Thursday, May 9, 2013

Serikali yashauriwa kuboresha kilimo cha mpunga

 https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEja5ruF1cI73v7-vjmKbFZvJGHMjUWNDco2jXgHKFoCWX-u_w0HjwlRH8abF4vHrJilVQj0cS_G_a1Gw8A35kGMAY0pmVgyFk4fXCyI-AXxklvQ-y0goN3Kc4HGPQ9jjVaIqZP2WpFDfRs/s1600/AA_3356.JPG
SERIKALI imeshauriwa kutumia fedha zinazonunulia mchele toka nje ya nchi kuboresha kilimo cha mpunga hapa nchini. Ushauri huo ulitolewa na Meneja wa Mradi wa Shirika linalojihusisha na Shughuli za Maendeleo Vijijini (RLDC), Francis Massawe.

Alisema Serikali imekuwa ikitumia fedha nyingi kununua mchele toka nje ya nchi hivyo ni vyema fedha hizo ingezitumia kutoa elimu kwa wakulima namna ya kuboresha kilimo hicho waongeze vipato vyao.


“Ni vyema Serikali ikaliangalia suala hili kwa kina ili kuweza kuwasaidia wakulima wetu hapa nchini kwa lengo la kuwawezesha kujikwamua na umasikini,” alisema Massawe.

Alisema wakati umefika sasa kwa wakulima kupatiwa mikopo na taasisi za fedha waweze kutumia mbegu bora na pembejeo za kilimo za kisasa kuendana na mazingira ya kilimo bora na cha kisasa.

Aalisema wamejipanga kuhakikisha uzalishaji wa mazao ya vyakula unaongezeka waweze kuuza nje ya nchi na kuongeza Pato la Taifa.

Alisema wamekuwa wakiwawezesha wakulima na wafugaji kwa kuwapa elimu bora kuhusiana na kilimo na ufugaji ikiwemo kuwapa mikopo.

Alisema mkakati wao ni kuhakikisha wanaongeza uzalishaji wa mazao mbalimbali ya vyakula kuuza nje ya nchi na wala si kuagiza mazao toka nje ya nchi
.

No comments:

Post a Comment