Friday, February 20, 2015

ZIFAHAMU MBEGU BORA ZA MAHARAGE

mbegu_za_maharage_selian_39c9e.jpgNa. Josephine MkudeNi vema kwa wakulima kuzingatia mbegu bora katika kilimo ili kupata mazao bora yatakayowapa faida baada ya mavuno.  Kituo cha Utafiti wa Kilimo Selian Arusha ambacho ni makao makuu ya utafiti ya kanda ya Kaskazini kwa miaka mingi imekuwa ikitafiti aina bora za maharage ambazo hutoa mazao mengi, ambazo pia zinastahimaaili ukame na magonjwa. Kwa kufuata kanuni bora za kilimo wakulima wanaweza kuongeza uzalishaji wa zao la maharage kwa kutumia mbegu bora kama vile Jesica, Lyamungu na Selian. Mbegu hizi zimeshasambazwa kwa wakulima na wanazitumia kwa uzalishaji

No comments:

Post a Comment