Monday, December 3, 2012

Wakulima 40,000 Kiteto wabomolewa nyumba zao

WAKULIMA wapatao 40,000 waishio katika vijiji 11 vilivyoko katika Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto, mkoani Manyara, hawana mahala pa kuishi baada ya nyumba zao kubomolewa na uongozi wa halmashauri hiyo.
Wakizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti mwishoni mwa wiki wakazi hao ambao wanadaiwa kuvamia hifadhi ya mbuga ya Embloy Murtangosi, walisema wameonewa na kunyanyaswa kwa kuitwa wakimbizi kutokana na baadhi ya vigogo wa serikali kulitaka eneo hilo la hifadhi.Mmoja wa wakulima hao ambaye ni Mwenyekiti wa Kitongoji cha Leitimi, Majaliwa Mbaigwa, alisema wao ni wakazi wa wilaya ya Kiteto tangu mwaka 2003 na waliambiwa na halmashauri hiyo kusogea umbali wa kilomita mbili tu na si vinginevyo.
Alisema wamekuwa wakifanya shughuli zao za kilimo na kulipa ushuru wa halmashauri na kupatiwa risiti ikiwa ni pamoja na kuchangia shughuli za maendeleo kama ujenzi wa barabara, lakini cha kushangaza wanaitwa wakimbizi.
“Ajabu wameongeza eneo kutoka kilomita mbili hadi 20 na kutufanya sisi tuonekane tumevamia, jambo ambalo si halali,” alisema Mbaigwa.
Naye Anna Ngamia ambaye alikuwa akizungumza huku akilia, alisema kijiji cha Laitimi kipo toka mwaka 1985 bali ni hujuma ya wakubwa wenye hela ambao wanataka kuhodhi eneo hilo bila kujali utu na haki.
Kwa upande wake, Imamu wa Msikiti wa Laitimi, Hamisi Haji, alilaani bomoabomoa hiyo ambayo haikujali hata nyumba za ibada.

Thursday, November 29, 2012

Watanzania wahakikishiwa kutoporwa ardhi na wawekezaji

SERIKALI imewahakikishia Watanzania kwamba hakuna ardhi ya wanavijiji itakayochukuliwa kutoka kwao na kukabidhiwa wawekezaji kwa ajili ya miradi mikubwa ya kilimo.
Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Chrostopher Chiza, alitoa kauli hiyo jana alipozungumza na wanavijiji toka vijiji vya Kidunda, Mkurazi na Usungura katika Wilaya ya Kisarawe, mkoani Pwani.
Waziri Chiza alikuwa ameambatana na kundi la wawekezaji waliokwenda kuangalia eneo la hekari 63,000 lililotengwa kwa ajili ya kilimo cha mpunga na miwa katika eneo la Gwata mkoani hapa. Ziara hiyo ilikuwa ni moja ya ratiba ya mkutano mkubwa wa wawekezaji wa kilimo uliofanyika jijini Dar es Salaam.
“Kunyang’anya ardhi wananchi sio sera yetu hata kidogo. Hizo ni propaganda zinazoenezwa na baadhi ya watu kwa nia mbaya,” alisema.
Alisema sera ya serikali ni kufanya kila liwezekanalo kuhakikisha maisha ya Watanzania yanainuka na si vinginevyo na kwamba serikali imetayarisha mpango mzuri wa matumizi bora ya ardhi kwa maslahi ya nchi.
Katika siku za hivi karibuni kumekuwapo na madai kutoka taasisi na watu mbalimbali wanaodai maelfu ya ardhi ya wakazi asilia katika maeneo mbalimbali Afrika yanaporwa na kuuziwa au kukodishwa kwa wawekezaji wakubwa na hata serikali za nje ya bara hilo.
Mapema katika mkutano huo uliotayarishwa na Ofisi ya Waziri Mkuu kwa kushirikiana na Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) na kituo cha mpango maalum wa uendelezaji kilimo katika ukanda wa kusini mwa Tanzania (SAGCOT), Waziri Mkuu, Mizengo Pinda alisisitiza wawekezaji wote katika ukanda wa SAGCOT kupewa kipaumbele pale ambapo uwekezaji wao unalenga pia kushirikisha wakulima wadogowadogo.

Wednesday, November 28, 2012

How to Grow a Tomato Plant

Are you learning to grow your own sweet, juicy tomatoes? Luckily for you, tomato plants can grow almost anywhere, that is warm and a little damp. But as with most vegetation that produce a fruit, a little "tender, loving care" or TLC goes a long way. With adequate sunlight, water, and patience, you'll be greatly rewarded with a six foot tall tomato plant with big red juicy tomatoes! Tomatoes take a long time to grow so you must have great patience. That's all you need to do to get your tomato plant growing. Have fun growing!
 Steps
  1. Buy small tomato plants from a nearby nursery and transplant them to your garden for the first-time grower. More experienced growers will find it easy enough to start their own tomatoes from seed.

    ~ Begin to raise your own plants, if you wish, from seed, in a
    greenhouse or sunny window indoors about a month before you intend to set them out in the garden.

    ~ You can use fluorescent lights hanging a couple inches (5cm) above the planting flat and keep raising it as the plants grow--in a not well lighted room.Raise these plants until they are about 6 to 10 inches tall (15 to 25cm) for example and then transplant them when spring weather is appropriate for your zone.


    • Don't pay extra to buy the larger plants; there is not much reason, unless you are getting a "latish" start, to catch up.
  2. Get good first-time growers’ varieties including Better Boy, Creole, Big Boy, Early Girl, Brandywine, Celebrity, Lemon Boy, or just about any cherry or grape tomato variety.

    ~ Plant several varieties rather than all of one type -- this ensures a steady harvest.

  3. Grow two plants for each member of the family who will eat lots of tomatoes, as a rule of thumb. If you plan on canning tomatoes or making fresh and canned salsa, use up to four plants per person.

Your planting plot

  1. Choose a sunny spot to place the plants to transplant them. Place tomato plants in a site receiving full sun (7 hours or more daily). Tomatoes need lots of warm sunshine for optimum taste.

    ~ Caveat: In hot climates when the nights get to a low temperature of about 75°F (24°C), then most tomatoes "quit setting new fruit". The ones already set will grow great. But none will set when nights are very warm through the wee hours really near sunrise.


    ~ Don't wait more than a few days late to put them out past the recommended dates for your climate zone, or it may be too late (if there are such early warm/hot weather nights).

  2. Prepare the garden bed by adding lots of well rotted--not green--compost (5 to 8 pounds per square foot/25 to 40 kilograms per square meter) to the soil. Turn compost into the top 3 inches (6 to 8 cm). Tomatoes demand a growing medium rich in organic matter. If you don't make your own compost, use store-bought compost or composted manure available in the 40-pound bags.

Placing transplants

  1. Transplant the tomato deeply. Bury about 50 to 75% of the plant (especially for leggy plants, that became skinny in raising them before transplanting). It’s okay to bury some of its lower leaves. New roots will emerge along the buried stem, giving the plant a developmental boost; a new transplant needs to focus on root production.
  2. Give each plant about 1 gallon (about 4 litres) of warm water (about 80 degrees F/ 27 degrees C) within ten minutes of transplanting to avoid transplant shock.
  3. Space tomato plants 18 to 36 inches (45 to 90 cm) apart; space them half the suggested distance in warmer climates, especially if using tomato cages. The normal distance recommended is for plants allowed to bush out hugely on the ground, while planting closer together in cages allows the plants to shade each others fruit, helping prevent burn and allowing a sweeter flavor.
    • Don't forget to leave yourself enough space to get in between the plants to water, weed, and harvest. Those cute, little seedlings may not remain that way for long.

Watering

  1. Water in the first 7 to 10 days after transplanting at about 16 ounces (about 500 ml) of warm water per plant every day.
  2. Wait a week or two after transplanting, and then place a mulch of straw, dried grass, or pine needles to control weeds and keep the soil moist during dry weather. The mulch should be about an inch (2.5 cm) thick and surround at least a circle 12 inches (about 30 cm) in diameter around the stem. Pine needles are especially good for helping raise the acidity of the soil.

    ~ Caution: Do '
    not keep the soil continuously wet or "soggy". That will kill (smother) the roots and will cause a stem disease (fungus) especially once it is really warm/or hot weather.
  3. Drip or soaker hose watering is better than overhead, which can encourage diseases that tomatoes are particularly prone to.
  4. Space water out more after 10 days and ensure that plants are receiving 1 to 3 inches (2.5 cm to 7.6 cm) of rain weekly. If not, give each plant about 2 gallons (about 7.5 litres) per plant "per week", beginning by about the end of the second week after transplanting.
    • Water deeply 2 to 3 times weekly (so, water each plant with about .75 to 1 gallon each time (about 3 to 4 litres), increase water as the plants get larger and when weather is hotter.
    • It's okay in hot or dry weather to water even more frequently with larger volumes.

Using stakes and cages

  1. Consider using a tomato cage or a tall stake to support the tomato vine about 14 days after transplanting.
    • A stake should be at least 0.5 x 2 inches (1.3 x 5cm) boards and 6 to 8 feet (1.8 to 2.4 meters) long. Pound stakes about 12 to 24 inches (30 cm to 60 cm) deep, at least 2 inches (5 cm) away from the plant. Secure the plant to the stake using "loosely knotted double-loops" that won't strangle the plant. Stakes can be made of bamboo, scrap wood, electrical conduit, or iron bar.
    • While it is less common, "vining" type tomato plants can be tied onto a trellis or fence, like grapes, beans, squash, and other vining plants. This can produce especially large yields, but vining is less popular because tomato plants grow so large and bulky (some are called "indeterminate" but are not vines, and the third kind are "determinate" type are shrub-like plants).

      ~ A determinate tomato plant grows to a certain (determined), limited size and then stops or at least slows its growth greatly. An indeterminate plant keeps growing and spreading out.
    • A cage should be at least 48 inches (1.2 m) tall, even taller if you grow the plant well. Tying plants is unneeded. Some tomato plants can be more than six feet (1.8 m) tall in cages (you may need to stake and tie the cage to the stakes). Cages have a tendency to bend if the plants get heavy, and sometimes collapse in summer storms. Carefully pull leaves and secondary stems inside the cage as the plant grows.
  2. Make your own tomato cages, if you like. Get a roll of 4 feet height (1.25 M) "welded-wire" garden fencing 2" X 4" rectangular openings (5cm X 10cm) garden fencing with -- or 4" square openings (10cm) -- and soon you can make it double height, tied to more stakes, so wind will not knock them over as plants climb. Roll it into 18 inch wide (45cm) cylinders to make your own, larger cages. Cut and bend the wire ends around the uncut wires on the opposite end, making a circle. This type of cage needs strong stakes well tied for support.

Fertilizing

  1. Choose whether to use chemical fertilizers. Do not use lawn fertilizer. The ratio of minerals in lawn fertilizer is for growing stems and leaves. Look for a vegetable fertilizer which is for stimulating fruit. Tomatoes can grow very well organically, provided the soil is well enriched with organic matter. If you do use chemical fertilizers, try using half the recommended concentration per gallon (using package directions), but fertilize twice as often, in order to avoid the stress caused by the feast-famine of the longer fertilization gaps.
    • Over-fertilization can cause plants to grow too quickly, leaving them more susceptible to disease and insects.
    • Remember that your goal in growing tomatoes is fruit, not just leaves. Fertilizers, especially when used in excess, or the wrong kind may cause the plant to produce more leaves and foliage than fruit.
  2. Shake your plant poles or cages gently once or twice each week for about 5 seconds once flowering begins to promote pollination of the blossoms (from one flower to another). According to the National Gardening Association, shaking the tomato plant increases fruit production by more evenly distributing pollen.

Fruiting

  1. Watch for fruit to appear 45 to 90 (about 60) days after transplanting. Tomato plants usually have small, green fruit to start. Wait until the fruit is of good size with a bright, deep coloring: This means that the fruit is ripe and ready to pick. The texture of the fruit can also determine when it is ready to pick. Ripeness is usually determined by a slight softness. Be careful to only "palm the tomatoes"; do not squeeze with the finger tips and bruise the fruit.
    • Also, be careful of not allowing it to become overly ripe, which results in a very soft tomato.
    • Realize that birds, possums, raccoons and some dogs will take ripened tomatoes, corn and sweet green peppers, etc.
  2. Pick fruit earlier to ripen indoors if you like: Fruit may be picked any time after it starts changing to its ripe color and set on a sunny windowsill. This will reduce the chances of it rotting on the vine or being eaten by a bird or squirrel.
    • Tomatoes do, however, taste sweeter when ripened on the vine, so you need to balance risk of threats versus taste.

Protecting ripe fruit from "critters"

  1. Place a "zip-" of "snap-" seal sandwich type of bag over the nearly ripe fruit, very carefully, from the bottom up onto the stem to protect ripening tomatoes from predators.
  2. Close the bag from both sides at the top, above the fruit, coming near the stem, leaving about 1/4" (.6cm) on each side for air flow.
  3. Cut the lower corner for drainage and air flow. In hot weather, carefully punch more air holes, 1/2 inch slits (1.2cm), or smaller, will work.
    • Don't be disappointed by losing fruit to the animals; spend the time bagging it!
Another tip is to put red Christmas tree ornaments around the top of the tomato cage. The birds will peck at them, be confused and leave your tomatoes alone.

Monday, November 26, 2012

Wakulima watakiwa kuchangamkia fursa

WAZIRI wa Kilimo na Chakula, Injinia Christopher Chiza, amewataka wakulima na wafanyabiashara nchini kuchangamkia fursa mbalimbali zinazojitokeza katika sekta hiyo.
Akizungumza jijini Dar es Salaam leo wakati akiwaaga wakulima kutoka mikoa nane ya Tanzania Bara ambao wanakwenda Sudan kwa ajili ya maonyesho ya kilimo na warsha, Chiza alisema wakulima wengi wanatabia ya kuuza mazao yakiwa shambani, hali inayowafanya wasiendelee kimaisha.
Alisema katika maonesho hayo ya siku tano anatarajia wakulima watanufaika na mpango huo ikiwemo kukuza biashara ya kilimo na kupata fursa mbalimbali zinazohusiana na masuala ya kilimo.
Chiza alisema kuwa wakulima wanatakiwa wawe wajanja, kwani kwasasa watu wanaotoka nchi za nje wamekuwa wakisajili magari yao kwa namba za Tanzania ili wapate urahisi wa kusafirisha mazao wanayoyachukua nchini.
Naye mmoja wa wakulima hao, William Mbogo, alisema wanatarajia kupata soko, uzoefu utakaowaongezea tija katika kuzalisha mazao na kuonyesha bidhaa zao katika maonyesho hayo.
Jumla ya wakulima 11 kutoka Mikoa ya Iringa, Morogoro, Kilimanjaro, Katavi, Kagera, Arusha , Kigoma na Dodoma wanaondoka leo wakiambatana na Katibu Mkuu, Athuman Mfutakamba na Mkuu wa Wilaya ya Bahi, Betty Mkwasa.

Friday, November 23, 2012

MILONGE (moringa oleifera)

  Hii ni miti ambayo haiwi mikubwa sana, inakuwa na maua meupe na kisha hutoa mbegu ndogo zinazokuwa kwenye magamba marefu kama kisu. miti hii hustawi zaidi ukanda wa pwani wenye mvua kiasi na joto, hustawi zaidi kwenye udongo usiotuamisha maji na inaweza kustawi kwenye udongo usio na rutuba nyingi na inahimili ukame kwa kiasi kikubwa.

MATUMIZI
Majani yake huweza kupikwa kama mboga na kuliwa, pia yanaweza kuhifadhiwa kwa muda mrefu bila ya kuathiri ubora wake wa virutubisho (nutritional value) majani yake yanavirutubisho vingi kuliko vyakula vingi tulivyozoea mfano


Ina vitamin A nyingi zaidi ya karoti
Ina Calcium nyingi zaidi ya Maziwa
Ina madini ya chuma zaidi ya spinach
Ina vitamin C nyingi zaidi ya Machungwa
Ina madini na pottasium zaidi ya Ndizi
ina protein nyingi zaidi ya nyama na mayai



MATUMIZI MENGINE
Maganda ya mbegu zake yanaweza kutumika kutibu maji(water treatment)unachukua maji yako ambayo unahisi si salama, unachanganya na maganda ya mbegu zilizopondwa pondwa kiasi, unayaacha kwa muda yatuame kisha unayachuja na yanakuwa salama kwa matumizi


Mbegu za milonge zinaweza kutumika kama dawa ya kupunguza sukari mwilini kwa wagonjwa wa kisukari, unachukua mbegu mbili au tatu unazipasua na kuchukua kokwa ya ndani na kutafuna mara 3 kwa siku, matumizi yanaweza kuongezeka au kuzidi kutegemeana na hali ya mgonjwa

Picha hapo chini inaonyesha mbegu za mlonge juu na kulia kwake ni baada ya kupasuliwa na kupata kokwa ya ndani (ambayo ni dawa ya kupunguza sukari mwilini), funguo imewekwa ili kujua ukubwa halisi wa mbegu


Sehemu yoyote ya mmea kama majani, magamba, mizizi, au maua yakipondwa pondwa na kupakwa kwenye sehemu yenye uvimbe ni dawa tosha ya kupunguza hali hiyo, pia dawa hii inauwezo mkubwa wa kupunguza sumu kama umeng'atwa na wadudu kama nyuki, manyigu/dondola, siafu, tandu, nge nk

Mbegu zake zinatoa mafuta (40%) yanayojulikana kama BEN OIL, ambayo hutumika kulainishia mitambo maalum kama saa za ukutani, pia mafuta haya ni dawa ya upele na harara

Wednesday, November 21, 2012

KILIMO CHA MATIKITI MAJI - watermelon

ili kulima matikiti maji, inakubidi uwe na sehemu ya kutosha, yenye jua la kutosha, maji mengi na ardhi yenye rutuba ya kutosha, matikiti maji hukua haraka kama mimea mimgine ya jamii yake itambaayo mfano Matango, maboga na maskwash.
Kwa mtu ambaye anaanza kilimo yatampa tabu kidogo tofauti na Yule ambaye ana ujuzi kidogo na mambo ya kilimo kwa sababu yanahitaji umakini kiasi.

HALI YA HEWA
Mimea hii haihimili hali ya joto kali sana, mvua nyingi na udongo unaotuamisha maji, magonjwa ya fangasi na wadudu waharibifu, inastawi vizuri kwenye ukanda wa pwani na miinuko kidogo kama DSM,Tanga, Morogoro, Mtwara, lindi na Pwani ambapo kuna jua la kutosha. Muda mzuri wa kupanda ni kipindi cha kipupwe mwezi machi mpaka septemba .

UPANDAJI
Panda kwa kutumia Mbegu zinazouzwa madukani, ukitumia Mbegu kutoka kwenye tikiti ulilonunua linaweza likawa ni hybrid na matokeo yake matikiti yatakayozaliwa hayatakuwa bora kwa sababu yatakuwa ni kizazi cha pili (F2)
Panda Mbegu yako moja kwa moja kwenye shamba, usinunue miche au kupanda Mbegu kwenye mifuko ya plastiki halafu ndo uhamishie shambani, panda Mbegu mbili sentimeta 2 chini ya udongo kwa umbali wa sentimeta 30 kutoka shina hadi shina na mita 2 - 3 kutoka mstari hadi mstari, baada ya siku chache Mbegu zitaanza kuota, baada ya kama wiki 2 katika Mbegu mbili ulizopanda kata moja na uache ule mche wenye afya zaidi, angalizo using’oe mche bali ukate ili kuzuia kusumbua mizizi ya mche uliobaki.
Unaweza kupandishia udongo kwenye mashina na hii itasaidia kupunguza maji yasituame kwenye mimea yako, pia unaweza kuweka samadi badala ya kupandishia udongo ukiwa na nia ileile ya kuzuia maji yasituame na kuongeza rutuba.
Kama una sehemu ndogo ya shamba unaweza kuyawekea matikiti waya wa kutambalia, ila inabidi uwe imara kwa sababu ya kuhimili uzito wa matunda yenyewe, na wakati wa kuanza kutambaa kwenye waya ni lazima uifundishe mimea kwa kuielekezea kwenye waya na kufungia

MCHE ULIOCHIPUA


UANGALIZI
Miche ikiwa imetambaa kiasi unaweza kuweka matandazo kwenye udongo ili kuzuia upotevu wa unyevu, unaweza kuweka samadi au mbolea za viwandani, mimea ikiwa midogo tumia zaidi mbolea zenye nitrojen na utumie zaidi mbolea za potasiam mara baada ya maua kutokeza hadi matunda kukomaa, matawi yakifikia urefu wa mita 2 kata mbele ilikuruhusu kutoa matawi na hivyo kupata maua mengi zaidi hatimaye mavuno zaidi

MAUA NA MATUNDA
Matikiti hutoa maua dume na jike kwenye tawi moja, maua dume ambayo ni madogo zadi hutoka kwanza yakifuatiwa na maua jike ambayo ni makubwa zaidi, usipoona maua dume na jike kuna tatizo mfano maji kidogo yalimwagiliwa, upungufu wa viritubisho kwenye udongo, hali ya hewa ni joto/baridi sana n.k
Uchavushaji kwenye matikiti hufanyika na wadudu, kama huwaoni wakifanya kazi yao unaweza kufanya mwenyewe, muda mzuri ni wa asubuhi, unakata maua dume kwa kisu na kufanya uchavushaji kwenye maua jike, maua jike ya mwanzo kwenye tawi ndiyo yenye ukuaji bora zaidi, unaweza kukata tawi lisiendelee kukua baada ya matunda kutokeza hii husababisha kuwa na matunda makubwa zaidi

UCHAVUSHAJI KWA MKONO


UVUNAJI MATIKITI
Ili kujua matikiti yamekomaa inahitaji ujuzi kidogo, upande wa chini wa tunda huanza kuwa na rangi ya njano, pia kikonyo juu ya tunda hukauka kabisa na kuwa kijivu, ila njia nzuri ni kuyapiga kwa kiganja na kusikiliza mlio wake kama tunavyofanya kwenye mafenesi, hii nayo ni shule nyingine. Tumia kisu wakati wa kuvuna matikiti, yabebwe na kuhifadhiwa vizuri kwenye makasha tayari kuuzwa au kwa matumizi binafsi


MAGONJWA NA WADUDU
Wadudu wa matikiti wako wanaoshambulia majani na maua, na wengine hushambulia matunda , pia kuna magonjwa ya fangasi ambayo hushambulia mimea, ili kujua dawa za magonjwa ni vizuri kuchukua sampuli na kwenda nayo kwenye duka la dawa na pembejeo za kilimo ili kupata dawa sahihi, dawa aina ya KARATE itasaidia kuua wadudu wa majani, maua na matunda na FUNGICIDE itasaidia kwa mashambulizi ya fangasi

Tuesday, November 20, 2012

UGONJWA WA NAGANA - Trypanosiasis

Ugonjwa huu hushambulia karibia mifugo yote na pia binadamu, kwa binadamu ugonjwa huu hujulikana kama malale. ugonjwa huu husababishwa na vijidudu vya protozoa vijulikanavyo kama Trypanosoma evansi na kusambazwa na mbung'o au ndorobo (glossina spp) vijidudu hivi vikimuingia mnyama vinatumia kiasi kingi cha sukari kwenye mwili wa  mnyama na  kuharibu seli nyekundu za damu na kusababisha  upungufu mkubwa wa damu kwa mnyama.

DALILI

1-
Ugonjwa huu kwa ng'ombe unaweza kuwa wa hatari na  hata  kuwa sugu na kuleta madhara makubwa ikiwamo kifo
2
-Joto la mnyama hupanda hadi kufikia sentigredi 39 - 41
3
-Mnyama hupata tabu kuona huku akitoa machozi mengi kama anayelia
4
-Uzalishaji wa maziwa hupungua ghafla kwa kiasi kikubwa
5
-Mnyama hupumua kwa tabu kwa kutumia nguvu
6
-Mnyama huonyesha kuchanganyikiwa akili, anaweza kutembea kwa mduara, kupiga piga kichwa kwenye mabanda au chochote na mnyama  huweza kupoteza fahamu
7
-Baadhi ya wanyama wajawazito huweza kutoa mimba, hii ni kwenye ile hali ya ugonjwa sugu ambao hushambulia pole pole
8
-Kuvimba kwa matezi
9
-Manyoya ya ng'ombe mgongoni wakati wa asubuhi yana kuwa yanang'aa kwa aina fulani jua likiwaka, ila inahitaji uonyeshwe na wataalam kwanza

NG'OMBE AINA YA N'DAMA



UCHUNGUZI

Maafisa ugani wa mifugo watachukua sampuli za damu kutoka kwenye mkia au sikio la mnyama na vijidudu kuonekana kwa darubini ya umeme mkali kabla ya damu kukauka, pia njia ya kimaabara ya GIEMSA itasaidia
kwa uchunguzi zaidi wa kimaabara wadudu wanaweza kupandikizwa kwenye sungura, panya na simbilisi/pimbi na baadae njia ya PCR, ELISA kutumika kuangalia vichochezi vya mwili

TIBA

Kwa mifugo kama ng'ombe, mbuzi, kondoo, jamii ya farasi, mbwa na paka dawa kama diminaphen, diminakel hutumika kutibu ugonjwa huu, kwa upande wa binadamu sifahamu dawa gani inatumika


KINGA

1
- Kuna njia ya kitaalam ijulikanayo kama sterile male technique, ambapo madume ya mbung'o hupigwa na mionzi ya gama na kushindwa kuzalisha yanapo panda, hii husaidia sana kwa sababu majike ya mbung'o hupandwa mara moja tu katika maisha yao wakati madume haya tasa huendelea kupanda majike tofauti tofauti
2-
Dawa zinazotumika kutibu ugonjwa huu zinaweza kukinga wanyama kama watapigwa kila baada ya miezi mitatu na mara 4 kwa mwaka
3-
Kuna jamii ya ng'ombe wanaojulikana kama N'DAMA ambao hupatikana Afrika ya magharibi, aina hii ya ng'ombe inastahimili sana ugonjwa huu

Friday, November 9, 2012

Used Tractors For Sale

Call: +255 777 086 076

Serikali yakamilisha utafiti misimu ya kilimo

SERIKALI imesema tayari imeshafanya utafiti wa misimu ya kilimo nchini na kutambulika kwa kanda za kilimo kulingana na kiasi cha mvua zinazonyesha.
Naibu Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Adam Malima, alibainisha hayo bungeni jana alipokuwa akijibu swali la mbunge wa Kasulu Vijijini, Agripina Buyogera (NCCR).
Katika swali lake, mbunge huyo alitaka kujua kama serikali haioni kuwa kuna haja ya kufanya utafiti wa misimu ya kilimo nchini, ili kupeleka mbolea ya ruzuku kwenye eneo husika katika muda muafaka.
Pia alitaka kujua ni kwa nini serikali isiwakopeshe wakulima mbolea hiyo, ili wawe nayo kwa wakati unaofaa kisha walipe baada ya kuuza mazao yao.
Akiendelea kujibu swali hilo, Malima alisema serikali imekuwa ikiratibu mahitaji halisi ya pembejeo za kilimo kwa kila wilaya ya mikoa kwa aina na kiasi.
“Baada ya kupokea mahitaji hayo serikali inawasiliana na makampuni ya pembejeo za kilimo, ili kuhakikisha uwepo wa pembejeo hizo katika maeneo yote hapa nchini kwa wakati kabla ya msimu huo kuanza,” alisema.
Alifafanua kuwa katika mwaka 2012/2013 mahitaji ya mbolea nchini yanakadiriwa kuwa tani 485,000.
Naibu waziri huyo alisema pamoja na mahitaji ya pembejeo kujulikana na kampuni, bado imekuwepo changamoto kwa baadhi ya mikoa kutofanya tathmini ya mahitaji halisi ya pembejeo katika maeneo yao na hivyo kuwahimiza kununua pembejeo mapema.
Aidha alisema changamoto hizo zimesababisha mawakala kukaa muda mrefu bila kuuza kutokana na wakulima kusubiri hadi mvua zinyeshe ndipo wanunue pembejeo.

Wednesday, November 7, 2012

Karoti inahitaji palizi ya mara kwa mara

Nimepanda karoti lakini sitaki kutumia dawa za viwandani kuua magugu mbali na kupalilia kwa mikono ni dawa gani za asili ninazoweza kutumia kuua magugu?

 
Magugu ni tatizo kubwa kwa karoti.  Hii ni kwa sababu ni zao linalokuwa taratibu na pia majani yake si mapana kuweza kuweka kivuli halikadhalika kupambana na wadudu. Magugu yasipodhibitiwa, yataathiri mavuno kwa kiasi kikubwa. Kwa bahati mbaya hakuna dawa za asili za kuulia magugu. Viini vyovyote vinavyoweza kutumika kuulia magugu ni wazi kuwa pia vinaweza kuathiri mazao pia. Hivyo, wakulima wanaofanya kilimo hai hufanya palizi kwa kutumia mikono au mashine.

Utunzaji wa karoti kwa njia ya kilimo hai, ni lazima uanze hata kabla ya wakati wa palizi. Panda karoti sehemu ambayo haina magugu mengi, na ambayo haija athiriwa sana na magugu kama vile mbaruku, mtunguja na nyasi.  Panda karoti kwenye sehemu uliyovuna mazao kama vile maboga, matango, tikiti, vitunguu au spinachi.  Baada ya kuvuna mazao yaliyotangulia, lima shamba lako na upande mbegu za karoti kwenye kitalu kisichokuwa na magugu.


Udongo ni lazima uvunjwe vizuri ili kuepusha hali itakayozuia mizizi kwenda chini ipasavyo. Karoti inahitaji udongo unaoweza kuruhusu kwenda chini vizuri, na unaopitisha maji vizuri, na wenye kiasi kikubwa cha malighafi zinazo oza (udongo mweusi). Utunzaji wa udongo kwa ajili ya kilimo hai, ni pamoja na kuweka mbolea vunde, pamoja na matandazo ambayo huongeza rutuba kwenye udongo kwa kiasi kikubwa. Hata hivyo wakati wa kupanda karoti, inabidi shamba lisiwe na mabaki ya mazao ambayo hayaozi kwa kuwa yanaweza kuathiri uotaji wa mbegu za karoti. Endapo dawa za kuulia magugu zitatumika, inabidi zitumike kabla ya kupanda kwa kuwa zinaweza kuuwa miche ya karoti pia.


Karoti zinahitaji kukua kwa haraka bila vipingamizi ili kuwa na majani pamoja na mizizi iliyo imara. Kupalilia mapema ni muhimu ili kuepuka upotevu wa mavuno, hasa katika wiki 10 za mwanzo toka kuota. Wakulima wa karoti hutumia jembe la mkono kupalilia kati ya mstari na mstari wa miche ya karoti. Lakini magugu yanayo ota katikati ya karoti ni lazima yang’olewe kwa mikono. Kuwa makini ili usijeruhi mimea! Kwa kawaida kupalilia kwa kutumia jembe la mkono hufanyika mara 3 katika kipindi chote cha ukuaji.

Bei mpya ya korosho yatangazwa



Bodi ya Korosho Tanzania imetangaza bei ya kununulia korosho kwa msimu wa 2012/ 2013 kwa wakulima.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Makamu Mwenyekiti wa bodi hiyo. Mudhihir Mudhihiri, alisema katika msimu huo kilo moja ya korosho kwa daraja la kwanza itakuwa inanunuliwa kwa Sh. 1200 wakati daraja la pili itanunuliwa kwa Sh. 960 kwa kilo.
Mudhihili alisema kwamba wadau wa korosho wamekubaliana kuwa wakulima watalipwa malipo yao kwa awamu mbili na malipo ya kwanza yatakuwa asilimia 70 ya bei dira na ya pili yatakuwa asilimia 30.
Aliongeza kuwa kwa mwaka huu zoezi la kukusanya korosho kwa wakulima ambalo hufanywa na vyama vya msingi kwa katika msimu wa manunuzi limechelewa kufanyika kutokana na vyama hivyo kuchelewa kupata mikopo ya kuviwezesha kulipia zao hilo kwa wakulima.
Mudhihili alisema licha ya msimu wa ununuzi wa zao hilo kufunguliwa tangu Septemba mwaka huu, lakini ununuzi huo umechelewa kuanza na hivyo kuwaathiri sana wakulima.
Aliongeza kuwa akutokana na tatizo hilo, Waziri wa Chakula, Ushirika na Masoko, Christopher Chiza, aliamua kuitisha kikao cha dharura kilichojumuisha Bodi ya Korosho, Bodi ya Leseni ya Maghala, Wizara ya Viwanda na Biashara, Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Benki ya CRDB, NMB na Benki ya Rasilimali (TIB) kwa ajili ya kuzungumzia mkanganyiko wa bei dira.

Tuesday, November 6, 2012

Vitunguu, kiungo cha chakula chenye faida kwa mkulima


Hapo awali kitungu kilikuwa ni zao lililokuwa linapatikana porini katika ukanda wa bahari ya Mediterania. Zao hili hulimwa katika nchi nyingi za magharibi, nchi za milima zilipo kaskazini mwa dunia, likwemo bara la Afrika. Vitunguu hustawi katika hali ya hewa ya jotoridi 13°C – 24°C, hali ya hewa inayofaa kwa kuotesha na kukuzia miche kwenye kitalu ni jotoridi 20°C – 25°C. Kwa kawaida vitunguu huhitaji kiasi cha joto nyuzi 20°C-25°C ili kuweza kustawi na kukua vizuri. Joto zaidi ya hapo hufanya vitunguu kudumaa na kutoweza kutengeneza viazi (bulbs).

Matumizi


Kitunguu hutumika kama kiungo cha kuongeza ladha kwenye chakula, na pia hutumika kama dawa ya kansa ya tumbo, vidonda na majipu.



Ustawi

Zao la vitunguu hustawi katika udongo wa tifu tifu wenye mbolea ya kutosha, ukiwa na uchachu wa udongo (PH) kiasi cha 6 – 6.8.  Udongo wa mfinyanzi haufai kwa zao la vitunguu kwa kuwa hauruhusu viazi vya vitunguu (bulbs) kutanuka.  Hivyo uwezekano wa kupata mazao ni mdogo. Pia udongo wa kichanga haufai kwa zao la kitunguu kwa kuwa hauna mbolea na hivyo vitunguu huwa vidogo sana, jambo ambalo ni vigumu kupata mazao yanayofaa kwa soko.
Zao la kitunguu huhitaji unyevu muda wote wa ukuaji wake. Zao hili lina mizizi mifupi hivyo linahitaji kumwagiliwa maji mara kwa mara.

Aina za vitunguu


Kuna aina mbili za vitunguu ambazo zimezoeleka:
• Vitunguu vya asili kama vile Singida, na Rujewa (aina hii ina rangi ya kahawia iliyopauka).
• Chotara: Hii ni aina ya vitunguu inayojulikana kama vitunguu vya kisasa. Katika kundi hili kuna vitunguu kama Texas grano, Red creole, Bombay red, White granex, na Super rex.

Mgawanyiko


Zao la vitunguu limegawanyika katika makundi mawili. Hii inatokana na uhitaji wa mwanga na ukuaji wake.  Aina ya kwanza inahitaji mwanga kwa saa 8-13 ili kuweza kuchanua na kutoa mbegu.


Aina ya pili inahitaji mwanga kwa saa 13-15 kuweza kuchanua na kutoa mbegu.


Kupanda


Vitunguu hupandwa kwa kutumia mbegu ambazo husiwa kwenye vitalu.  Kitalu kinaweza kuwa na upana wa mita 1, urefu unategemeana na ukubwa wa eneo ulilo nalo.


Unaweza kupanda vitunguu kwenye matuta mbonyeo (
Sunken bed). Aina hii ya upandaji hutumika kwenye eneo lenye shida ya maji. Upana wa tuta uwe mita moja.

Kupanda kwenye matuta mwinuko (
Raised bed) upandaji wa iana hii hutu mika sehemu yenye maji mengi au yanayotuama.

Tahadhari
: Maji yakituama kwenye vitunguu hufanya vitunguu kuoza, hivyo kuathiri mavuno.

Nafasi


Vitunguu vipandwe kwa nafasi ya sentimita 7.5 kutoka mche hadi mche, sentimita 12.5 kutoka mstari mmoja hadi mwingine kwenye matuta.


Mbole ya kupandia


Unaweza kutumia mboji, au samadi iliyo oza vizuri kupandia. Baada ya hapo unaweza kuongeza mboji baada ya miezi miwili. Endapo unafanya kilimo kisichozingatia misingi ya kilimo hai, unaweza kupanda kwa kutumia mbolea aina ya NPK (20:10:10) baada ya mwezi na nusu, unaweka mbolea ya Urea.


Palizi


Vitunguu ni zao lenye uwezo mdogo sana wa kushinda na magugu. Hivyo, inabidi shamba liwe safi muda wote wa ukuaji hadi kuvuna.


Uvunaji


Kwa kawaida, vitunguu huchukua muda wa miezi 5-6 tangu kupandwa hadi kuvunwa. Unaweza kuanza kuvuna vitunguu baada ya asilimia 75 ya shingo za vitunguu kuvunjika.  Baada ya kuvuna, unaweza kuweka kwenye madaraja (grades) kwa kufuata ukubwa, rangi na unene wa shingo ya kitunguu. Vitunguu vyenye shingo nyembamba hudumu zaidi, vyenye shingo nene huoza haraka.


Ukataji


Hakikisha kuwa shingo ya kitunguu inabaki kiasi cha sentimita 2. Hii husaidia kuzuia kuoza haraka.


Namna ya kuhifadhi vitunguu


Baada ya kuvuna, hifadhi vitunguu kwenye kichanja chini ya kivuli na uvitandaze vizuri.  Unaweza kuhifadhi vitunguu kwa kufunga kwenye mafungu na kuvitundika.  Vitunguu vikihifadhiwa vizuri vinaweza kukaa hadi miezi minne bila kuharibika, hii hutegemeana na aina ya uhifadhi.


Wadudu wanaoshambulia vitunguu

Kuna aina nyingi za wadudu wanaoweza kushambulia vitunguu.  Hawa wafuatao ni baadhi ya wadudu waliozoeleka kwenye zao la vitunguu.


Thiripi
Thiripi (Thrips): Wadudu hawa hukaa kwenye jani sehemu inayokutana na shina. Wadudu hawa hufyonza maji kwenye majani ya vitunguu na kusababisha majani kuwa na doti nyeupe.

Madhara:
Husababisha vitunguu kudumaa hivyo kuathiri ukuaji wake jambo ambalo huathiri mavuno pia.

Kimamba
Kimamba: Wadudu hawa hufyonza maji kwenye vitunguu, na kusambaza ugonjwa wa virusi. Husababisha kudumaa kwa vitunguu. Wadudu hawa ni hatari zaidi kwa kuwa husambaza virusi vinavyoingia hadi kwenye mbegu.

Minyoo fundo (Nematodes):
Aina hii ya minyoo hushambulia mizizi ya vitunguu. Hali hii husababisha kudumaa kwa vitunguu kwa kuwa hushindwa kufyonza maji na chakula kutoka ardhini.

Vidomozi (Leaf minor):
Hushambulia majani kwa kujipenyeza kwenye ngozi ya jani na kusababisha michoro ambayo huathiri utendaji wa majani.

Utitiri mwekundu (Red spider mites):
Wadudu hawa hufyonza maji kwenye majani na kusababisha vitunguu kunyauka.

Funza wakatao miche:
Funza hawa hutokana na wadudu wajulikanao kama Nondo, na hushambulia shina na kulikata kabisa.

Namna ya kukabiliana na wadudu hawa


Unaweza kukabiliana na wadudu hawa kwa kufanya kilimo cha mzunguko.  Usioteshe vitunguu sehemu moja kwa muda mrefu, au kufuatanisha mazao jamii ya vitunguu kama vile
leaks.

Tumia mbegu bora zilizothibitishwa kutoka kwenye kampuni zinatambuliwa kisheria na kibiashara.  Kupanda kwa wakati unaotakiwa; vitunguu visipandwe wakati wa kiangazi. Vipandwe wakati wa majira ya baridi na kuvunwa wakati wa joto. Tumia dawa za asili za kuulia wadudu, au dawa nyinginezo zinazopendekezwa na wataalamu wa kilimo.


Magonjwa yanayoshambulia vitunguu


Purple blotch
1. Purple blotch: Ugonjwa huu husababishwa na ukungu (fungus). Ugonjwa huu husababisha mabaka ya zambarau na meusi katika majani ya vitunguu.  Ugonjwa huu hutokea wakati wa unyevu unyevu mwingi.
Madhara:
Ugonjwa huu hupunguza mavuno mpaka asilimia hamsini (50%).

2. Stemphylium leaf blight:
Hukausha majani kuanzia kwenye ncha hadio kwenye shina.; Ugonjwa huu hutokea wakati wa unyevu na ukungu mwingi.
Madhara
: Hupunguza mavuno hadi kwa asilimia sabini na tano (75%).

Onion yellow draft virus
3. Magonjwa ya virusi (Onion yellow draft virus): Ugonjwa huu husababisha vitunguu kuwa na rangi iliyochanganyika, kijani na michirizi myeupe au njano.  Vitunguu hudumaa kwa kiasi kikubwa;Ugonjwa huu husababishwa na kimamba.
Madhara:
Huathiri mavuno kwa asilimia 80 mpaka asilimia 100%.

4. Kuoza kwa kiazi (Bulb rot): Husababishwa na fangasi. Ugonjwa huu hutokea vitunguu vikishakomaa, huku udongo ukiwa na maji maji.  Vitunguu vikishakomaa visimwagiliwe tena.

Uharibifu wa vitunguu usiotokana na magonjwa


1. Kuchipua baada ya kuvunwa:
Hali hii hutokea endapo vitunguu vitavunwa kabla ya muda wake.  Endapo vitunguu havitakaushwa vizuri baada ya kuvunwa. Hali hii husababisha uharibifu mpaka asilimia themanini (80%).  Sehemu ya kukaushia vitunguu iwe na hewa inayozunguka na mwanga wa kutosha. Vitunguu vikiwekwa gizani huchipua kwa urahisi.

2. Muozo laini (Soft rot):
Ugonjwa huu hushambulia vitunguu baada ya kukomaa; husababishwa na vimelea (bacteria). Vitunguu hutoa harufu mbaya ya uozo.  Kuepuka hilo vuna kwa wakati unaofaa, hifadhi sehemu yenye mwanga na hewa inayozunguka.

Virusi

Unaweza kuzuia vimamba ambao ndio wanaoeneza virusi kwa kutumia dawa za kuulia wadudu.

Ufugaji wa nguruwe

Nguruwe ni mnyama mwenye faida, na ni rafiki kwa mazingira na hahitaji gharama kubwa.....


Ufugaji wa Nguruwe ni lazima uwe wa kisasa ili kupata mazao bora. Unaweza kupata kila unachohitaji wewe, familia na hata ndugu zako kutokana na ufugaji wa nguruwe”, anasema Bwana Lomaiyani Molel kutoka Arusha. Jamii nyingi hapa Tanzania huchukulia nguruwe kama mnyama mchafu na asiyefaa kuwa karibu naye na hata kwa matumizi kama lishe. Zaidi, nyama yake inapendwa na haina madhara kwa afya na inapendekezwa kuliwa zaidi kuliko nyama nyekundu. Unaweza kuanzisha mradi wa nguruwe kwa gharama ndogo lakini baada ya kipindi cha miezi tisa tu ukaanza kujipatia kipato kutokana na ufugaji huo.


Ufugaji
Kwa kawaida nguruwe wanafugwa na watu wa kada zote, wafugaji wadogo wadogo na hata wakubwa. Aina hii ya ufugaji huweza kumpatia mkulima kipato pamoja na lishe kwa familia, na hauhitaji gharama kubwa.

Banda

Nguruwe wanahitaji kuwa na banda lililojengwa kwa vifaa nafuu. Unaweza kutumia mchanga na simenti kuweka sakafu, ama ukatumia udongo wa mfinyanzi kwa ajili ya kuweka sakafu. Ukubwa wa banda unategemeana na idadi ya nguruwe unaotaka kufuga. Mita 3 kwa mita 2.5 zitawaweka guruwe 8-10 wanaonenepeshwa kwa soko au nguruwe jike mmoja na nguruwe ndume mmoja.

Malisho

Ulishaji wa nguruwe ni rahisi kwa kuwa wanakula aina mbalimbali za vyakula kulingana na mazingira wanayofugwa. Unaweza kuwalisha kwa kutumia majani laini ya aina mbalimbali, na pia hulishwa kwa kutumia masalia ya nafaka (pumba). Unaweza kuwalisha kwa kutumia mashudu au pumba aina ya Wheat Poland. Pia unaweza kuwalisha kwa kutumia mabaki ya jikoni.

Kuzaliana

Nguruwe hubeba mimba kwa kipindi cha siku 114, ambazo hugawanyika kwa miezi 3, wiki 3 na siku 3. Nguruwe mmoja ana uwezo wa kuzaa watoto 6 hadi 14 kwa mara moja. Watoto wa nguruwe (piglets) huanza kula chakula cha kawaida wanapofika umri wa mwezi mmoja na nusu mpaka miezi miwili. Endapo nguruwe watapata matunzo mazuri, baada ya miezi 8 wanakuwa na uzito kati ya kilo 50-70 na wanaweza kuuzwa.

Matunzo

Baada ya nguruwe kuzaa anatakiwa kupatiwa chakula cha kutosha na cha kutia nguvu ili kupata maziwa ya kutosha kwa ajili ya watoto wake. Watoto wa nguruwe wachomwe sindano ya madini ya chuma (Iron injection) baada ya siku moja au mbili toka kuzaliwa. Hii ni muhimu sana vinginevyo wanaweza kufa wote. Kata meno (tooth clipping) baada ya miezi mitatu. Unaweza kuhasi madume (castration) baada ya miezi miwili.

Magonjwa yanayoathiri nguruwe

Kuna aina nyingi za magonjwa yanayoshambulia nguruwe, lakini yapo yale yaliyozoeleka ambapo ni lazima kukabiliana nayo ili kuwa na ufugaji wenye tija.

Ugonjwa wa miguu na midomo

Ugonjwa huu huathiri nguruwe sehemu za miguu na midomo. Ni ugonjwa ambao hushambulia nguruwe mara kwa mara hasa wasipokuwa na matunzo mazuri. Ugonjwa wa miguu na midomo, hudhoofisha nguruwe kwa haraka sana, ikiwa ni pamoja na kupungua uzito.


Chanjo:
Chanjo kwa ajili ya ugonjwa wa midomo na miguu (FMD vaccine) hutolewa kila baada ya mwaka mmoja. Hii inasaidia kuwaweka nguruwe wako katika hali nzuri zaidi bila kushambuliwa na magonjwa hayo.

Tiba:
Ugonjwa huu hauna tiba halisi. Inapotokea nguruwe wakawa wameshambuliwa kinachofanyika ni kutibu magonjwa nyemelezi kwa kutumia antibiotics.
 
Homa ya Nguruwe (Swine fever)
Virusi vinavyosababisha ugonjwa wa homa ya nguruwe huenea kwa haraka sana miongoni mwa makundi ya nguruwe, na huua kwa haraka sana, lakini hauna madhara kwa binadamu na hauambukizwi kwa binadamu. Nguruwe walioambukizwa waanshikwa na vindonda ama mapunye kwenye ngozi. Pia masikio na ngozi huwa mekundu.

Chanjo: Ugonjwa huu hauna chanjo wala tiba. Kinachofanyika mlipuko unapotokea ili kuwa salama ni kuwateketeza nguruwe wote walioathirika na kuanza upya. Unaweza kuteketeza kwa kuwachoma moto.
Muhimu: Baada ya kuwateketeza nguruwe wagonjwa, safisha banda kisha nyunyiza dawa aiana ya Acon au Ectomin, na uache banda wazi kwa kipindi cha wiki moja kabla ya kuweka nguruwe wengine.

Ugonjwa wa mapafu (Pneumonia)

Huu ni ugonjwa unaoshambulia sehemu za koo na mapafu ya nguruwe, ambapo husababisha kukohoa na kupumua kwa shida. Ugonjwa huu husababishwa na bacteria (Secondary bacterial), joto kupita kiasi, vumbi na gesi inayotokana na madawa makali.


Tiba:
Homa ya mapafu kwa nguruwe inatibika kwa kutumia antibiotics. Pamoja na kuwaweka wanyama sehemu safi, isiyo na baridi kali au joto la kupitiliza kiwango.

Kimeta (Anthrax)

Huu ni ugonjwa unaosababishwa na bakteria wanaojulikana kama Bacillus anthracis, wadudu hawa wanabaki kuwa hai kwa muda mrefu na wanaweza kuwa kwenye udongo wakiwa hai kwa kipindi cha miaka mingi.

Chanjo:
Chanja nguruwe wako dhidi ya kimeta kama utakavyoelekezwa na wataalamu wa mifugo walio karibu nawe.
Tiba:
Unaweza kutibu nguruwe wako kwa kutumia dawa aina ya Penisilin au Oxytetracycline.

Muhimu:
Homa ya nguruwe ni lazima iwekewe karatini kwa sababu husambaa kwa haraka sana. Nchini Tanzania mlipuko wa homa ya nguruwe umekuwa ukitokea mara kwa mara maeneo ya mpakani mwa Tanzania na Malawi na katika mkoa wa Mbeya.

Saturday, November 3, 2012

How do you care for pregnant dairy cattle?

The  Best Answer
Pregnant dairy cattle need to have comfort, adequate nutrition in the form of hay and silage, fresh water, shelter, and a calm, relaxed environment. They need to be cared for in such a way that they do not harm their growing calf inside them, but also not so stressed out that there are increased risk of abortions. Most dairy cattle will still be lactating during their first and second trimester of pregnancy, then allowed a break to dry up before calving so that the calf can have access to colostrum when the cow starts freshening and producing milk again.