Friday, March 7, 2014

KENYA KUANZISHA ENEO LA KWANZA LA BIASHARA HURIA




Serikali ya Kenya tarehe 13 ilifanya mkutano wa baraza la mawaziri ikiidhinisha kuanzisha eneo la kwanza la biashara huria mjini Mombasa. 

Mkutano huo ulioongozwa na rais Uhuru Kenyatta. Sababu ya kuidhinisha kuanzisha eneo la biashara huria ni kwamba serikali ya Kenya imetambua kuwa uchumi wa dunia unafufuka, na uchumi wa nchi za Afrika zilizoko kusini mwa jangwa la Sahara una mwelekeo mzuri, na mambo hayo yote yameonesha mustakabali mzuri wa uchumi wa Kenya. 

Mji wa Mombasa ni mji wa pili kwa ukubwa nchini Kenya, ni bandari kubwa zaidi nchini humo, pia ni kituo muhimu cha viwanda na biashara. Mji huo umeunganishwa na mji mkuu Nairobi kwa reli, barabara kuu na mabomba ya kusafirisha mafuta. Bandari ya Mombasa ina vifaa vya kisasa, ambayo inashughulikia uchukuzi wa baadhi ya bidhaa za Kenya, Uganda, Tanzania, Burundi na Rwanda. Bandari hii iko katikati ya pwani ya Afrika Mashariki. Hakuna bandari kubwa kaskazini yake hadi bahari nyekundu, na kusini yake kuna bandari ya Durban ya Afrika Kusini tu ambayo ina uwezo wa kushindana na bandari hii. Sababu zote hizi zimeweka mazingira mazuri ya kuanzisha eneo la kwanza la biashara huria mjini Mombasa. 

Licha ya Mombasa, serikali ya Kenya pia inapanga kuanzisha maeneo ya biashara huria katika miji ya Kisumu na Lamu. Hivi sasa imetenga ardhi kilomita 3,400 za mraba kwa ajili ya ujenzi wa maeneo ya biashara huria. Eneo la biashara huria la Mombasa litakuwa kilomita elfu 2000 za mraba, lile la Kisumu na lile la Lamu yote ni kilomita 700 za mraba. 

Taarifa zilizotolewa na serikali ya Kenya zinaonesha kuwa, ushuru wa bidhaa utafutwa katika maeneo hayo ya biashara huria, na hatua hii itaimarisha na kuboresha biashara kati ya nchi za Afrika Mashariki, ya Kati na Kusini. Pia Kenya inatazamiwa kuagiza bidhaa za nchi hizi moja kwa moja katika maeneo ya biashara huria badala ya kwenda Umoja wa Falme za Kiarabu, China na Japan.

No comments:

Post a Comment