Wednesday, April 1, 2015

Sugar production -Tanzania

Sugar is a sweet crystalline substance, which may be derived from the juices of various plants. Chemically, the basis of sugar is sucrose, one of a group of soluble carbohydrates, which are important dietary sources of energy in the human diet. It can be obtained from trees, including the maple and certain palms, but virtually all manufactured sugar comes from two plants sugar beet (Beta vulgaris) and sugar cane, a giant perennial grass of the genus Saccharum. Sugar cane, found in tropical areas, grows to a height of up to 5 metres or more In Tanzania sugar is produced from Sugar cane. Sugar cane in Tanzania is primarily grown in four estates, namely Kilombero Sugar Company, Mtibwa Sugar Estate, Tanganyika Planting Company and Kagera Sugar Limited. Apart from sugar cane grown by the estates, other sugar cane is grown by out growers who are found at Kilombero and Mtibwa estates and there contribution has gradually increased in recent years. In general the annual sugar production in Tanzania is about 115,000 tonnes per annum while the estimated demand of sugar is estimated at 300,000 tonnes. Tanzania imports about 200,000 tonnes per annum to offset the shortfall. Sugar Production

Monday, March 30, 2015

Eneo linalofaa kwa ufugaji

Eneo linalofaa kwa ufugaji
Baadhi ya maeneo yanayofaa ni yale mashamba ya mpunga, na maeneo yaliyo karibu na vyanzo vya
maji. Zifuatazo ni sifa za maeneo yanayofaa:
1. Udongo: Mfinyanzi husaidia kupunguza gharama za ujenzi wa bwawa na maji kwakuwa
linaweza kutuamisha maji na kuruhusu maji yasipotee. Likiwa la kichanga bwawa ni lazima
lijengewe au kuwekwa nylon sheet ili kuzuia upotevu wa maji. Unaweza ukahamisha udongo
wa mfinyanzi kutoka sehemu moja hadi nyingine ili kuzuia upotevu wa maji (muone
mtaalamu kwa ushauri zaidi juu ya mbinu ya kuhamisha udongo)
2. Chanzo cha maji ya uhakika
Eneo liwe na maji ya uhakika. Vyanzo vya maji ni kama vile mito, bahai, maziwa, chem
chem., kisima, maji ya dawasco na mvua. Maji yasiwe na kemikali hatarishi kwa viumbe.
3. Miundombinu ya barabara: Inasaidia kwa ajili ya usafirishaji wa bidhaa na samaki wakati wa
kuvuna.
4. Eneo lisiwe na historia ya mafuriko ili kuzuia athari za mafuriko kwa miundombinu yako.
Utatumia gharama nyingi katika kuimarisha miundombinu yako.Jamii/aina ya samaki
5. Eneo lenye mwinuko wa wastani husaidia katika ujenzi wa bwawa.
6. Miundombinu ya umeme ni sifa ya ziada hususan kwa mkulima wa kati na wajuu kwa ajili ya
kutumika katika kuendesha visambaza hewa.
7. Ulinzi muhimu
Note: Aina ya eneo lako ndilo linaweza kukufanya uchague muundombinu gani wa kufugia
utumie
Aina ya samaki unaoweza kufuga Tanzania kwa sasa
Maji baridi
Sato/perege, Kambale, Kambamiti wa maji baridi na Trout (maeneo ya baridi kama vile
Iringa, Kilimanjaro Arusha na Mbeya) na samaki wa mapambo.
Maji bahari
Kambamiti wa maji bahari, mwatiko, chewa, kaa, chaza wa lulu
Upatikanaji wa Vifaranga vya samaki husika
Vyanzo vya vifaranga ni kutoka katika mito, bahari, maziwa na wale wa kuzalishwa katika
vituo vya kuzalishia vifaranga.
Sato na Kambale
Vituo vya serikali Utapata sato wa kike na kiume mixed sex). Kingolwira –Morogoro, Luhira-
Songea, Mbegani-Bagamoyo . Kifaranga huuzwa Tsh. 50-100 kwa kifaranga.
Vituo binafsi kama vile Faith aquaculture-Kibamba (DSM) (utapata monosex sato), Peramiho-
Songea (mixed sex). Monosex huuzwa Tsh. 200 kwa kifaranga, na mixed ni 100 kwa
kifaranga.
Trout
Mayai huagizwa toka Marekani, Israel
Kambamiti wa baharini
Alphakrust –Mafia.
Chakula cha samaki
Chakula cha asili
Hurutubishwa kwa mbolea ya wanyama kama vile kuku, ngombe, mbuzi nk. Kwa kiwango
cha 1000kg/ha. Mbolea ya kuku ni kali hivyo unaweza punguza ikawa 250-500kg/ha.
Chakula cha kutengeneza
Samaki huitaji protein ili akuwe na kila samaki ana mahitaji yake hivyo ni species specific.
Formula zipo kwa wale wanaotaka kutengeneza. Tanzania hakuna kiwanda
kinachotengeneza. Ingredients zake ni kama vile dagaa, pumba, soya, unga wa ngano, unga
wa muhongo nk.
Uvunaji
Kwa kawaida ni miezi 4-6 amabapo unapata 250-400g kulingana na ulishaji wako. Kwa
prawns ni miezi 3-6 wanafikia 30-50g ambayo ni ukubwa wa soko.
Tathmini ya uchumi
Perege/sato
Mfano:
Ukubwa wa bwawa ni 20m by 30m= 600 mita za mraba
Idadi ya samaki (7 kwa mita ya mraba) kwa monosex tu= 600 x 7=4200 fish
Uzito hadi kuvuna (4-6months)- 250g= 4200 x 250g= 1050kg (Nimesha convert gram to kg)
Bei kwa kilo ni 6000-8000 kulingana na mahali= 6milion-8milion.

Vodacom Foundation yakabidhi msaada wa Umeme Jua kwa wahanga wa mvua Kahama

Mkuu wa Vodacom Tanzania,Kanda ya Tanganyika George Venanty(kushoto) na Meneja Masoko wa Kampuni ya Associate AEG Winnie Nyamubi(kulia) wakielezea matumizi ya Umeme Jua”Solar Power” wakati wakukabidhi msaada huo uliotolewa na Vodacom Foundation kwa wahanga wa maafa ya mvua kwenye kijiji cha mwakata wilayani Kahama Mkoani Shinyanga mwishoni mwa wiki.

AIRTEL YAKARABATI DARASA SHULE YA MSINGI USHINDI


Mkurugenzi Mkuu wa Airtel Tanzania, Sunil Colaso (wa tatu kulia), akizungumza kabla ya kukabidhi Darasa la Chekechea lililokarabatiwa kwa udhamini wa Wafanyakazi wa Airtel, kama sehemu ya huduma kwa jamii, katika Shule ya Msingi Ushindi iliyopo Mikocheni ‘B’, jijini Dar es Salaam jana. Kutoka (kulia) ni Mwenyekiti wa Shule hiyo, Jumanne Konara na Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Elias Katunzi, Meneja wa Huduma kwa Jamii wa Airtel, Hawa Bayumi (kushoto) na baadhi ya wafanyakazi wa kampuni hiyo.