Friday, May 24, 2013

Waziri akiri kuhusu mbolea feki nchini

Naibu Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Adam Malima 

Dodoma
 Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika, imekiri kuwa inakabiliwa na changamoto ya kuwapo kwa mbolea isiyokuwa na viwango vinavyokubalika na inayoathiri uzalishaji wa mazao.
Kauli hiyo ilitolewa bungeni na Naibu Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Adam Malima, alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Peramiho, Jenister Mhagama (CCM).
Mbunge huyo alitaka kujua kauli ya Serikali kuhusu tatizo la ubora wa mbolea, linalowakabili wakulima katika kila msimu wa kilimo.
Naibu Waziri alisema Serikali kwa kutambua hilo, imeweka udihibiti wa mbolea isiyokuwa na viwango kwa kupitia sheria ya mbolea ya mwaka 2009, kifungu cha 7 (1).
“Pamoja na hayo, lakini pia Serikali imeunda Mamlaka ya Usimamizi wa Mbolea ambayo kazi yake ni kuthibitisha ubora wa mbolea viwandani,” alisema Malima.
Alisema katika kukabiliana na tatizo hilo katika ngazi ya halmashauri na wakulima, Serikali imeanza kutoa mafunzo kwa wakaguzi wa mbolea na kwamba hadi Mei mwaka jana kulikuwa na wakaguzi 44 kutoka katika halmashauri mbalimbali.
Kwa upande mwingine kiongozi huyo alisema tayari wizara imeweka utaratibu mzuri wa kuhakikisha kuwa mbolea inawafikia wananchi kila ifikapo Agosti mosi.


No comments:

Post a Comment