Wednesday, April 8, 2015

ULIMAJI WA VITALU VYA BUSTANI BIASHARA RAHISI YENYE FAIDA



ULIMAJI WA VITALU VYA BUSTANI BIASHARA RAHISI YENYE FAIDA

ULIMAJI WA VITALU VYA BUSTANI BIASHARA RAHISI YENYE FAIDA
Katika falsafa ya Kilimo kwanza nchini Tanzania, baadhi ya watanzania wengi wameitikia kauli hiyo na baadhi ya wafanya biashara na wakulima mbalimbali kusahau suala la ulimaji na utunzaji wa vitalu Bustani kama Maua, miche ya matunda, miti, nyanya na mazao yoyote ya bustani ni biashara rahisi na yenye faida.
Ukulima wa vitalu vya Bustani ni biashara ambayo inafanya vizuri na kupata mwitikio mkubwa katika nchi mbalimbali hususani Kenya nchi jirani na Tanzania ambapo wanawake wamewekeza katika biashara hii na kupata mafanikio kwa urahisi kama mwanamama Loyce ambaye pia ni msomkama anavyvo elezea katika kidokezo hapo chini.
Aidha teknolojia hii ni chanya kwa watanzania kuanza kuitumia kwani Tanzania ni nchi yenye rutuba nzuri kwa kilimo na asilimia kubwa ya watanzania ni wakulima wakitegemea kilimo kama uti wa Mgongo. Hata hivyo Njia Mpya inalitazama suala hili kwa jicho pana na faida kwa mkulima au mfanyabiashara wa ulimaji na utunzaji wa vitalu na kuiona ni fursa muhimu kwa mfanyabiashara kupitia njia hii kupata kipato na hatimaye kupunguza na kuondoa kabisa umasikini katika familia na nchi kwa ujumla. Kuna maadui watatu ambao ni hatari sana kwa maendeleo katika jamii nao ni “Umasikini, Ujinga na Maradhi” ni wakati sasa wa kupambana na umasikini huu tujitokeze na kuiona fursa hii. Biashara hii haibagui wanaume wala wanawake 

No comments:

Post a Comment