Thursday, March 19, 2015

Kikwete ataka kilimo kutumia teknolojia mpya

Na Ibrahim Yamola, Mwananchi

Posted  Jumatano,Januari29  2014  saa 24:0 AM
KWA UFUPI
Alisema uhifadhi wa vyakula katika maghala hauridhishi, kutokana na asilimia 30 ya mazao yanayohifadhiwa huharibika jambo ambalo linaweza kuepukika likitafutiwa ufumbuzi.Rais Kikwete alisema bila kuviwezesha vituo vya utafiti na kuwatumia wataalamu wengi wa kilimo kama mabwana na mabibishamba, sekta hiyo haitapiga hatua.
Alikuwa akifungua mkutano wa wadau wa kilimo na biashara kutoka nchi mbalimbali za Afrika na Ulaya, jana.
Alisema uhifadhi wa vyakula katika maghala hauridhishi, kutokana na asilimia 30 ya mazao yanayohifadhiwa huharibika jambo ambalo linaweza kuepukika likitafutiwa ufumbuzi.
“Tunatakiwa kutumia ugunduzi wa teknolojia mpya zinazogunduliwa ndani na nje ya nchi kwa vitendo, ili kusaidia kuboresha kilimo nchini jambo ambalo linawezekana tukiamua hasa kwa kushirikiana na wadau wengine,” alisema Rais Kikwete.
Alisema wakulima wengi hususan wadogo wanatakiwa kupewa elimu jinsi ya kulima mazao ambayo yanaendana na udongo wa eneo husika, kazi ambayo inatakiwa kufanywa na mabwana na mabibishamba na wadau wa kilimo.
“Pia, rasilimali fedha na watu katika vituo vyetu vya utafiti wa kilimo vinahitaji kuongezewa nguvu, ili kufanya tafiti nyingi na zitakazoweza kusaidia kutatua matatizo,” alisema.
yanayowakumba wakulima wengi.”

No comments:

Post a Comment