Friday, February 6, 2015

KILIMO BORA CHA NYANYA- MAGONJWA NA WADUDU




Nyanya ni zao la chakula na biashara. Kilimo cha zao hili hufanyika majira yote
(masika na kiangazi), na faida hupatikana haraka na ni ya kuridhisha ikilinganishwa
na mazao mengine. Pamoja na umuhimu wa zao hili, wadudu waharibifu na
magonjwa huathiri uzalishaji na ubora wa matunda. Ili mkulima aweze kupata faida
na kuongeza pato la kaya yake ni vema kuzingatia udhibiti wa magonjwa na wadudu
wa zao hili. Kipeperushi hiki kinatoa maelezo ya udhibiti wa magonjwa na wadudu
muhimu ya zao la Nyanya.

MAGONJWA YA NYANYA
Bakajani chelewa (Late blight)
Ugonjwa huu huenenzwa na vimelea vya fangasi. Husababishwa na hali ya hewa hasa
ya unyevunyevu, na huenezwa na upepo. Majani, shina, matunda hushambuliwa.
Majani huwa na ukungu mweupe na kijivu, na baadaye hukauka. Matunda huwa na
mabaka ya kikahawia na baadaye kuoza. Mashina pia huwa na mabaka ya kikahawia.


Wednesday, February 4, 2015

KILIMO BORA CHA UFUTA

    KILIMO BORA CHA UFUTA

Ufuta (sesamum indicum)ni zao linalolimwa kwa wingi katika mikoa ya Lindi, Mtwara, Ruvuma, Pwani, Morogoro, Dodoma, Tanga na ukanda wa chini katika mikoa ya Rukwa na Mbeya. Zao hili hulimwa kwa ajili ya chakula na biashara. Mbegu za zao hili huwa na wastani wa mafuta kiasi cha asilimia 45.
  MAMBO YA KUZINGATIA WA KATI WA KUZALISHA MBEGU •
 Chagua aina ya mbegu inayotoa mazao mengi na bora, inayovumilia mashambulizi ya magonjwa na wadudu, inayokomaa mapema na kutoa mafuta mengi.
 • Chagua mbegu inayokomaa kwa pamoja ili kurahisisha uvunaji na pia kuepuka upotevu wa zao shambani. • Aina nyeupe ya mbegu ya ufuta hupendelewa zaidi kuliko aina nyeusi.


Tuesday, February 3, 2015

Magimbi, mkombozi wakati wa njaa

Hello Mkulima Mbunifu, naomba maelezo jinsi ya kuzalisha zao la magimbi hali ya hewa, ardhi, mvua au umwagiliaji na mda gani tangu kupanda hadi kuvuna. Asante – David Kilangi. yamMagimbi ni chakula muhimu chenye kiwango kikubwa cha wanga kinachohitajika katika mwili wa binadamu na moja kati ya mazao makuu ya chakula kama vile viazi mviringo, mihogo na viazi vitamu. Zao hili hulimwa katika sehemu mbalimbali duniani kama barani Afrika, Caribbean, Asia, America na Pacific. Kwa nchi za Afrika, zao hili hutumika zaidi kunapokuwa na uhaba wa chakula, kwani lenyewe hupatikana msimu wote wa mwaka na katika majira yote.
 Matumizi Magimbi hutumika kama chakula kikuu na huweza kupikwa kwa kuchanganya na ndizi, nyama, viazi, kupika kwa kukaanga, kuchemsha, kuchoma au kwa namna yoyote ila ambayo mlaji ataamua kutengeneza mlo wake.
  Pia hutumika kutengenezea unga wa ugali kwa kukatakata na kukausha kisha kuchanyanga na mahindi pamoja na mtama. Kulingana na kukua na kuongezeka kwa njia nyingi za ujasiriamali, zao hili kwa sasa hutumika kwa kutengenezea kaukau (crisps) kama ilivyo kwa viazi mviringo, viazi vitamu, ndizi na mihogo.

Papai, zao linalozalishwa kwa urahisi

Papai ni tunda lenye ladha nzuri, na rahisi kuliwa. Aina hii ya tunda ni chanzo cha virutubisho muhimu mwilini, ambavyo husaidia kujenga mwili. Zao hili asili yake ni ukanda wa kitropiki ambao hauna baridi kali na joto kiasi. 

Udongo pawpaw 2Mipapai hustawi vizuri kwenye udongo usiotuhamisha maji. Endapo maji yakituama kwenye eneo lililopandwa mipapai kwa muda wa siku mbili, mpapai unaweza kuoza kwa haraka na kufa. Kwa kuwa mipapai haina mzizi mkuu, inahitaji udongo wenye rutuba ya kutosha. Halikadhalika, zao hili halihitaji udongo wenye kina kirefu, hivyo ni muhimu kumwagilia mipapai wakati wa kiangazi. Wakati wa mapapai kuiva kama kuna ukame basi hali hiyo huongeza ubora wa papai ikiwamo kutooza mapema baada ya kuvunwa. 

Kupanda Mipapai ipandwe sehemu ambazo hazina upepo mkali. Hii itasaidia mipapai kukua vizuri bila kuvunjika kwani mti wa mpapai huvunjika kirahisi. Inashauriwa kupanda miti ya kukinga upepo kuzunguka shamba la mipapai. Ili kuwa na tija zaidi, unaweza kupanda aina nyingine ya miti ya matunda kama vile miparachichi, na miembe. Hakikisha miti ya kukinga upepo inakuwa mirefu kuzidi mipapai. Miti hiyo inaweza kutangulia kupandwa miezi kadhaa kabla ya kupanda mipapai.

Sunday, February 1, 2015

ZANA ZA KISASA KUWAINUA WAKULIMA

Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika chini ya Idara ya Zana za Kilimo imeandaa mkakati wa kuboresha sekta ya kilimo ili wakulima waondokane na jembe la mkono na kutumia zana za kisasa ikiwa ni moja ya sababu zinazoweza kuleta tija kwenye sekta ya kilimo nchini.
Zana ambazo zimetengenezwa kwa kutumia teknolojia ya kisasa na kutumia mafuta ya dizeli zinaweza kutumika katika mazingira mbalimbali ya kilimo nchini.
Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya zana za kilimo ya Savoy Farm Ltd Bw. Omari  Issa akizungumza katika maonesho ya Nane Nane , viwanja vya Nzuguni alisema mashine aina ya ‘palleting’ zimetengenezwa kwa ajili ya kuwakomboa wajasiriamali wadogo wanaojishughulisha na kilimo ili wazitumie katika shughuli zao.