Friday, January 16, 2015

JINSI YA KUMTAMBUA KUKU ANAYE UMWA NA KUKU MWENYE AFYA


TOFAUTI ZA MUONEKANO YA KUKU MWENYW AFYA NA KUKU MGONJWA

KUKU MWENYE AFYA
    Macho na sura angavu
     Hupenda kula na kunywa maji
     Pua zilizo safi, upanga na undu mwekundu, manyoya
     laini na yaliyopangika vizuri
     Hupumua kwa utulivu
     Sehemu ya kutolea haja huwa kavu
     Kinyesi kikavu, cheupe na kisicho na rangi
     Hutaga mayai kawaida

 KUKU ASIYE KUWA NA AFYA NZURI(MGONJWA)
           Huonekana mchovu na dhaifu
           Hula na kunywa kidogo au zaidi ya kawaida
           Hutoa kamasi puani, ute na matongotongo; manyoya
           yaliyovurugika
           Hupumua kwa shida na kwa sauti
           Sehemu ya kutolea haja inakuwa na unyevunyevu na
           kinyesi kuganda
           Huharisha, kinyesi huwa na damu au minyoo
           Hutaga mayai machache au husimama kutaga kabisa
           Huwa na tabia ya kujitenga na wenzake katika kundi

No comments:

Post a Comment