini wataendelea kupata mapato duni hadi hapo Serikali itakaposaidia uwekezaji wa viwanda vya ubanguaji wa korosho katika mikoa inayolima zao hilo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti ya Kuondoa Umaskini (Repoa), Profesa Samwel Wangwe alisema juzi kwamba uuzaji wa korosho zisizobanguliwa nje ya nchi ni hasara kwa wakulima.
Profesa Wangwe alisema hayo wakati wa majadiliano ya utafiti unaolinganisha ufanisi wa zao hilo kati ya Tanzania na Vietnam uliofanywa na Dk Blandina Kilama wa Repoa.
“Tunahitaji kuongeza thamani ya zao hili kwa kujenga viwanda vya kisasa vya kubangua korosho  ili tuweze kuuza kwa thamani itatayowanufaisha wakulima,” alisema Profesa Wangwe.
Wakati Profesa Wangwe akisema hayo, viwanda vya kubangua korosho ambavyo Serikali ilibinafsisha kwa watu binafsi, vimegeuzwa maghala ya kuhifadhia mazao na kusababisha korosho kuuzwa zikiwa hazijabanguliwa.
Kwa upande wake, Dk Kilama alisema katika utafiti wake kwamba ingawa Tanzania ilianza kilimo cha korosho kabla ya Vietnam lakini nchi hiyo iko juu kiuzalishaji kuishinda Tanzania.
Alisema kinachowasaidia ni kwamba mbali na Serikali hiyo kuweka sera bora za kilimo, pia kuna viwanda vingi vya kubangua korosho hali inayowafanya waongeze thamani ya zao hilo.
“Hata Bodi ya Korosho ya Vietnam inajumuisha wataalamu wa kilimo, wakulima na wabanguaji jambo ambalo ni tofauti hapa kwetu ambapo bodi inaweza kuwa na watu ambao siyo wadau wa korosho,” alisema na kuongeza kwamba Tanzania imeshuka kwa kiasi cha kutisha katika uzalishaji zao


Mwenyekiti wa wakulima kizimbani, anunua pamba bila leseni

Mwenyekiti wa Chama cha Wakulima wa Pamba Tanzania (Tacoga), Elias Zizi amepandishwa kizimbani kwa kosa la kuhujumu kilimo cha zao.
Zizi anashtakiwa kwa kununua pamba kabla ya msimu, ikiwamo kufanya biashara ya pamba bila leseni.
Mwendesha Mashtaka Polisi, Clement Kitundu alidaiwa mahakamani hapo kuwa mshtakiwa alikamatwa May 6, mwaka huu Kijiji cha Mbiti, Kata ya Mango, wilayani Bariadi, akinunua pamba.
Kitundu alidai kuwa suala hilo ni kosa tena bila leseni. Ilidaiwa kuwa kwa vipindi na siku tofauti, mshtakiwa ambaye ni kiongozi wa chama cha wakulima anayetambua na kuelewa sheria na kanuni, alitenda kosa hilo na kufanikiwa kununua zaidi ya tani moja ya pamba kwa nia ya kuiuza baadaye.
Mshtakiwa alikana mashtaka hayo na kuachiwa kwa dhamana, Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Wilaya Bariadi, Robert Oguda aliamua mahakama kuhamia eneo la tukio kupima na kushuhudia pamba hiyo ikiwamo kupima uzito, kazi iliyofanyika chini ya usimamizi wa polisi.

Saturday, May 11, 2013

Wakulima 3,000 kunufaika na kilimo shadidi

WAKULIMA 3,000 wa zao la mpunga katika vijiji vinane vilivyopo Halmashauri ya Wilaya ya Iringa, watanufaika na mfumo wa kilimo shadidi (System of Rice Intensification (SRI) kuanzia msimu ujao wa kilimo.
Katibu Tawala wa Wilaya ya Iringa, Elvin Mwakajinga, alibainisha hayo kwenye maadhimisho ya Siku ya Mkulima yaliyofanyika katika Kijiji cha Makifu na kuwakutanisha baadhi ya wakulima wa mpunga wa Wilaya ya Kilombero mkoani Morogoro, Mbarali, mkoani Mbeya na Iringa.
“Kunufaika kwa wakulima hao ni matokeo ya mafunzo ya kuanzishwa kwa mfumo huo katika Wilaya ya Iringa yaliyoendeshwa kwa wakulima 512 na Taasisi ya Maendeleo Mijini na Vijijini (RUDI) Novemba, mwaka jana na kufuatiwa na mashamba darasa 50 msimu huu wa kilimo,” alisema Mwakajinga.
Mwakajinga alisema ni jambo jema kwa mfumo huo kuwafikia wakulima wengi na ikiwezekana wote na kuwataka watendaji wa vijiji na kata kuanzisha na kufufua vikundi vya wakulima, ili wawe na nguvu ya pamoja.
Mtendaji Mkuu wa RUDI, Abel Lyimo, alisema katika maeneo ambayo mfumo tayari unatumika kama Kilombero na Mbarali, uzalishaji umefikia magunia 40 kwa ekari moja.
Kwa upande wao, wakulima hao walisema mfumo utawasaidia kuongeza kipato cha kaya na taifa kwa jumla na kuiomba serikali kusaidiana na taasisi ya RUDI kueneza mfumo huo kwa wakulima wote nchini.

Waziri Chiza kuzindua bodi mpya ya kahawa

 
Bodi mpya ya Wakurugenzi wa Bodi ya Kahawa Tanzania (TCB), itazinduliwa wiki ijayo mjini Dodoma na Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Christopher Chiza.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TCB, Astery Bitegeko, alithibitisha jana kuwa uzinduzi wa bodi hiyo ambao umepokewa kwa furaha na wakulima wa kahawa nchini utafanyika Jumatano ijayo.
Kuvunjwa kwa bodi ya awali kulitokana na malalamiko kutoka kwa wakulima akiwamo Mbunge wa Mbozi Mashariki, Godfrey Zambi aliyedai uteuzi wake ulikiuka sheria ya kahawa ya mwaka 2001.
Wajumbe wapya wa bodi hiyo ni Dk Juma Ngasongwa anayekuwa mwenyekiti na Mkurugenzi Mkuu wa TCB, Adolf Kumburu anayekuwa katibu wa bodi hiyo.
Wengine na taasisi wanazotoka zikiwa kwenye mabano ni Novatus Tiigelerwa (Kdcu), Profesa Suleiman Chambo (Muccobs), Thahir Nzalawahe na Philip Mbogela kutoka Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika.
Profesa Chambo na Mbogela wameingia katika bodi hiyo kama wataalamu wa zao la kahawa linalokabiliwa na changamoto mbalimbali, ikiwamo kuongeza uzalishaji, ubora na kusaka masoko mapya.
Wajumbe wengine ni Fatima Faraji (TCGA), Hyasinth Ndunguru (Kimuli Amcobs), Amir Hamza (TCA) na Maynard Swai kutoka Chama Kikuu cha Ushirika Mkoa wa Kilimanjaro (KNCU).

Thursday, May 9, 2013

KILIMO BORA CHA MAHINDI

Mahindi ni chakula muhimu na ni aina ya nafaka katika mataifa ya Afrika yaliyomo kusini mwa jangwa la Sahara. Ni chakula cha matumizi ya nyumbani kwa idadi ya watu inayokadiriwa kuwa asilimia 50. Ni chanzo muhimu cha madini na kuongeza nguvu mwilini, protini, madini ya chuma (iron) vitamini na madini mengine asilia.Waafrika hutumia mahindi kwa njia mbalimbali – (uji, ugali na pombe). Na mahindi ya kuchoma. Kila sehemu ya mmea wa mahindi ina thamani kiuchumi : punje, majani, shina na magunzi huweza kutoa kiasi kikubwa cha bidhaa nyinginezo zilizo chakula na zisizokuwa chakula.

Vile vile mahindi ni chakula muhimu cha mifugo (ng’ombe) na huhifadiwa kama silage. Pia mabaki ya mimea na nafaka na pia hutumika viwandani kutengeneza wanga na mafuta.
Mahitaji ya mahindi katika hali ya hewa, udongo na Mahindi ni mimea ambayo hustahimili mabadiliko mengi ya hali ya hewa na humea katika maeneo mengi tofauti. Kuna aina nyingi za mahindi yanayotofautiana katika muda wa kukomaa, mahindi huwa na ustahimili mkubwa kwa mabadiliko katika kiwango cha joto. Mahindi haswa huwa mimea ya maeneo ya joto ambako unyevu ni wa kutosha. Mmea huu unahitaji kiwango cha joto cha kila siku cha nyuzi joto 20º ili umee vyema. Joto la juu sana kwa mazao mazuri ni kama nyuzi joto 30º. Hupandwa sana katika sehemu zilizo katika kimo cha mita 3000 kutoka bahari hadi kwenye ukanda wa pwani. mahindi yaweza kupandwa kama chakula cha mifugo. 

Mahindi huwa yanaathirika na ukosefu wa unyevu wakati wa kutoa maua na matunda. Pia yanahitaji maji ya kutosha wakati wa kupanda. Katika nchi za joto jingi (tropiki), mahindi hufanya vyema katika mvua ya kiwango cha milimita 600 hadi 900 wakati wa kukua. Mahindi yanaweza kukuzwa kwenye aina nyingi za udongo lakini hukua vyema zaidi katika mchanga, usiotuamisha maji mengi, ulio na hewa ya kutosha na ulio na rutuba na madini ya kutosha. Kuwepo kwa mazao mengi ya mahindi kunapelekea kunyonywa sana kwa madini kwenye udongo. Mahindi yaweza kukuzwa katika udongo ulio na hali ya mchanga na (PH) kutoka 5 hadi 8 ingawa 5.5 hadi 7 ndio mwafaka. Mahindi yako katika kikundi cha mimea kinachoaminika kuathirika na hali ya chumvi katika maji na udongo. Kwa vile mimea ambayo ni michanga huwacha sehemu kubwa bila kuzingirwa na ardhi, mmomonyoko wa udongo na kupoteza maji hutokea sana sana hivyo basi ni bora umakini uzingatiwe katika uhifadhi wa udongo na maji kwa kuweka matandazo (mulching).

MATUMIZI YA MBOLEA
Mahindi hustawi zaidi yakiwekwa mbolea, iwapo mambo mengine yanayosaidia katika kukua pia yapo kwa kiwango kinachostahili. Mbolea inayotumiwa na wakulima wadogo mara nyingi huwa haitoshi. Mahindi ya kiwango cha juu yaweza tu kufikia kiwango cha juu cha Uzalishaji iwapo yatapewa lishe na madini ya kutosha. Mahindi ya tani 2 kwa hekta na tani 5 kwa hekta hutumia karibu kilo 60 N, kilo 10 za P205 na kilo 70 K20 kutoka katika udongo. MAhindi hunyonya Nitrogen pole pole katika miezi ya kwanza baada ya kupanda, lakini huongezeka hadi kiwango cha juu kabisa wakati wa kutoa maua na kukuza tunda (gunzi). Mahindi huhitaji nitrogen kwa kiwango cha juu na ukosefu huwa ndio kizingiti. Kiwango cha juu cha nitrogen kinahitajika mara tatu; kwanza wakati wa kupanda, pili, wakati ambapo mmea umefikia sentimita 50 za urefu na tatu, wakati matunda ya mahindi yanaanza kutoa zile nyuzi nyuzi nyororo (silking).

Udongo mwingi huwa na madini ya phosphorous (P205) na potassium (K20) lakini sio kiwango kinachotosheleza mahitaji haswa ya mbegu za mahindi zinapochipua. Nyunyuzia P205 karibu na mbegu ili ziote kwa haraka. K20 hutumika kwa kiwango kikubwa lakini hitaji la mimea hubainika baada ya upimaji wa hali ya udongo kujua kiasi cha mahitaji (soil test).

DALILI ZA UPUNGUFU WA MBOLEA
Ukosefu wa K20 husababisha ncha za majani kuwa na rangi ya njano na kuunda gunzi (cob) lisilo na punje hadi juu. Ukosefu wa P205 hufanya matawi kuwa na rangi ya samawati na mbegu zisizo laini. Dalili za ukosefu wa nitrogen ni majani ya rangi ya manjano na mimea dhaifu mifupi. Phosphate haifyonzwi haraka na mahindi na pia udongo mwingi wa nchi za joto hukosa madini hayo ya phosphate. Inashauriwa unyunyuzie mbolea ya kiasili kama samadi kabla ya kulima ili uboreshe hali ya udongo na kuongezea madini.

Katika ukulima wa kiasili,
(organic farming, Nitrogen (N) hutiwa kwenye udongo kupitia kwa upandaji wa mimea ya jamii ya mikunde (legumes) ambayo hutoa nitrogen katika hewa, Hata hivyo mapendekezo ya kimbolea yaliyo katika misingi ya uchunguzi wa udongo hutoa nafasi nzuri ya kupata kiasi kizuri cha mbolea bila kuweka kiwango cha chini au juu. Omba msaada kutoka kwa mafisa ugani wa kilimo waliyo katika eneo lako.
Katika maeneo yanayo tegemea mvua kukuza mahindi, panda mbegu wakati wa mvua ya kwanza. Hii itaruhusu mizizi kunyonya madini yaliyotengenzwa na bakteria katika udongo. Maji yaliyosimama huyeyusha na kuondoa madini ya nitrogen kutoka katika udongo na kusababisha ukosefu wa Nitrogen.


KUDHIBITI MAGUGU
Udhibiti wa magugu ni muhimu sana. Katika wiki 4 hadi 6 za mbele baada ya kumea, mahindi huathiriwa sana na magugu. Ni lazima mahindi yapandwe mara moja baada ya kutayarisha shamba. Unaweza kulima katikati ya laini za mahindi ili udhibiti magugu. Nchini Tanzania, kupalilia mara mbili kunahitajika kwa aina nyingi za mahindi, ingawa kupalilia kwa mara ya tatu kutahitajika kwa aina ambazo zinahitaji miezi 6 hadi 8 kukomaa. Kupalilia kwa mikono kunahitaji siku 15 kwa hekta la mikono (power tiller) ni masaa mawili mpaka matatu kwa ekari.

UHUSIANO WA NIPE NIKUPE
Desmodium (desmodium uncinatum) nyasi ya Molasses (melinis minutifolia) zikipandwa kati kati ya laini za mahindi huzuia wadudu kama stalk borers moths. Mimea hii hutoa kemikali ambazo huwafukuza wadudu aina stem borers’ moths. Zaidi ya hayo Desmodium huzui gugu haribifu,witchweed striga hermonthica. Napier grass (pennisetum purpureum) na Sudan grass (sorghum vulgare sodanese) ni mimea mizuri sana inayonasa wadudu aina ya stem borers. Napier grass ina njia yake madhubuti ya kujikinga dhidi ya wadudu wanaotoboa mmea kwa kutoa utomvu kutoka kwenye shina, ambayo huzuia wadudu kufyoza mmea na kusababisha uharibifu. Nyasi hizi pia huvutia adui wa stem borers kama mchwa, earwigs na buibui. Nyasi aina ya Sudan pia husaidia maadui asilia, kama nyigu (parasitic wasp)

MAHINDI TAYARI KWA KUVUNWA

Mahindi huweka kivuli kwenye mimea ya mboga mboga ikipandwa safu moja katikati ya mboga kwenye maeneo yaliyo na jua kali. Hii huongeza mazao ya mboga zilizopandwa hivi. na mimea jamii ya mikunde huongeza nitrogen kwenye udongo ambayo huitajika zaidi katika ukuaji wa mahindi pia hupunguza wadudu aina ya (leafhoppers, leafbeatles, stalk borers na fall army worm), upandaji wa mimea jamii ya mikunde ufanyike mara baada ya palizi ya kwanza

UVUNAJI
Uvunaji hufanyika kwa kutumia mikono kwa mashamba madogo na mashine (combine harvester) hutumika kwa ajili ya mashamba makubwa, Zao la wastani la mahindi ulimwenguni mnamo mwaka 2000 lilikuwa kilogramu 4255 kwa kila hekta. Zao la wastani nchini Marekani ilikuwa kilo 8600 kila hekta, huku mataifa yaliyo chini ya jangwa la Sahara la Afrika yakivuna kilo 1316 kwa kila hekta ya shamba. Zao la wastani katika taifa la Tanzania kati ya mwaka 2001-2005 lilikuwa kati ya gunia 15-19 kwa hekta (sawa na kilo 1350-1750) Ukilima kwa kuzingatia ukulima wa kisasa na kanuni zake kwa Tanzania utavuna kilo 5000 kwa hecta (ukanda wa pwani) na kilo 7500 kwa nyanda za juu kama Iringa, Mbeya, Ruvuma, Arusha n.k

Serikali yashauriwa kuboresha kilimo cha mpunga

 https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEja5ruF1cI73v7-vjmKbFZvJGHMjUWNDco2jXgHKFoCWX-u_w0HjwlRH8abF4vHrJilVQj0cS_G_a1Gw8A35kGMAY0pmVgyFk4fXCyI-AXxklvQ-y0goN3Kc4HGPQ9jjVaIqZP2WpFDfRs/s1600/AA_3356.JPG
SERIKALI imeshauriwa kutumia fedha zinazonunulia mchele toka nje ya nchi kuboresha kilimo cha mpunga hapa nchini. Ushauri huo ulitolewa na Meneja wa Mradi wa Shirika linalojihusisha na Shughuli za Maendeleo Vijijini (RLDC), Francis Massawe.

Alisema Serikali imekuwa ikitumia fedha nyingi kununua mchele toka nje ya nchi hivyo ni vyema fedha hizo ingezitumia kutoa elimu kwa wakulima namna ya kuboresha kilimo hicho waongeze vipato vyao.


“Ni vyema Serikali ikaliangalia suala hili kwa kina ili kuweza kuwasaidia wakulima wetu hapa nchini kwa lengo la kuwawezesha kujikwamua na umasikini,” alisema Massawe.

Alisema wakati umefika sasa kwa wakulima kupatiwa mikopo na taasisi za fedha waweze kutumia mbegu bora na pembejeo za kilimo za kisasa kuendana na mazingira ya kilimo bora na cha kisasa.

Aalisema wamejipanga kuhakikisha uzalishaji wa mazao ya vyakula unaongezeka waweze kuuza nje ya nchi na kuongeza Pato la Taifa.

Alisema wamekuwa wakiwawezesha wakulima na wafugaji kwa kuwapa elimu bora kuhusiana na kilimo na ufugaji ikiwemo kuwapa mikopo.

Alisema mkakati wao ni kuhakikisha wanaongeza uzalishaji wa mazao mbalimbali ya vyakula kuuza nje ya nchi na wala si kuagiza mazao toka nje ya nchi
.

Tuesday, May 7, 2013

Wakulima waaswa kuzingatia ushauri wa watafiti, watalaamu

WAKULIMA nchini wametakiwa kuzingatia ushauri wa watafiti na wataalam mbalimbali wa kilimo waweze kuzalisha mazao bora yenye tija katika soko la Afrika Mashariki (EAC).

Akizungumza Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa Taasisi ya Kimataifa ya Utafiti wa Kilimo (IITA), Dk.Victor Manyong alisema endapo wakulima watazingatia ushauri watazalisha bidhaa bora zenye kukidhi matakwa ya walaji na hatimaye kuzalisha faida itakayowakwamua wao na familia zao.


Alisema IITA imekuwa ikifanya utafiti katika nchi mbalimbali za EAC kwa wakulima wadogo na kwa Tanzania tangu utafiti wa kilimo uanze mwaka 1994 kwa zao la mihogo na imeweza kuwaelekeza wakulima ni mbegu zipi zinafaa kulingana na ardhi yao.

“Kwa kushirikiana na Wizara ya Kilimo tumejikita katika utafiti mbalimbali na lengo kuu ni kuwasaidia wakulima waweze kulima kilimo cha kisasa kwa kutumia mbegu bora ambazo zitawasaidia kujiongezea kipato na kuachana na tabia ya kulima kwa mazoea,”alisema Manyong.

Alisema si kila mbegu au ardhi inafaa kwa kila zao hivyo kila fursa iliyopo inatumiwa kufanya utafiti na kugawa aina ya mazao yanayoonekana ni bora kwa majaribio kwa kuwapa wakulima ili na wao wajaribu na kutoa maoni yao.

Manyong alisema katika mkakati huo hadi sasa taasisi imeweza kubaini mbegu 18 za mihogo ambazo ni bora na zifaa kwa mkulima kupanda na kuzalisha faida kwa wingi endapo atazingatia maelekezo ya wataalam.

Alisema ili kuendelea kutoa huduma bora kwa wakulima nchini taasisi imejenga jengo lenye maabara ya kisasa la utafiti ambalo linatarajiwa kulizinduliwa Mei 13 mwaka huu na Rais Jakaya Kikwete.

Manyong alisema kuzinduliwa kwa jengo hilo kutasaidia kuwapa uelewa zaidi wanafunzi na watalaam wa utafiti mbalimbali wa kilimo nchini.

Grace Kihwelu alilia zao la kahawa

Dodoma
Mbunge wa Viti Maalum, Grace Kihwelu (Chadema) ameitaka Serikali kuja na mpango madhubuti wa kufufua kilimo cha kahawa katika Mkoa wa Kilimanjaro.
Akiuliza swali bungeni jana,mbunge huyo alisema kwa miaka mingi zao hilo limekuwa tegemeo kwa wananchi wa Mkoa wa Kilimanjaro,lakini kwa sasa kilimo hicho ni kama kimekufa.
“Je Serikali ina mpango gani madhubuti na mahsusi wa kufufua kilimo cha kahawa Kilimanjaro ambacho kwa miaka mingi kimekuwa tegemeo kwa wananchi wa Kilimanjaro na mhimili mkubwa kwa uchumi wa taifa?” Alihoji Kiwelu.
Akijibu swali hilo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mahusiano na Uratibu, Stephen Wassira alisema Serikali imeandaa mkakati wa kuendeleza tasnia ya kahawa kwa lengo la kuendeleza kilimo cha kahawa nchini kwa kuongeza tija na ubora wa kahawa kitaifa.
Aliyataja maeneo mahsusi ya mkakati huo ni pamoja na kuongeza uzalishaji wa kahawa safi kutoka wastani wa sasa wa tani 50,000 kwa mwaka hadi tani 100,000 ifikapo mwaka 2022.
Nyingine ni kuongeza ubora wa kahawa ili kupata bei ya ziada katika masoko ya nje kutoka wastani wa asilimia 35 hadi kufikia wastani wa asilimia 70 ifikapo mwaka 2022,” alisema
Alisema maeneo muhimu katika mkakati huo ni pamoja na kuimarisha huduma za ugani ili wakulima wazingatie kanuni bora za kilimo cha kahawa na kushirikiana na Taasisi ya Utafiti wa Kahawa (TaCRI) ili kuhakikisha upatikanaji wa miche bora ya kahawa.
Wassira alisema pia serikali inaendelea kuongeza matumizi ya viwanda vya kati vya kutayarisha kahawa ili kuongeza ubora wa zao hilo hivyo wakulima kunufaika na bei nzuri.

Saturday, May 4, 2013

MAELEZO YA MSINGI KUHUSU KILIMO CHA MIGOMBA

 
UTANGULIZI
Ndizi ni zao linalolimwa katika ukanda wa tropiki na hutumika kwa ajili ya kupikia na kama matunda. Vilevile ndizi huweza kutengenezea starch, chips, pombe (mbege), ama kukaushwa na kuuzwa kama matunda yaliyokaushwa. Wakati mwingine ndizi hutumika kutengenezea unga ambao huweza kutumika kwenye supu, mikate, ugali na uji. Maua ya ndizi huweza kutumika kama mboga, ila ni lazima yachemshwe kwenye mji ya chumvi ili Kuondoa ladha ya uchungu. Majani ya mmea huu ni chakula kizuri cha kuku na wanyama na huwa na virutubisho aina ya protein kwa wanyama hawa. Pia majani haya hutumika kwa ajili ya kupakia vitu mbalimbali na kwa ajili ya kuezekea nyumba. Pia ni mazuri sana kwa kutandazia shamba ama bustani. Halikadhalika migomba hutumika kuzuiya ama kupunguza kasi ya upepo.


MAHITAJI YA MAJI, HALI YA HEWA NA UDONGO
Wakulima wa mwanzo kabisa wa ndizi walitokea huko Maleshia na kusini mashariki mwa bara la Asia. Huko ndizi ilikuwa ikilimwa kwenye udongo wenye rutuba nyingi sana na udongo wa volkano. Pia kwenye delta za mito na kandokando ama ndani ya misitu ambako udongo huwa na rutuba sana.
Ndizi hukua vizuri sehemu zenye joto kidogo na unyevu nyevu na mwinuko wa 0-1800 m kutoka usawa wa bahari . Aina nyingine kama ‘DWARF CAVENDISH’ huweza kusitawi hadi kwenye mwinuko wa mita 2100 kutoka usawa wa bahari (sehemu za milimani sana).
Mahitaji ya mvua ni ya wastani wa 1000mm kwa mwaka japokuwa migomba husitawi vizuri kama ikipata maji ya kutosha. Hii ni pamoja na kumwagilia kipindi cha kiangazi bila kutuamisha maji.
Halijoto ya 27°C hadi 38°C ndio ifaayo kwa kilimo cha ndizi na migomba hudumaa kama kuna baridi sana (chini ya 13°C.)
Upepo mwingi ni tatizo kwa migomba kwa kuchana majani na kuyaharibu pia kuangusha migomba. Kupanda migomba kwa vikundi husaidia kuzuiya upepo na ikibidi migomba iliyobeba ndizi iwekewe nguzo kama zinapatikana.
Udongo mzuri kwa kilmo cha ndizi ni tifutifu yenye uwezo wa kupitisha maji na hewa kwa urahisi. Udongo wenye mbolea nyingi ni mzuri sana kwa migomba.


UPANDAJI
Ndizi hupandwa kwa kutumia vichipukizi ama migomba midogo ama sehemu za viazi zenye uwezo wa kutoa vichipukizi. Uzao wa ndizi hutegemea sana aina na umri wa vichipukizi vilivyotumika wakati wa upandaji. Vichipukizi vizuri ni vile vilivyochongoka vyenye urefu wa sentimeta 75 na upana wa chini ya shina wa sentimeta 15 na majani yake yamechongoka. Hivi huzaa baada ya miezi 18 tangu hayajapandikizwa. Vipandikizi hutoa ndizi hata baada ya miaka 2-3. Migomba mikubwa wastani huzaa bada ya miezi 5-8. Vichipukizi maji vyenye majani mapana havifai kwa kupandikiza kwani huzaa ndizi ndogo na uwezekano wa kupona baada ya kupandikizwa ni mdogo.
VIPIMO
Miche ama vichipukizi vya migomba vipandwe kwenye shimo lenye urefu wa sm 60 na upana wa sm 60. Udongo uchanganywe vizuri na mbolea ya kutosha. Kama mvua hazitoshi, shimo liwe na urefu wa sm 150 na upana wa sm 100.
NAFASI
Kwa aina za migomba midogo nafasi kutoka mmea hadi mmea iwe mita 3, na kutoka mstari hadi mstari iwe mita 3. Migomba 1000 kwa ekari.
Kwa aina ndefu. Mmea hadi mmea mita 3 na mstari hadi mstari mita 4. Migomba 480 kwa ekari.
MUDA WA KUPANDA MIGOMBA
Muda muafaka ni mwisho wa msimu wa kiangazi ama mwanzo wa msimu wa mvua.
MCHANGANYO WA MAZAO
Mazao kama kahawa, mahindi,mbogamboga, papai, miti ya matunda, kivuli na mbao, na mikunde kunde.
MATUNZO
Wiki 4-6 tangu migomba ipadwe, inapaswa kupaliliwa. Pia migomba inafaa kupangiliwa kwa mafungu. Migomba isizidi minne kwa kila kifungu. ‘KISUMU’, vichipukizi vyote viondolewe kubaki na mgomba mmoja mkubwa, na midogo mitatu yenye umri tofauti tofauti ili kupata mazao mwaka mzima.
Migomba mingi sana husababisha kuzaa ndizi ndogo. Vichipukizi vyenye afya ndio vibakishwe, Uchaguzi ufanyike kufuata nafasi iliyopo. Vichipukizi visivyotakiwa vikatwe na kuharibiwa sehemu inyokua.
KUTANDAZIA
Matandazo ni muhimu sana na ikibidi yawekwe shamba zima. Matandazo yawekwe umbali wa sm 60 kutoka kwenye kila fungu la migomba. Hii inasaidia Kuepuka wadudu waharibifu kwenye mizizi ya migomba.
MBOLEA
Migomba huhitaji sana mbolea ili izae vizuri. Mimea aina ya mikunde kunde inaongeza rutuba kwenye udongo kama ikipandwa shambani. Pia mbolea ya samadi na mboji ni muhimu sana. Kama kipato kinaruhusu tunashauriwa kutumia mbolea ya miamba ya Minjingu; ‘MINJINGU ROCK PHOSPHATE’ kwa ajili ya kuboresha na kuimarisha mizizi ya migomba.
MAGONJWA NA WADUDU WANAOSHAMBULIA MIGOMBA
Bacterial wilt(Mnyauko wa bacteria).
Mwanzoni jani mojawapokati ya majani machanga matatu huanza kuwa njano na kuvunjika. Baadae majani mengine hunyauka na kudondoka kuzunguka shina la mgomba. Ndizi iliyoshambuliwa na ugonjwa huu huwa na madoadoa kwa ndani kama inavyoonekana.

 

NINI CHA KUFANYA
 Tumia aina zinazostahimili ugonjwa huu kama zipo.
 Tumia vichipukizi visivyo na ugonjwa huu.
 Ondoa migomba yote iliyoathirika na uiteketeze.
UGONJWA YA VIRUSI
BUNCHY TOP

Ugonjwa huu huweza kutokea wakati wowote wa ukuaji wa migomba.
Huenezwa na aphids na hushambulia hata vichipukizi. Mimea iliyoathiriwa huweza kushindwa kuzaa na ama ikizaa huzaa ndizi ndogo na ngumu.
NINI CHA KUFANYA
 Tumia vichipukizi visivyo na ugonjwa huu.
 Ondoa kabisa migomba yenye dalili za ugonjwa huu, pamoja na viazi vyake na teketeza.
 Thibiti aphids ambao ndio waenezaji.
MAGOJWA YA FANGASI
MICHIRIZI MEUSI (Black leaf streak )
Ni ugonjwa hatari sana wa migomba na unashambulia majani ya ndizi. Vimelea vya ugonjwa huu husambazwa na upepo na hukua vizuri kwenye hali ya unyevunyevu. Sehemu za pembezoni mwa jani huanza kukauka na hatimaye jani zima hufa.
Ugonjwa huu husababisha mazao duni na ndizi kuiva kabla ya kukomaa.


 
NINI CHA KUFANYA
 Ondoa na haribu kwa moto majani yaliyoathirika. Vinginevyo ondoa majani yaliyoathirika na weka mbali na shamba la migomba ama fukia chini sana.
 Epuka kumwagilia majani kwa juu, tunashauriwa kumwaga maji kwenye shina.
Epuka kupanda kwenye msongamano.
UGONJWA WA PANAMA (Fusarium wilt).
Huu ni ugojwa utokanao na fangasi waishio ardhini na hushambulia mizizi na kuziba njia za kusafirisha maji na madini kwenye mmea, kwahiyo mmea hunyauka na kufa. Majani huwa ya njano na hatimaye kukauka
NINI CHA KUFANYA
 Tumia migomba inayostahimili huu ugonjwa kama Dwarf Cavendish.
 Kusafisha shamba na Kuondoa visiki vilivyo shambani huweza kusaidia kupunguza ugonjwa huu.
 Majivu yanaweza kuwekwa kuzunguka
(UGONJWA WA MUOZO SIGARA) THE CIGAR END ROT DISEASE
Ugojwa huu unaweza kuathiri matunda ya ndizi yaliyoiva, na kusababisha kuoza na kukauka kwa ndizi kuanzia mwisho. Palipoathirika huwa na ungaunga kama majivu.Huonekana kama sigara iliyozimwa. Ugojwa huweza kuendelea hadi wakati wa kuhifadhi ama kusafirisha. Huweza kuharibu mkungu mzima na kusababisha hasara kubwa.
NINI CHA KUFANYA
 Zingatia usafi shambani.
 Epuka kujeruhi ndizi na usikate ua la ndizi wiki 8-11 tangu izae.
ANTHRAC NOSE
Huu ni ugonjwa unaoshambulia ndizi baada ya kuvuna, hasahasa wakati wa kuhifadhi na kusafirisha. Madoa madogo ya kahawia ama jeusi huanza kutokea kwenye ndizi. Mara nyingi hushanbulia ndizi zilizokomaa vizuri. Hushamiri vizuri kukiwa na hali ya unyevunyevu
Anthracnose Anthracnose fruit rot on banana


NINI CHA KUFANYA
 Hakikisha usafi shambani
 Punguza kujeruhi ndizi.
 Ziweke ndizi kwenye maji ya moto 50° kwa dakika 5.
 Kunyuzia mafuta ya jatrofa yaliyochanganywa na maji huzuiya anthracnose hadi siku 12