Friday, April 10, 2015

Wafanyabiashara wagoma kununua mazao ya kilimo

Wafanyabiashara wagoma kununua mazao ya kilimo


Wafanyabiashara wagoma kununua mazao ya kilimo
Wafanyabiashara ya mazao ya kilimo wilayani mpwapwa wamegoma kununua mazao mbali mbali kutoka kwa wakulima kutokana na kile wanachodai kuwa tabia ya viongozi wa halmashauri ya wilaya hiyo kupandisha tozo za ushuru wa mazao kiholela bila kuwashirikisha.

Mgomo huo umekuja mara baada ya Halmashauri ya MPWAPWA kupandisha ushuru wa mazao kutoka shilingi elfu moja hadi elfu tano kwa gunia moja la mahindi na shilingi elfu moja hadi tatu kwa mazao mengine hali ambayo imezua malalamiko kutoka kwa wakulima.

NJOMBE waanza kutumia mbegu mpya za viazi mviringo

NJOMBE waanza kutumia mbegu mpya za viazi mviringo
Mbegu Bora Nne za Viazi Mviringo zimeanza kutumika katika wilaya ya WANGING’OMBE, Mkoani NJOMBE, kufuatia utafiti uliofanywa na Taasisi ya Utafiti wa Kilimo, UYOLE, na kubaini kuwa mbegu hizo ni bora kwa kilimo.

Afisa Kilimo wa Halmashauri ya wilaya hiyo , HENRY VAHAYE amesema wakulima wamekuwa na mwitiko katika matumizi ya mbegu hizo ambazo zinatajwa kuhimili magonjwambalimbali ya mazao.

Watalaam wa kilimo katika Halmashauri ya wilaya Mpya ya Wanging’ombe, wamesema kugunduliwa kwa mbegu hizo Nne za Viazi Mviringo,yawezekana ikawa suluhisho la adui Umaskini katika wilaya hii Mpya.

Pamoja na Mbegu hizo mpya za Viazi Mviringo ambazo zimeanza kutumiwa na wakulima wa wilaya tano za mikoa ya Njombe, Iringa na Mbeya, inadaiwa magonjwa mengine yamedhibitiwa isipokuwa Ugonjwa wa Mnyauko ambao umekuwa ni sumu kwa mimea ya mizizi nchini.

HANANG watakiwa kupanga matumizi bora ya ardhi

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Mahusiano na Uratibu Dkt. MARY NAGU
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Mahusiano na Uratibu Dkt. MARY NAGU, amevitaka vijiji vyote wilayani HANANG mkoani MANYARA, kupanga matumizi bora ya ardhi ili kuepusha migogoro miongoni mwa makundi mbalimbali katika jamii

Dkt. NAGU ametoa wito huo wakati wa ziara yake katika vijiji vipya vilivyosajiliwa mwaka jana na kuwataka wananchi kushirikiana na viongozi wao kudumisha amani miongoni mwao.

Waziri NAGU amewaeleza wananchi hao kuwa uamuzi wa serikali wa kuanzisha vijiji vingi zaidi umelenga kusogeza huduma za kijamii karibu na wananchi.

Hata hivyo ameonya kuwa bila kupanga matumizi bora ya ardhi katika vijiji ili kuyapanga makundi mbalimbali yaweze kuishi kwa usalama, upendo na mshikamano, maendeleo ya haraka yaliyokusudiwa hayawezi kufikiwa kwa wakati.

Viongozi wa vijiji hivyo kwa upande wao, wameiomba serikali na Mbunge huyo wa Jimbo la HANANG, kuwasaidia kutatua kero mbalimbali zinazowakabili wananchi katika maeneo yao ikiwemo maji, elimu na baadhi ya barabara za vijiji.

Katika ziara hiyo pia ambayo mpaka sasa imehusisha vijiji vipya 30, DOKTA NAGU amewahimiza wananchi kujiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kura, kujiunga katika mfuko wa afya ya jamii-CHF ili kuboresha upatikanaji wa huduma za afya wilayani humo pamoja na kuipigia kura katiba inayopendekezwa wakati utakapofika.

Wednesday, April 8, 2015

ULIMAJI WA VITALU VYA BUSTANI BIASHARA RAHISI YENYE FAIDA



ULIMAJI WA VITALU VYA BUSTANI BIASHARA RAHISI YENYE FAIDA

ULIMAJI WA VITALU VYA BUSTANI BIASHARA RAHISI YENYE FAIDA
Katika falsafa ya Kilimo kwanza nchini Tanzania, baadhi ya watanzania wengi wameitikia kauli hiyo na baadhi ya wafanya biashara na wakulima mbalimbali kusahau suala la ulimaji na utunzaji wa vitalu Bustani kama Maua, miche ya matunda, miti, nyanya na mazao yoyote ya bustani ni biashara rahisi na yenye faida.
Ukulima wa vitalu vya Bustani ni biashara ambayo inafanya vizuri na kupata mwitikio mkubwa katika nchi mbalimbali hususani Kenya nchi jirani na Tanzania ambapo wanawake wamewekeza katika biashara hii na kupata mafanikio kwa urahisi kama mwanamama Loyce ambaye pia ni msomkama anavyvo elezea katika kidokezo hapo chini.
Aidha teknolojia hii ni chanya kwa watanzania kuanza kuitumia kwani Tanzania ni nchi yenye rutuba nzuri kwa kilimo na asilimia kubwa ya watanzania ni wakulima wakitegemea kilimo kama uti wa Mgongo. Hata hivyo Njia Mpya inalitazama suala hili kwa jicho pana na faida kwa mkulima au mfanyabiashara wa ulimaji na utunzaji wa vitalu na kuiona ni fursa muhimu kwa mfanyabiashara kupitia njia hii kupata kipato na hatimaye kupunguza na kuondoa kabisa umasikini katika familia na nchi kwa ujumla. Kuna maadui watatu ambao ni hatari sana kwa maendeleo katika jamii nao ni “Umasikini, Ujinga na Maradhi” ni wakati sasa wa kupambana na umasikini huu tujitokeze na kuiona fursa hii. Biashara hii haibagui wanaume wala wanawake 

Vijana waaswa kutumia Fursa wazipatazo

WAZIRI wa habari vijana utamaduni na michezo FENELLA MKANGARA
WAZIRI wa habari vijana utamaduni na michezo FENELLA MKANGARA,amewashauri vijana kote nchini kuwa wabunifu na kutumia fursa zinazojitokeza mbele yao ili kujiletea maaendeleo

Hayo ameyasema katika mkusanyiko wa magari hamsini na pikipi 10 za vijana wa BONGO RIDE wakiwa tayari kufanya msafara unaotwa BONGO CHARITY CRUIZE kutoka DAR hadi MORO.

mkurugenzi wa makapuni ya TSN GROUP, FAROUQ BAGHOZA anaeleza kwa nini amedhamini msafara huo kuwa ni kuwaleta vijana pamoja na kuibuwa vipaji vya vijana hapa nchini.

Msafara huo wa MAGARI na PIKIPIKI kutoka DAR HADI MOROGORO, utatembelea kikundi cha watu wanaoshi na virusi vya ukimwi mkoani morogoro,WAVUMO ili kujua shida zao na kuzitafutia ufumbuzi.

Monday, April 6, 2015

Mkutano wa Sita wa Baraza la mwaka la wadau wa Tasnia ya Nyama Tanzania

Msajili wa Bodi ya Nyama Tanzania anawatangazia wadau wote wa Tasnia ya Nyama nchini kwamba kutakuwa na Mkutano wa Baraza la Mwaka hivi karibuniMsajili wa Bodi ya Nyama Tanzania anawaalika  kuhudhulia Mkutano wa Baraza la Mwaka la Wadau wa Tasnia ya Nyama hapa nchini ambao utafanyika tarehe 15/04/2015 na 16/04/2015,katika hoteli ya Glonency 88, saa 2:30 asubuhi. Wajumbe wa Mkutano huu ni wadau wote walioteuliwa na Mhe. Waziri wa Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi kwa mujibu wa Sheria ya Nyama Na. 10 ya Mwaka 2006 kutoka:-
  1. Mamlaka zote za Serikali za Mitaa za Tanzania Bara,
  2. Taasisi za Serikali, Wizara na Idara za Serikali.
  3.  Asasi za kiraiya zenye maslahi na tasnia ya nyama
Taarifa ya tarehe na mahali utakapofanyika mkutano huu zitatolewa baadae.

Aidha, wadau wenye nia ya kushiriki kwa lengo la kubadilishana na uzoefu kwenye tasnia na hawako kwenye orodha tajwa hapo juu wawasiliane na Msaji wa Bodi ya Nyama Tanzania.

Agriculture - Tanzania

Agriculture is the leading sector of the economy of Tanzania. Apart from providing food, agriculture remains the country's main source of income for the rural population, which forms 80% of the total population and employs 70% of the active labour force of the population. It contributes about 50% of the GDP and about 75% of the foreign exchange earnings. In Tanzania Agriculture is dominated by smallholder farmers with farm sizes ranging between 1 hectare and 3 hectares. Most of these smallholders use the hand hoe as the main cultivating tool. Ox ploughs are used by about twenty percent of the farmers and about ten per cent use tractors.
A wide variety of crops can be grown in Tanzania due to its wide climatic variation and agro-ecological conditions. Area cultivated for food production makes up the bigger part of land under crop production. Maize and rice are principal food crops as well as commercial crops, while cassava and bananas are important subsistence crops. Traditional export crops of Tanzania are coffee, cotton, tea, sisal and cashew nuts. Other widely grown crops include beans, sorghum, millet, sweet potatoes and various types of oil seeds. A wide variety of fruits, vegetables and flowers are also grown in Tanzania.

Wilaya ya Kwimba yakabiliwa na Njaa


Wilaya ya KWIMBA mkoani MWANZA inahitaji msaada wa zaidi ya Tani Elfu Kumi za chakula ili iweza kukabilina na tatizo la njaa ambalo limeikumba wilaya hiyo. 

Mkuu wa wilaya ya KWIMBA - PILI MOSHI amethibitisha wilaya hiyo kuhitaji msaada wa haraka wa chakula kufuatia hali ya ukame uliosababisha kukauka kwa mazao mbalimbali. 

Mkuu wa wilaya hiyo ya KWIMBA alikua akitoa taarifa hiyo kwa wajumbe wa halmashauri kuu ya Chama Cha Mapinduzi – CCM wilayani KWIMBA, viongozi pamoja na watendaji wa serikali wa wilaya hiyo.

Wednesday, April 1, 2015

Sugar production -Tanzania

Sugar is a sweet crystalline substance, which may be derived from the juices of various plants. Chemically, the basis of sugar is sucrose, one of a group of soluble carbohydrates, which are important dietary sources of energy in the human diet. It can be obtained from trees, including the maple and certain palms, but virtually all manufactured sugar comes from two plants sugar beet (Beta vulgaris) and sugar cane, a giant perennial grass of the genus Saccharum. Sugar cane, found in tropical areas, grows to a height of up to 5 metres or more In Tanzania sugar is produced from Sugar cane. Sugar cane in Tanzania is primarily grown in four estates, namely Kilombero Sugar Company, Mtibwa Sugar Estate, Tanganyika Planting Company and Kagera Sugar Limited. Apart from sugar cane grown by the estates, other sugar cane is grown by out growers who are found at Kilombero and Mtibwa estates and there contribution has gradually increased in recent years. In general the annual sugar production in Tanzania is about 115,000 tonnes per annum while the estimated demand of sugar is estimated at 300,000 tonnes. Tanzania imports about 200,000 tonnes per annum to offset the shortfall. Sugar Production

Monday, March 30, 2015

Eneo linalofaa kwa ufugaji

Eneo linalofaa kwa ufugaji
Baadhi ya maeneo yanayofaa ni yale mashamba ya mpunga, na maeneo yaliyo karibu na vyanzo vya
maji. Zifuatazo ni sifa za maeneo yanayofaa:
1. Udongo: Mfinyanzi husaidia kupunguza gharama za ujenzi wa bwawa na maji kwakuwa
linaweza kutuamisha maji na kuruhusu maji yasipotee. Likiwa la kichanga bwawa ni lazima
lijengewe au kuwekwa nylon sheet ili kuzuia upotevu wa maji. Unaweza ukahamisha udongo
wa mfinyanzi kutoka sehemu moja hadi nyingine ili kuzuia upotevu wa maji (muone
mtaalamu kwa ushauri zaidi juu ya mbinu ya kuhamisha udongo)
2. Chanzo cha maji ya uhakika
Eneo liwe na maji ya uhakika. Vyanzo vya maji ni kama vile mito, bahai, maziwa, chem
chem., kisima, maji ya dawasco na mvua. Maji yasiwe na kemikali hatarishi kwa viumbe.
3. Miundombinu ya barabara: Inasaidia kwa ajili ya usafirishaji wa bidhaa na samaki wakati wa
kuvuna.
4. Eneo lisiwe na historia ya mafuriko ili kuzuia athari za mafuriko kwa miundombinu yako.
Utatumia gharama nyingi katika kuimarisha miundombinu yako.Jamii/aina ya samaki
5. Eneo lenye mwinuko wa wastani husaidia katika ujenzi wa bwawa.
6. Miundombinu ya umeme ni sifa ya ziada hususan kwa mkulima wa kati na wajuu kwa ajili ya
kutumika katika kuendesha visambaza hewa.
7. Ulinzi muhimu
Note: Aina ya eneo lako ndilo linaweza kukufanya uchague muundombinu gani wa kufugia
utumie
Aina ya samaki unaoweza kufuga Tanzania kwa sasa
Maji baridi
Sato/perege, Kambale, Kambamiti wa maji baridi na Trout (maeneo ya baridi kama vile
Iringa, Kilimanjaro Arusha na Mbeya) na samaki wa mapambo.
Maji bahari
Kambamiti wa maji bahari, mwatiko, chewa, kaa, chaza wa lulu
Upatikanaji wa Vifaranga vya samaki husika
Vyanzo vya vifaranga ni kutoka katika mito, bahari, maziwa na wale wa kuzalishwa katika
vituo vya kuzalishia vifaranga.
Sato na Kambale
Vituo vya serikali Utapata sato wa kike na kiume mixed sex). Kingolwira –Morogoro, Luhira-
Songea, Mbegani-Bagamoyo . Kifaranga huuzwa Tsh. 50-100 kwa kifaranga.
Vituo binafsi kama vile Faith aquaculture-Kibamba (DSM) (utapata monosex sato), Peramiho-
Songea (mixed sex). Monosex huuzwa Tsh. 200 kwa kifaranga, na mixed ni 100 kwa
kifaranga.
Trout
Mayai huagizwa toka Marekani, Israel
Kambamiti wa baharini
Alphakrust –Mafia.
Chakula cha samaki
Chakula cha asili
Hurutubishwa kwa mbolea ya wanyama kama vile kuku, ngombe, mbuzi nk. Kwa kiwango
cha 1000kg/ha. Mbolea ya kuku ni kali hivyo unaweza punguza ikawa 250-500kg/ha.
Chakula cha kutengeneza
Samaki huitaji protein ili akuwe na kila samaki ana mahitaji yake hivyo ni species specific.
Formula zipo kwa wale wanaotaka kutengeneza. Tanzania hakuna kiwanda
kinachotengeneza. Ingredients zake ni kama vile dagaa, pumba, soya, unga wa ngano, unga
wa muhongo nk.
Uvunaji
Kwa kawaida ni miezi 4-6 amabapo unapata 250-400g kulingana na ulishaji wako. Kwa
prawns ni miezi 3-6 wanafikia 30-50g ambayo ni ukubwa wa soko.
Tathmini ya uchumi
Perege/sato
Mfano:
Ukubwa wa bwawa ni 20m by 30m= 600 mita za mraba
Idadi ya samaki (7 kwa mita ya mraba) kwa monosex tu= 600 x 7=4200 fish
Uzito hadi kuvuna (4-6months)- 250g= 4200 x 250g= 1050kg (Nimesha convert gram to kg)
Bei kwa kilo ni 6000-8000 kulingana na mahali= 6milion-8milion.

Vodacom Foundation yakabidhi msaada wa Umeme Jua kwa wahanga wa mvua Kahama

Mkuu wa Vodacom Tanzania,Kanda ya Tanganyika George Venanty(kushoto) na Meneja Masoko wa Kampuni ya Associate AEG Winnie Nyamubi(kulia) wakielezea matumizi ya Umeme Jua”Solar Power” wakati wakukabidhi msaada huo uliotolewa na Vodacom Foundation kwa wahanga wa maafa ya mvua kwenye kijiji cha mwakata wilayani Kahama Mkoani Shinyanga mwishoni mwa wiki.

AIRTEL YAKARABATI DARASA SHULE YA MSINGI USHINDI


Mkurugenzi Mkuu wa Airtel Tanzania, Sunil Colaso (wa tatu kulia), akizungumza kabla ya kukabidhi Darasa la Chekechea lililokarabatiwa kwa udhamini wa Wafanyakazi wa Airtel, kama sehemu ya huduma kwa jamii, katika Shule ya Msingi Ushindi iliyopo Mikocheni ‘B’, jijini Dar es Salaam jana. Kutoka (kulia) ni Mwenyekiti wa Shule hiyo, Jumanne Konara na Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Elias Katunzi, Meneja wa Huduma kwa Jamii wa Airtel, Hawa Bayumi (kushoto) na baadhi ya wafanyakazi wa kampuni hiyo.

Friday, March 27, 2015

wakulima moshi wakabiliana na ukame

Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi CCM, ABDULARAMAN KINANA
Baadhi ya wakulima wa zao la Mpunga katika SKIMU ya umwagiliaji katika Halmashauri ya wilaya ya MOSHI, mkoani KILIMANJARO wanakabiliwa na tatizo la ukame unaosababisha upungufu wa maji na kuharibu miundombinu ya SKIMU hiyo na kuhatarisha uzalishaji wa mpunga.

Hayo yalibainika katika ziara ya Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi CCM, ABDULARAMAN KINANA ambazo zilianzia katika kijiji cha MIKOCHENI hapa wilayani MOSHI mkoani KILIMANJARO kijiji kilichopo pembezoni mwa kiwanda cha Sukari cha TPC.

Ziara ya KINANA ikamfikisha katika SKIMU ya umwagiliaji ya LOWA iliyopo wilayani humo ambapo SKIMU hiyo hivi sasa haina tija tena licha ya kudumu kwa uzalishaji kwa zaidi ya miaka

Akitoa taarifa ya SKIMU hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya MOSHI, FULGENCE MPONJI amesema SKIMU hiyo yenye wakulima ELFU TATU, hivi sasa inauweza wa kulimwa Hekari 700 tu, tofauti na ilivyokuwa hapo awali kabla ya changamoto hiyo, ambapo wakulima hao walikuwa na uwezo wa kulima Hekari 1500.

Treni ya mizigo kutoka Bandari ya DSM - ISAKA hadi KIGALI yazinduliwa jijini DSM


Fri Mar 27 2015

 safari za treni za mizigo kuelekea Rwanda katika stesheni ya Reli ya Dar es salaam aa mkutano wa nchi sita za ukanda wa kati na walipotembelea

Rais Paul Kagame wa Rwanda akipeperusha bendera kuashiria kuzinduliwa kwa safari za treni za mizigo kuelekea Rwanda katika stesheni ya Reli ya Dar es salaam akiwa na mwenyeji wake Rais Jakaya Mrisho Kikwete
Rais PAUL KAGAME wa RWANDA na RAIS JAKAYA KIKWETE wa TANZANIA wameridhia kutekelezwa kwa mradi wa ujenzi wa reli ya kisasa kutoka bandari ya DSM-ISAKA hadi KIGALI nchini RWANDA utakaozihusisha nchi tano za AFRIKA MASHARIKI baada ya kuona fursa zilizopo za kibiashara.

Wakizungumza wakati wa mkutano wa nchi sita za ukanda wa kati na walipotembeleaBandari za DSM na Shirika la Reli TRL, marais hao wamesema ili kuharakisha utekelezaji wa mradi huo ni muhimu kuweka wazi faida za mradi huo kwa kila nchi ili itambue jinsi wananchi wake watakavyofaidika kiuchumi na kijamii kabla haijatoa rasilimali zake kuijenga Reli hiyo.

Rais JAKAYA KIKWETE amemuhakikishia RAIS PAUL KAGAME wa RWANDA kuwa amefanya mabadiliko makubwa ya uongozi bandarini hapo na miundombinu iliyowekezwa itaongeza kasi ya ushirikiano wa nchi za ukanda wa kati

Naye Rais PAUL KAGAME ameipongeza serikali ya Tanzania kwa kuweza kupunguza msongamano wa mizigo bandarini na kuhakikisha mizigo inasafirishwa kwa wakati kwenda nchi jirani zinazotegemea bandari hiyo ikiwemo nchi yake ya RWANDA.
Wakati wa majadiliano wa mkutano wa jukwaa la wawekezaji ulioongozwa na RAIS PAUL KAGAME wadau wameelezea namna ya kupata fedha za kutekeleza miradi hiyo ambapo sekta binafsi ndio itakayopewa jukumu hilo kwa ushirikiano na sekta ya umma.
Bandari za DSM na Shirika la Reli TRL, marais hao wamesema ili kuharakisha utekelezaji wa mradi huo ni muhimu kuweka wazi faida za mradi huo kwa kila nchi ili itambue jinsi wananchi wake watakavyofaidika kiuchumi na kijamii kabla haijatoa rasilimali zake kuijenga Reli hiyo. Rais JAKAYA KIKWETE amemuhakikishia RAIS PAUL KAGAME wa RWANDA kuwa amefanya mabadiliko makubwa ya uongozi bandarini hapo na miundombinu iliyowekezwa itaongeza kasi ya ushirikiano wa nchi za ukanda wa kati Naye Rais PAUL KAGAME ameipongeza serikali ya Tanzania kwa kuweza kupunguza msongamano wa mizigo bandarini na kuhakikisha mizigo inasafirishwa kwa wakati kwenda nchi jirani zinazotegemea bandari hiyo ikiwemo nchi yake ya RWANDA. Wakati wa majadiliano wa mkutano wa jukwaa la wawekezaji ulioongozwa na RAIS PAUL KAGAME wadau wameelezea namna ya kupata fedha za kutekeleza miradi hiyo ambapo sekta binafsi ndio itakayopewa jukumu hilo kwa ushirikiano na sekta ya umma

Thursday, March 26, 2015

KILIMO CHA CHA UMWAGILIAJI CHA FANIKIKIWA MKOANI ARUSHA

Skimu ya Maji ya Kabambe iliyojengwa katika Wilaya ya Monduli kata ya Majengo kuwasaidia wakulima kupata maji kwa ajili ya kilimo cha Mahindi, Ndizi na Mbogamboga, ikiwa ni sehemu ya miradi inayoratibiwa na ASDP na kusimamiwa na wadau wa maendeleo IFAD .
Mojawapo ya Shamba la Nyanya linalotumia Skimu ya Maji ya Kabambe inayoratibiwa na Miradi ya ASDP katika Wilaya ya Monduli.  
Shamba la Mbogamboga la Wakulima wa Monduli wanaotumia Skimu ya Maji ya Kabambe ikiwa ni sehemu ya mafanikio ya miradi ya ASDP inayosimamiwa na wadau wa maendeleo IFAD

KILIMO CHA UMWAGILIAJI MJINI DODOMA


 Kilimo cha umwagiliaji mjini dodoma kwenye maonesho ya nanenane zikionekana mbogamboga zinavyo kubari kilimo hicho katika maonesho
 Ni zao la sukuma wiki linavyo onekana pichani katika kilima cha umwagiliaji katika maonesho ya nanenane mjini dodoma 

NORWAY YADHAMIRIA KUWEKEZA LINDI KATIKA SEKTA YA GESI NA UVUVI

Balozi wa Norway Nchini,Bi Ingunn Klepsvik (Katikati) akikagua baadhi ya mabwawa ya ufugaji samaki manispaa ya Lindi walipotembelea mradi wa uvuvi katika Ziara ya Mameya wa miji ya Norway waliokubali kujenga urafiki na manispaa za Lindi na Mtwara,Kushoto ni Abdilah Salum mmiliki wa mabwawa hayo na Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Lindi Dr Nasor Hamid.





Balozi wa Norway Nchini,Bi Ingunn Klepsvik akipokea maelezo ya hali ya Uvuvi Ndani ya manispaa ya Lindi toka mkurugenzi wa manispaa Kelvin Makonda huku mmiliki wa mabwawa hayo akielezea mipango yake ya baadae ikiwa pamoja na kuiomba Norway kumsaidia Elimu na utaalamu bora wa ufugaji wa Kisasa.
Mabwawa yanayotumika kwa ufugaji wa samaki.
Meya wa manispaa ya Alstahaug,Bard Anders Lango akiwa na Mkuu wa Wilaya ya Lindi,Dk. Nassor Hamid wakibadilishana mawazo juu ya Ushirikiano huo ikiwemo Uwekezaji katika mji wa Lindi ambao hauna hata kiwanda kimoja hadi sasa huku kukiwa na harakati za kujengwa kwa kiwanda cha simenti cha Meis kitakachochangia ajira mbalimbali.
Meya wa manispaa ya Hammerfest Alf E Jakobsen (kati)akisikiliza maelezo ya Ufugaji wa samaki toka kwa Afisa Uvuvi wa manispaa ya Lindi Bi Sharifa Tomera.

Ujumbe toka Norway wakipata maelezo ya ukaushwaji wa samaki kwa njia ya kienyeji kutokana na kukosa dhana bora.

Na ABDULAZIZ ,Lindi
Miji miwili ya Hammerfest na Sandnessjoen iliyoko nchini Norway Imekubali kuanzisha ushirikiano baina ya manispaa ya Lindi na Mtwara Ambapo kwa pamoja wameitaka Halmashauri ya Manispaa ya Lindi pamoja na wanajamii kuwekeza katika Elimu ikiwemo kujijengea Tabia ya Kulipa kodi ambazo zitarudi katika huduma za jamii.

Uamuzi huo umefikiwa katika mkutano baina ya viongozi wa miji hiyo na Manispaa hiyo baada ya kutembelea miradi mbalimbali ya Gesi na Uvuvi vitu ambavyo vinachangia pato kubwa katika Nchi zao.

Katika makubaliano hayo viongozi kutoka pande zote wamekubaliana kuwa mji wa Harmmerfest utashirikiana na Lindi na ule wa Sandnessjoen utashirikiana na Mtwara, ushirikiano ambao unalenga kuzitumia fursa zilizopo kujikwamua kiuchumi kupitia sekta hizo ili kuhakikisha mikoa ya kusini inanufaika na rasilimali zake ikiwemo Ardhi ya kutosha na fukwe zenye ubora.

Akizungumzia umuhimu wa makampuni ya mafuta katita mji wa Sandnessjoen Meya wa mji huo Bard Anders Lango ameeleza kuwa mji wake unanufaika na mafuta na asilimia kubwa ya wananchi ni walipa kodi na asilimia 12 ya mapato urudishwa katika huduma za jamii zikiwemo Elimu na Afya.

Akiongea na globu hii,Mkurugenzi Mtendaji wa Manispaa ya Lindi Kelvin Makonda kwa Upande wake ametoa Shukrani kwa ujio huo na Kuanzishwa kwa ushirikiano baina ya miji hiyo na mikoa ya kusini kutasaidia kufungua ukurasa mpya wa mahusiano na kuwezesha wananchi kuwa sehemu ya mafanikio ya kuanzishwa kwa miradi ya umma katika maeneo yao.

Huu ujio umekuja muda muafaka huku manispaa yangu kwa kushirikiana UTT tayari imepima Viwanja vya kutosha na tumeanza mchakato wa kuviuza na hata hawa wageni wetu tumewapa Fursa ya kununua viwanja kwa ajili ya shughuli za uwekezaji ikiwemo Hotel,Elimu na Viwanda maeneo yapo ya kutosha".

Katika ziara hiyo inayoongozwa na Balozi wa Norway nchini Tanzania,Bi Ingunn Klepsvik walitembelea Mabwawa ya Uvuvi ya ASM Trading 2005 na kumilikiwa na Abdillah Salum Mfaume ambayo tayari jumla ya Samaki 96468 wameshapandwa katika mabwawa hayo.

Aidha Bw Abdilah salum alitoa wito kwa ugeni Huo kusaidiwa utaalam wa kutosha katika Ufugaji wa Kutosha bila ya kuathiri Mazingira na kubainisha kuwa matarajio yake ni kuvuma zaidi ya kilo 25000 katika kipindi cha miezi sita ijayo hali itakayomwongezea kipato na kujiwezesha kuboresha Uvuvi katika mkoa wa Lindi

Wednesday, March 25, 2015

Wakulima washauriwa kuboresha zao la ALIZETI

Maduka makubwa mchanganyiko- SUPERMARKETS yamewashauri wakulima kuboresha kilimo cha zao la Alizeti kwa vile mafuta yanayotokana na zao hilo yana soko kubwa kuliko mafuta ya kutoka nje. 

Wakizungumzia ubora wa mafuta hayo, msemaji wa duka la Mirado Fortunatus Bernard na msemaji wa duka la TSN Nassoro Abdallah wamesema mafuta ya alizeti yanapendwa kwa sababu yanawasaidia watu wenye matatizo ya moyo.

KINANA aishauri serikali kufanya tathmini ya mashamba yaliyochukuliwa na wawekezaji

Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi-CCM, ABDULRAHMAN KINANA
Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi-CCM, ABDULRAHMAN KINANA ameishauri serikali kufanya thamthni juu ya mashamba ya baadhi ya wananchi yaliyochukuliwa na wawekezaji ambao wameshindwa kuendeleza wakati wa kipindi cha ubinasfsishaji ili kuruhusu wigo mpana wa wananchi kupata fursa ya kumiliki ardhi. 

Akizungumza katika mkutano wa hadhara katika mji wa SANYAJUU, wilayani SIHA mkoani KILIMANJARO, KINANA amesema baadhi ya wawekezaji wakubwa katika mikoa mbalimbali ikiwemo TANGA, ARUSHA na KILIMANJARO wamehodhi maeneo makubwa ya ardhi ambayo wamekuwa wakiyakodisha kwa wafanyabishara, mashamba ambayo hapo zamani yalikuwa yakimilikiwa na wananchi. 

Akiwa ziarani mkoa wa KILIMANJARO, katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi ABDULRAHAMN KINANA, akatembelea katika bwawa la umwagilaiji katika kijiji cha KASHISHI wilayani SIHA, mradi ambao unatajwa kuwa chachu ya wananchi kujipatia kipato na kupitia sekta ya kilimo.
(imetolewa na tbc1)

MANYARA yakumbwa na ukame

Mkuu wa mkoa wa MANYARA, DOKTA JOEL BENDERA
Wakati hayo yakiendelea jijini DSM, huko Mkoani MANYARA hali ya ukame imekuwa tishio kwa wakulima Mkoani humo na kuwasababishia hofu ya kukabiliwa na njaa kutokana na uhaba wa mvua kwa kipindi kirefu. 

Baadhi ya wakulima wamesema uhaba huo wa mvua umesababisha mazao yaliyoko shambani hususan mahindi kunyauka. 

Katika msimu wa kilimo wa mwaka 2014/2015, mkoa wa MANYARA umefanikiwa kuwa na mavuno ya uhakika ya mazao mbalimbali kutokana na mvua za wastani zilizonyesha kwa mpangilio 

Lakini katika msimu huu, kila mahali mkoani Manyara, wakulima wanapaza sauti zao za kukosa matumaini ya kuvuna chochote baada ya jitihada kubwa walizowekeza katika kilimo kuonekana kugonga mwamba. 

Wataalamu wa idara ya kilimo katika wilaya ya HANANG wameielezea hali hiyo ya ukame kutishia upatikanaji wa chakula 

Mkuu wa mkoa wa MANYARA, DOKTA JOEL BENDERA, amesema katika mahojiano maalumu na TBC, mabadiliko ya tabia nchi yanachangia hali hiyo ya ukame 

Makundi mbalimbali ya kijamii yameanza kufanya ibada za aina mbalimbali zikiwemo za kimila na kwenye makanisa kuombea mvua inyeshe ili kunusuru hali hiyo

imetolewa na TBC 1


TANZANIA na KENYA zatiliana saini kudhibiti biashara haramu ya mazao ya misitu

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mazingira na Maliasili nchini Kenya Richard Lusiambe (wakwanza kulia) akiongozana na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Misitu na Nyuki nchini Tanzania Gladness Mkamba mara baada ya kutia saini makubaliano ya Tanzania na Kenya kupiga vita biashara haramu ya mbao pamoja na mazao ya misitu inayofanyika kupitia mipaka ya nchi hizo katika mkutano uliofanyika jijini Arusha na Kuandaliwa na Shirika la kimataifa la kulinda wanyama na viumbe hai World Wildlife Foundation (WWF) ambao n
Serikali za KENYA na TANZANIA zimetiliana saini makubaliano ya kudhibiti biashara haramu ya mazao ya mazao ya misitu ikiwa ni pamoja na mbao na biashara ya mkaa 


Naibu Mkurugenzi wa Misitu nchini akimwakilisha Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira GRADNESS MKAMBA,katika zoezi hilo jijini ARUSHA ambayo yamefadhiliwa na shirika la Uhifadhi wa masingira Duniani WWF,amesema makubalianao hayo yatasaidia biashara ya misitu inafanyika kwa kufuata sheria na si kwa njia za panya. 



Mara baada ya kusaini makubaliano hayo,Naibu Mkurugenzi wa Misitu ambaye amemwakilisha Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira GRADNESS MKAMBA amesema biasahara haramu ya mbao na mkaa imekuwa ikifanyika kwa njia za panya na sasa kupitia makubaliano hayo itadhibitiwa. 



Katibu Mkuu anayeshughulikia mazingira na maliasili nchini KENYA, Dk RICHARD LESIYAMPE,amesema misitu inafaida nyingi kiuchumi na hivyo ni vema kuwe na utaratibu sahihi. 



Mkurugenzi wa shirika lisilo la kiserikali la Uhifadhi wa Mazingira Duniani WWF anayewakilisha nchi ya TANZANIA,AMANI NGUSALU,amesema nchi hizo zilikuwa na maeneo makubwa ya misitu lakini kwa sasa hali ni tofauti. 



Makubaliano kama hayo yalishafanyika baina ya nchi ya TANZANIA na MSUMBIJI mwaka 2013 na yanadaiwa na wataalamu wa misitu kuonyesha mafanikio makubwa.
(IMETOLEWA NA TBC1)

Monday, March 23, 2015

Welcome to Rifaro Africa ... Simu Yako, Jembe Lako

Welcome to Rifaro Africa ... Simu Yako, Jembe Lako

Who We Are

RIFARO AFRICA is a network marketing company that uses the direct selling method to distribute telecommunication products and services primarily and exclusively using an online platform. At Rifaro Africa, we not only sell products that people NEED but products that EVERYONE uses .In addition, it is evident that telecommunication companies spend billions to compensate the middlemen involved in airtime distribution, but when subscribers buy airtime on mobile money platforms none of the middlemen get the direct financial benefits. Rifaro Africa forms a club of members consuming products i.e. airtime, by buying through the Rifaro port on the mobile money platforms and passes the commissions back to members like you and me as incentives and commissions when you just sign up and promote Rifaro products as a Rifaro Africa Distributor.