Friday, March 20, 2015

BRN yaanza kuwanufaisha wakulima wa umwagiliaji


Wakulima katika skimu 78 za umwagiliaji nchini, wameanza kunufaika na Mpango wa matokeo makubwa sasa kwaajili ya kilimo shadidi cha zao la mpunga kwa kulima eneo dogo na kuvuna mazao mengi. 

Mratibu wa kilimo shadidi kutoka Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika, Dkt KISSA KAJIGILI amesema shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Maendeleo - UNDP kwa kushirikiana na serikali wamedhamiria kuboresha kilimo kupitia kilimo shadidi. 

Tayari kilimo shadidi kimekuwa mkombozi kwa baadhi ya nchi barani afrika ambazo wakulima wan chi hizo,ikiwemo nchi za madagaska, Burkinafasso, Mali na zingine nyingi,nchini hapa wakulima katika skimu za umwagiliaji mkoani Morogoro, Arusha na hatimaye mkoani Mbeya,tayari wamefikiwa.

No comments:

Post a Comment