Friday, April 10, 2015

Wafanyabiashara wagoma kununua mazao ya kilimo

Wafanyabiashara wagoma kununua mazao ya kilimo


Wafanyabiashara wagoma kununua mazao ya kilimo
Wafanyabiashara ya mazao ya kilimo wilayani mpwapwa wamegoma kununua mazao mbali mbali kutoka kwa wakulima kutokana na kile wanachodai kuwa tabia ya viongozi wa halmashauri ya wilaya hiyo kupandisha tozo za ushuru wa mazao kiholela bila kuwashirikisha.

Mgomo huo umekuja mara baada ya Halmashauri ya MPWAPWA kupandisha ushuru wa mazao kutoka shilingi elfu moja hadi elfu tano kwa gunia moja la mahindi na shilingi elfu moja hadi tatu kwa mazao mengine hali ambayo imezua malalamiko kutoka kwa wakulima.

No comments:

Post a Comment