Monday, April 6, 2015

Wilaya ya Kwimba yakabiliwa na Njaa


Wilaya ya KWIMBA mkoani MWANZA inahitaji msaada wa zaidi ya Tani Elfu Kumi za chakula ili iweza kukabilina na tatizo la njaa ambalo limeikumba wilaya hiyo. 

Mkuu wa wilaya ya KWIMBA - PILI MOSHI amethibitisha wilaya hiyo kuhitaji msaada wa haraka wa chakula kufuatia hali ya ukame uliosababisha kukauka kwa mazao mbalimbali. 

Mkuu wa wilaya hiyo ya KWIMBA alikua akitoa taarifa hiyo kwa wajumbe wa halmashauri kuu ya Chama Cha Mapinduzi – CCM wilayani KWIMBA, viongozi pamoja na watendaji wa serikali wa wilaya hiyo.

No comments:

Post a Comment