Saturday, February 14, 2015

WAJUMBE WA ALAT RUVUMA WATEMBELEA KITUO CHA KILIMO NALIENDELE MKOANI MTWARA


Katibu tawala wa mkoa wa Mtwara,Yusuf Matumbo akizungumza na wajumbe wa jumuiya ya serikali za mitaa(Alat)mkoa wa Ruvumna wakati wa ziara ya wajumbe hao kutembelea mkoani humo kujifunza namna ya kilimo cha korosho na mazao mengine ya biashara.
Mtafiti wa zao la korosho kutoka kituo cha kilimo Naliendele mkoani Mtwara,Ramadhan Bashiru (kulia) akiwaonesha mche wa korosho baadhi ya wajumbe wa jumuiya ya serikali za mitaa(Alat)wa mkoa wa Ruvuma walipotembelea katika kituo hicho kujifunza kilimo cha kilimo bora cha korosho hivi karibuni.
Wajumbe wa jumuiya ya serikali za mitaa(Alat)mkoa wa Ruvuma wakimsikilimza mtaalamu wa kilimo cha korosho kutoka kituo cha kilimo cha Naliendele mkoani Mtwara,Bi Joan Kasuga (kushoto) juu ya kilimo bora cha korosho,kufuatia ziara ya wajumbe hao kutembelea kituo hicho kwa lemngo la kujifunza kilimo bora cha zao hilo.
Mtafiti wa zao la muhogo kutoka kituo cha kilimo cha Naliendele mkoani Mtwara Abdala Nyapuka (kulia) akiwaonesha wajumbe wa Alat mkoa wa Ruvuma aina moja wapo ya muhogo unaozalishwa katika kituo hicho.kufuatia ziara ya mafunzo ya wajumbe hao mkoani Mtwara kujifunza namna ya kilimo bora cha korosho na mazao mengine ya biashara.
Katibu wa jumuiya za serikali za mitaa(Alat)mkoa wa Ruvuma Musa Zungiza akiazungumza na wajumbe wa jumuiya hiyo juzi katika u8kumbiu wa halmashauri ya wilaya Tunduru mkoani humo,kushoto ni mwenyekiti wa jumuiya hiyo Oddo Mwisho.
Mwenyekiti wa jumuiya ya serikali za mitaa(Alat) mkoa wa Ruvuma Oddo Mwisho akiangali chupa yenye wadudu waharibifu wa korosho katika kituo cha kilimo cha Naliendele mkoani Mtwara,alipoongoza ujumbe wa wajumbe hao kutembelea mkoani Mtwara hivi karibuni.Picha na Muhidin Amri wa Globu ya Jamii,Ruvuma.
Chanzo: Michuzi Blog

No comments:

Post a Comment