Monday, May 13, 2013

Zao la korosho kuendelea kuzama kwa sera mbovu

 

Dar es Salaam. Imeelezwa kwamba wakulima wa Korosho nchini wataendelea kupata mapato duni hadi hapo Serikali itakaposaidia uwekezaji wa viwanda vya ubanguaji wa korosho katika mikoa inayolima zao hilo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti ya Kuondoa Umaskini (Repoa), Profesa Samwel Wangwe alisema juzi kwamba uuzaji wa korosho zisizobanguliwa nje ya nchi ni hasara kwa wakulima.
Profesa Wangwe alisema hayo wakati wa majadiliano ya utafiti unaolinganisha ufanisi wa zao hilo kati ya Tanzania na Vietnam uliofanywa na Dk Blandina Kilama wa Repoa.
“Tunahitaji kuongeza thamani ya zao hili kwa kujenga viwanda vya kisasa vya kubangua korosho  ili tuweze kuuza kwa thamani itatayowanufaisha wakulima,” alisema Profesa Wangwe.
Wakati Profesa Wangwe akisema hayo, viwanda vya kubangua korosho ambavyo Serikali ilibinafsisha kwa watu binafsi, vimegeuzwa maghala ya kuhifadhia mazao na kusababisha korosho kuuzwa zikiwa hazijabanguliwa.
Kwa upande wake, Dk Kilama alisema katika utafiti wake kwamba ingawa Tanzania ilianza kilimo cha korosho kabla ya Vietnam lakini nchi hiyo iko juu kiuzalishaji kuishinda Tanzania.
Alisema kinachowasaidia ni kwamba mbali na Serikali hiyo kuweka sera bora za kilimo, pia kuna viwanda vingi vya kubangua korosho hali inayowafanya waongeze thamani ya zao hilo.
“Hata Bodi ya Korosho ya Vietnam inajumuisha wataalamu wa kilimo, wakulima na wabanguaji jambo ambalo ni tofauti hapa kwetu ambapo bodi inaweza kuwa na watu ambao siyo wadau wa korosho,” alisema na kuongeza kwamba Tanzania imeshuka kwa kiasi cha kutisha katika uzalishaji zao


No comments:

Post a Comment