Saturday, May 25, 2013

Mkulima mbaroni kwa kukutwa na kobe 70

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, David Misime akionyesha kobe hai wapatao 70 waliokamatwa. Kulia kwake ni Afisa Mnadhimu wa Jeshi hilo mkoani humo, Suzan Kaganda akiwa ameshika Ngozi ya DigiDigi.
 Mkulima Moses Nyawage (42), Mkazi wa Kijiji cha Ng’hongona Manispaa ya Dodoma anashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kukutwa na kobe 70 wenye thamani ya zaidi ya Sh. milioni 7.8.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, David Misime alisema kuwa mtuhumiwa huyo alikamatwa na kobe hao Mei 22 mwaka huu saa 10.30 jioni katika  maeneo ya Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom).

Alisema alipohojiwa mtuhumiwa huyo, aliwaeleza kuwa aliwapata  kobe hao katika maeneo ya Mwitikila na kuwahifadhi kwenye viroba.

Naye Elias Mathias  (45), Mkazi wa Pwaga Wilaya ya Mpwapwa anashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kupatikana na ngozi mbili za mnyama aina ya digidigi.

Mtuhumiwa huyo alikamatwa Mei 22, mwaka huu saa 10.30 usiku katika Kijiji cha Pwaga akiwa na ngozi hizo zenye thamani ya Sh.800,00 kwa mujibu wa sheria.

Watuhumiwa hao watafikishwa mahakamani baada ya upelelezi kukamilika.Mkulima Moses Nyawage (42), Mkazi wa Kijiji cha Ng’hongona Manispaa ya Dodoma anashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kukutwa na kobe 70 wenye thamani ya zaidi ya Sh. milioni 7.8.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, David Misime alisema kuwa mtuhumiwa huyo alikamatwa na kobe hao Mei 22 mwaka huu saa 10.30 jioni katika  maeneo ya Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom).

Alisema alipohojiwa mtuhumiwa huyo, aliwaeleza kuwa aliwapata  kobe hao katika maeneo ya Mwitikila na kuwahifadhi kwenye viroba.

Naye Elias Mathias  (45), Mkazi wa Pwaga Wilaya ya Mpwapwa anashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kupatikana na ngozi mbili za mnyama aina ya digidigi.

Mtuhumiwa huyo alikamatwa Mei 22, mwaka huu saa 10.30 usiku katika Kijiji cha Pwaga akiwa na ngozi hizo zenye thamani ya Sh.800,00 kwa mujibu wa sheria.

Watuhumiwa hao watafikishwa mahakamani baada ya upelelezi kukamilika.

Mkulima Moses Nyawage (42), Mkazi wa Kijiji cha Ng’hongona Manispaa ya Dodoma anashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kukutwa na kobe 70 wenye thamani ya zaidi ya Sh. milioni 7.8.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, David Misime alisema kuwa mtuhumiwa huyo alikamatwa na kobe hao Mei 22 mwaka huu saa 10.30 jioni katika  maeneo ya Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom).


Alisema alipohojiwa mtuhumiwa huyo, aliwaeleza kuwa aliwapata  kobe hao katika maeneo ya Mwitikila na kuwahifadhi kwenye viroba.


Naye Elias Mathias  (45), Mkazi wa Pwaga Wilaya ya Mpwapwa anashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kupatikana na ngozi mbili za mnyama aina ya digidigi.


Mtuhumiwa huyo alikamatwa Mei 22, mwaka huu saa 10.30 usiku katika Kijiji cha Pwaga akiwa na ngozi hizo zenye thamani ya Sh.800,00 kwa mujibu wa sheria.


Watuhumiwa hao watafikishwa mahakamani baada ya upelelezi kukamilika.

No comments:

Post a Comment