Monday, April 6, 2015

Mkutano wa Sita wa Baraza la mwaka la wadau wa Tasnia ya Nyama Tanzania

Msajili wa Bodi ya Nyama Tanzania anawatangazia wadau wote wa Tasnia ya Nyama nchini kwamba kutakuwa na Mkutano wa Baraza la Mwaka hivi karibuniMsajili wa Bodi ya Nyama Tanzania anawaalika  kuhudhulia Mkutano wa Baraza la Mwaka la Wadau wa Tasnia ya Nyama hapa nchini ambao utafanyika tarehe 15/04/2015 na 16/04/2015,katika hoteli ya Glonency 88, saa 2:30 asubuhi. Wajumbe wa Mkutano huu ni wadau wote walioteuliwa na Mhe. Waziri wa Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi kwa mujibu wa Sheria ya Nyama Na. 10 ya Mwaka 2006 kutoka:-
  1. Mamlaka zote za Serikali za Mitaa za Tanzania Bara,
  2. Taasisi za Serikali, Wizara na Idara za Serikali.
  3.  Asasi za kiraiya zenye maslahi na tasnia ya nyama
Taarifa ya tarehe na mahali utakapofanyika mkutano huu zitatolewa baadae.

Aidha, wadau wenye nia ya kushiriki kwa lengo la kubadilishana na uzoefu kwenye tasnia na hawako kwenye orodha tajwa hapo juu wawasiliane na Msaji wa Bodi ya Nyama Tanzania.

No comments:

Post a Comment