Thursday, February 12, 2015

WASIRA AAGIZA WADAU WA SUKARA KUINGIZA SOKONI BIDHAA HIYO BADALA YA KUIFUNGIA GHALANI

Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika Mh Stephen Masatu Wasira amekutana na wadau wa sukari na kutoa tamko la serikali kuhusiana na kupanda kwa sukari hapa Nchini Mh Wasira amewaangiza wazalishaji na wafanya biashara wa sukari hapa Nchini kuingiza sukari badala ya kuiweka kwenye maghala ili kushusha bei ya bidhaa hiyo muhimu Agizo hilo la Wazili limekuja muda mfupi baada ya kupanda ghafla kwa bei ya sukari kutoka shilingi 1700/= iliyo kuwa ikiuzwa awali hadi shilingi 3000/= kwa kilo


Waziri wa kilimo Chakula na ushirikiano Mh Stephen Wasira na Naibu wake (kushoto) Mh Godfrey zambi , Bi Sophia Kaduma katibu mkuu kulia na Dkt Yamungu kayandabila (kushoto) wakifuatilia kwa makini mjadala baina yao na wazalishaji na wafanya biashara wa sukari katika mkutano uliofanyika katika ukumbi wa kilimo

No comments:

Post a Comment