ndugu zangu ambao mnabweteka na kutafuta kazi kuna kilimo cha vitunguu, two years unakuwa mtu mwingine kabisa na huta penda kuajiriwa na kama utakuwa kwenye ajira unaweza acha kabisa na kuamua kuwa mkulima. Tusiwaze kuajiriwa tu tutakufa maskin mwisho wa siku. Mimi nimejaribu na sasa nataka niache kazi na kuwa moja ya wakulima na wafanyabiashara wakubwa wa vitunguu na mazao yote ya shamba kwa ujumla ila pamoja na hilo bado nahitaji muongozo mkubwa kwa watu waliobobea kwenye ukulima pamoja na biashara ya mazao ya shambani ili waweze kunishauri zaidi. Mimi napatikana moshi pamoja na arusha ndiko napofanyia biashara zangu. Please kwa yoyote ambaye amebobea kwenye biashara hii zaidi naomba ani PM ili tuweze kupeana contact ili mkukuza network na bidae kuweza kuanzisha kitu flani kwa manufaa yetu asanteni sana na wakilisha.