Saturday, June 1, 2013

Tanzania kuongeza uzalisha wa kahawa ifikapo 2016

Morogoro. Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Christopher Chiza amesema kuwa Tanzania inatarajia kuzalisha tani 80,000 za kahawa ifikapo mwaka 2016 nia ikiwa ni kuongeza uzalishaji wa zao hilo na kukidhi masoko ya ndani na nje ya nchi.
Chiza pia alisema kuwa Tanzania imekuwa ikizalisha wastani wa tani 35,000 na 50,000 za aina mbalimbali za kahawa kwa mwaka ikiwa ni pamoja na aina ya Arabica, Robusta zenye soko kubwa katika soko la dunia.
Akizungumza katika ufunguzi wa mkutano wa wadau wa kahawa unaofanyika mjini Morogoro, Waziri Chiza alisema wizara yake imeweka mikakati mbalimbali ya kuboresha zao hilo ikiwa ni pamoja na kuongeza mikoa minane ya ulimaji wa zao hilo ambayo ni pamoja na Morogoro, Iringa, Njombe, Katavi, Geita na Manyara huku Serikali ikiendelea kujenga mazingira mazuri zaidi ya kilimo cha zao hilo.
Alisema hakuna sababu ya kilimo cha zao hilo kushuka, kwa kuwa zao hilo lina bei nzuri katika soko la dunia, akiwataka Watanzania kuzalisha kwa wingi hata pale bei ya zao hilo inaposhuka katika soko la dunia kwa kuwa imekuwa na mtindo wa kupanda na kushuka mara kwa mara.
“Zao la kahawa ni muhimu sana na ni lazima kuwapo na utaratibu wa kuwa na bei moja yenye manufaa kwa mkulima na nchi yetu kwani mkulima amekuwa na mahitaji makubwa ya kimaisha na anatakiwa kukuza uchumi wake,” alisema waziri huyo.
Waziri Chiiza alisema, umefika wakati wa kuanza kutafuta masoko mapya ndani na nje ya nchi badala ya kung’ang’ania soko moja na kujikita katika kulalamika na kuongeza kuwa ili kuweza kufanikiwa katika kutafuta masoko hayo, ni lazima balozi zitumike kusaidia ili wakulima waweze kunufaika.
Alisema Serikali itaendelea kushirikiana na wadau na bodi ya kahawa kusaidia kupitia ruzuku kila mwaka na kuzitaka halmashauri kutenga maeneo ya kilimo cha kahawa na kuweka bustani za miche ya zao hilo ili wakulima waweze kupata miche hiyo kwa bei nafuu.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa mkutano huo, Seleman Chambo mapema akimkaribisha Waziri Chiza alisema kuwa, uzalishaji wa zao la kahawa nchini umeshuka kutokana na sababu mbalimbali ikiwa ni pamoja na baadhi ya mashamba ya kahawa kulimwa mazao mengine huko mkoani Kilimanjaro wakati baadhi ya wadau wa kahawa nchini wakilalamikia kutofuatwa kwa bei elekezi ya kahawa.

Thursday, May 30, 2013

Stakabadhi ghalani yaongeza gharama kwa wakulima


Utaratibu ulioanzishwa na serikali wa kuuza bidhaa za mkulima kwa mfumo wa stakabadhi ghalani (WRS) katika baadhi ya maeneo yenye uzalishaji mkubwa, umeelezwa kuongeza gharama kwa mkulima, licha ya kuwapo kwa faida katika mfumo huo.
Kitendo cha wakulima kulipa tozo kwa kilo moja ya mazao inayonunuliwa kwa mfumo huo ni mzigo mzito kwa wakulima. Utafiti mpya unaonyesha kwamba
dawa ya kuondokana na gharama hizo ni wakulima kujiunga katika ushirika na kujiendesha wenyewe.
Imeelezwa kwamba ushirika huo utawasaidia wakulima kutumia vyema fursa za kiuchumi katika kuzalisha, kuhifadhi na kupata soko la uhakika.
Tunalipa Sh2 milioni
Ofisa Mtendaji wa Taasisi ya RUDI ambayo kazi yake ni kuongeza thamani ya bidhaa zinazozalishwa nchini, Abel Lyimo akizungumzia utafiti mpya unaohusu mfumo wa stakabadhi ghalani unaojulikana ‘Tanzania Warehouse Legal Framework and its Impact on Sesame and Rice Farmers,’amesema wakulima wanalazimika kumwajiri Meneja Dhamana wa kushughulikia mfumo huo na kwamba wanamlipa Sh2 milioni kwa mwezi.

Lyimo anasema utafiti huo uliangalia athari za
kisheria na kiutendaji wa mfumo wa stakabadhi ghalani kwa mazao ya ufuta na mpunga.
“Hii ni gharama kubwa kwa wakulima, kwanini wamwajiri Meneja Dhamana wa kuangalia ghala?” anahoji Lyimo. Anafikiri kwamba ni vyema wakulima
waachwe wachague namna nzuri ya kuhifadhi na kuuza bidhaa zao kupitia ushirika.
Kwa mujibu wa utafiti huo kitendo cha kumwajiri Meneja Dhamana ni kigumu kwa kuwa wataalamu wa aina hiyo wana gharama kubwa na inakuwa ngumu zaidi wanapotaka kulipwa kwa dola za Marekani, yaani fedha za kigeni.
Kwa mtazamo mwingine endapo wakulima wanapatiwa mafunzo na kwa kuzingatia teknolojia ya asili, wanaweza kabisa kuhifadhi mazao yao ghalani tena kwa ufanisi zaidi kuliko Meneja Dhamana.
“Mameneja dhamana wengi  hawana uzoefu na mazingira ya eneo husika,” anasema Lyimo. Anasema kupitia vyama vya ushirika gharama nyingi zisizokuwa na maana zitapungua kwa upande wa wakulima.
Kwa mujibu wa Chama Kikuu cha Ushirika cha Wakulima wa Mpunga cha Kilombero(AKIGIRO), shughuli ya hifadhi na masoko wao wanafanya vyema.
Kwa mujibu wa taarifa ya utafiti huo kuna tatizo la  maghala hivi sasa na yaliyopo yanaonekana kutumika kibinafsi zaidi,
na kusababisha wakulima kutokuwa na uwezo wa kudhibiti. Wakati mwingine wakulima wanalazimishwa kutumia mfumo wa stakabadhi ghalani hata kama
hawautaki mfumo huo.
Pia imebainika kwamba ni vigumu kwa wakulima kuteta na bodi yenye dhamana na masuala ya maghala kutokana na kuwapo kwa urasimu.
Kwa mujibu wa utafiti huo, wakulima hasa wale wa ufuta wa Mkoa wa Lindi wamekuwa katika mgogoro na serikali ya mkoa kwa sababu serikali hiyo iliwataka wauze ufuta kupitia mfumo wa stakabadhi ghalani na si vinginevyo.
Wakulima wa mpunga wa Kilombero wamesema bodi ya stakabadhi ghalani katika  eneo lao imekuwa na sheria kali ikiwa ni pamoja na kuwazuia wakulima wadogo kujenga na kumiliki maghala yao.
“Kwa mfano ili ghala litambulike katika mfumo wa malipo ya stakabadhi ghalani iwe na uwezo wa kuchukua si chini ya tani 200 na masharti mengine ambayo ni magumu,” inasema taarifa hiyo.


Kanuni zilizowekwa zinawazua watu binafsi na wakulima wadogo na wale
wa makundi kumiliki maghala yao katika maeneo yao,”inasema sehemu ya taarifa ya utafiti huo.
Kwa mujibu wa utafiti huo Halmashauri ya Kilwa mwaka 2012/13 iliamua
kujitoa katika mfumo wa Stakabadhi ghalani baada ya kubaini
kwamba wanapoteza fedha nyingi kwa kukumbatia mfumo huo.
“Sababu kubwa ni kwamba bei iliyokuwa inatolewa na chama cha ushirika
cha ILULU ilikuwa ndogo kuliko zile zinazotolewa katika mikoa ya Dar es Salaam na Mkoa wa Pwani zinazopakana na wilaya ya Kilwa,” inasema
taarifa hiyo.
Kuhakikisha kwamba mkulima, vyama vya msingi na serikali za mitaa zinafaidika, halmashauri ilitengeneza muundo mwingine wa soko la ufuta na pia mfumo wa soko la wazi ulidhibitiwa. Imeelezwa kwamba faida kubwa ya mfumo huo katika Wilaya ya Kilwa, gharama nyingi zilizopo katika mfumo wa stakabadhi ghalani, ziliondolewa.
“Wafanyabiashara walielekezwa kwenda katika vijiji kadhaa, kuamsha ushindani wa kibiashara,bei ya juu ilipatikana na hivyo kuongeza kipato kwa mkulima, vyama vya ushirika vya msingi na kwenye serikali za mitaa,” inasema taarifa hiyo iliyodhaminiwa na BEST AC.

Taarifa ya utafiti huo inaonyesha kwamba tofauti na mifumo mingine na  gharama za usafirishaji zinamezwa na mkulima. Katika mfumo huo mnunuzi
anabeba gharama za usafirishaji kwa kiwango kikubwa.
Mnunuzi alikuwa ananunua gunia la kuhifadhia mazao na kulipia riba za benki.

Kutokana na mfumo huo Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa iliingiza kama kodi katika mfuko wake Sh395 milioni katika msimu wa mwaka 2012/2013 kutoka Sh70 milioni katika miaka iliyopita,huku vyama vya msingi vikiwa vimevikusanya Sh250 milioni  na Sh7 bilioni.
Kwa upande wake mwanzilishi wa shirikisho la wakulima waliohitimu vyuo vikuu Stephano Kingazi anasema wakulima hawana nongwa na mfumo wa stakabadhi ghalani, lakini hawataki serikali kuwalazimisha kuuza au kutouza mazao yao.
“Wakulima wengi wanakubaliana na ukweli kwamba mfumo wa stakabadhi ghalani ni mzuri kwao, lakini wanasema kuna makato mengi kwa kilo
na kusababisha mzigo mzito kwa mkulima,” anasema Dk Kinganzi katika mahojiano hivi karibuni mkoani Morogoro.

Kwa mujibu wa utafiti huo, wakulima wa mpunga walikuwa wanakatwa asilimia
15 katika Wilaya ya Kilombero katika mfumo wa stakabadhi ghalani, asilimia 29 wilayani Lindi na asilimia 8 Kilwa kutokana na mfumo wake.
Wakulima wawe huru
“Kinachoonekana hapa, kuna watu wengi wanachukua fedha kwa mkulima hata kabla mazao yake hayajafikia mwisho wa safari.
“Itakuwa vyema kama wakulima watafanya shughuli za kuuza mazao yao
bila kuingiliwa na mtu,” inasema taarifa ya utafiti huo.
Kwa mujibu wa utafiti, stakabadhi ghalani inakuwa na faida zaidi kwa wakazi wa vijijini. Dk Elibariki Msuya, miongoni mwa watu walioandaa taarifa ya utafiti huo amesaema ingawa Tanzania inasheria nzuri zinazowezesha mfumo wa
stakabadhi ghalani ukilinganisha na majirani zake, bado serikali haijaufikisha mfumo huo mahali pa zuri.

“Wadau mbalimbali wameonyesha matatizo hapa na pale katika mifumo tofauti inayofanyakazi nchini kwa lengo la kusaidia wakulima; mfumo wa Mkoa wa Lindi unaonekana kuwa kikwazo,kwani una sheria nyingi zinazobana katika soko la wazi na unaonekana ni dhaifu.
Katika mfumo wa Kilwa unaonekana kuwa na nafuu zaidi na mzuri kwa wakulima kwani ulifanikiwa kupunguza tozo mbalimbali,” anabainisha Dk Msuya.
Mfumo wa Kilombero unawezesha mfumo wa stakabadhi ghalani kufanyakazi huku pia watu binafsi wakiendelea kufanyakazi na kumpa fursa mkulima kuchagua soko lenye bei nzuri.
 Habari zaidi:
Kuna maghala 60 katika mikoa 19.
Biashara ya maghala nchini inasimamiwa na Bodi ya kutoa leseni ya Maghala ambayo inafanyakazi chini ya sheria namba 10 ya mwaka 2005 ya stakabadhi ghalani na kanuni zake za mwaka 2006.
 Tangu kuanzishwa kwa bodi hiyo imetoa leseni kwa maghala 60 katika mikoa 19 yenye uwezo wa kuhifadhi tani 267,000.

Wednesday, May 29, 2013

Spika Makinda azima hoja ya Mdee kuhusu umiliki wa mashamba makubwa

Dar es Salaam. Spika wa Bunge, Anne Makinda jana aliizima hoja ya Mbunge wa Kawe (Chadema), Halima Mdee kuhusu umiliki wa mashamba makubwa yasiyoendelezwa wakati wa kujadili hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi ambayo ilihitimishwa bungeni jana.

Mdee alivutana na Spika Makinda wakati wa kujadili bajeti hiyo kifungu kwa kifungu, Mdee alipotaka kufahamu kauli ya Serikali kuhusu kampuni zinazomiliki ardhi bila kuziendeleza na hatua zinazochukua kuhakikisha zinarudishwa kwa wananchi.
Baada ya kuuliza swali hilo huku akisisitiza kutoa shilingi, Spika Makinda alimtaka kukaa chini kwa kuwa hoja yake haina mashiko ya kufanya hivyo na kwamba kama anataka aiwasilishe kama hoja binafsi.
“Kaa chini, nakwambia kaa chini,” alisema Makinda huku Mdee akionekana kuendelea kuzungumza... “Nasema kaa chini,” alirudia na Mdee kukaa huku akikipeperusha karatasi hewani kuonyesha kutokubaliana naye.
Awali, Mdee alisema shamba la Simanjiro ambalo Halmashauri ya wilaya hiyo ilipendekeza mwekezaji kupewa ekari 500 lakini Wizara ya Ardhi iliidhinisha ekari 25,000 ambazo mwekezaji hajaziendeleza zote wakati mashamba ya Kisarawe na mashamba ya mkonge Tanga ambayo wawekezaji wameyakopea fedha nayo hadi sasa hayajaendelezwa.
Alitaka kauli ya Serikali kuhusiana na hali hiyo na jinsi ya kurudisha mashamba hayo katika miliki ya umma. Mbunge mwingine aliyetishia kutoa shilingi ni Dk Faustine Ndungulile wa Kigamboni (CCM), akijikita katika suala la ujenzi wa mji mpya wa Kigamboni akisema wananchi wake hawakushirikishwa katika mipango ya ujenzi huo.
Akijibu hoja hizo, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka alisema wananchi wameshirikishwa kikamilifu katika mchakato mzima na kuahidi kukaa na mbunge huyo pamoja na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Fredrick Werema kuzungumzia suala la Kigamboni.
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Goodluck ole Medeye alisema kila mkazi atalipwa Sh35,000 kwa kila mita moja ya mraba na mwenye ekari moja atapata Sh141 milioni na kuwataka wananchi kutoa ushirikiano kwa kuwa mradi huo utakuwa wa maendeleo kwa kila mmoja.
Baada ya majibu hayo, Dk Ndungulile alisimama na kusema kuwa anakubali kurejesha shilingi hasa baada ya Waziri Tibaijuka kutamka kuwa wananchi wameshirikishwa na watashirikishwa katika kutatua mgogoro wa Kigamboni.
Spika Makinda aliwataka kushirikiana kutatua mgogoro wa Kigamboni ili mradi uanze.    

Plot For Sale


Tuesday, May 28, 2013

Starlet for sale

3.3 m pungufu unaongea
FOR MORE INFO CALL +255 713 615365
+255 765 615365, +255 784 615365

Maandilizi ya kilimo cha Mpunga Sengerema


Watoto  wa kijiji cha Luchili wilayani Sengerema wakiandaa shamba kwa ajili ya kupanda Mpunga. Zao la Mpunga  hivi sasa linalimwa na wananchi wengi wa mikoa ya Mwanza na Shinyanga kwa ajili ya chakula na Biashara. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).