Thursday, February 26, 2015

Wakazi wa arusha wahimizwa kulima mazao yanayohimili ukame

Mkuu wa mkoa wa ARUSHA,FELIX NTIBENDA
Mkuu wa mkoa wa ARUSHA,FELIX NTIBENDA amewaagiza wakazi wa wilaya ya ARUMERU mkoani ARUSHA,kulima mazao yanayostahimili ukame ili kuondokana na tatizo la upungufu wa chakula unajitokeza kutokana na uhaba wa mvua.

Akizungumza katika kikao cha baraza la madiwani cha Halmashauri ya MERU,mkuu wa mkoa amesema kuanzia sasa hakuna maafisa kilimo kukaa ofisini na badala yake watembelee mashamba ya wakulima ili kuona tatizo linalowakabili katika kilimo.

No comments:

Post a Comment