Thursday, February 27, 2014

WAJASIRIAMALI WAPATA MAFUNZO USINDIKAJI MUHOGO




WAJASIRIAMALI 16 kutoka Mikoa ya Mwanza, Pwani na Kagera wamepata elimu ya usindikaji wa zao la muhogo na viwango vinavyozingatia ubora unaokubalika katika nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EA C).

Akizungumza na waandishi wa habari hivi karibuni, wilayani Misungwi baada ya mafunzo hayo, mshauri wa usindikaji na masoko wa IITA Dkt. Gabriel Nduguru, alisema wakulima wasindikaji wa zao la muhogo, hawakuwa na elimu ya kutosha kuhusu viwango na ubora wa bidhaa zao.

 Alisema kuwa mafunzo hayo kwa wasindikaji hao, yalitolewa na Taasisi ya Kimataifa ya Kilimo Alisema wanafanya utafiti wa mazao na kusaidia kuainisha viwango vinavyotumika kwa nchi za EAC, baada ya kuridhiwa na mawaziri wa nchi za Jumuiya hiyo.

Alisema wananchi watafahamu viwango vya ubora baada ya kuwapa mafunzo ya usindikaji na watazalisha chakula chenye ubora na kuuza katika masoko ya uhakika na watajiongezea kipato .

cha Kitropiki (IITA) kwa kushirikiana na Shirika la Viwango nchini (TBS ).
Alisema IITA ilifanya utafiti na kubaini changamoto hiyo kwa wasindikaji wengi wa zao la muhogo, hivyo ikaamua kutoa elimu inayohusu ubora na viwango kwa wasindikaji hao ili kuwawezesha kupata masoko ya uhakika.

"Wakulima na wasindikaji hao hawakuwa na elimu, hivyo bidhaa zao hazikuwa bora na salama na zilitishia afya za walaji.Baada ya kubaini hilo tukaona tuwafundishe jinsi ya kusindika muhogo salama kwa kuzingatia viwango vya ubora kulingana na mahitaji ya walaji," alisema Dkt. Ndunguru.

Dkt. Ndunguru alisema changamoto kubwa kwa wasindikaji zao la muhogo, ni vifungashio na mitambo ya kisasa kwani ni kiwanda kimoja tu ambacho hakitoshelezi mahitaji.
 


No comments:

Post a Comment