![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhxD0nGJphkc-TH85AxDIrA5Lhin6BKqhxJfcByW6NX6l4TzPiJaSIBs7RAPPZilOwHeMYfuWDycHGJ-JTfbrzZEGMpCNHHZqC8TfaQavSrvu1igNSP6IRrkWOs1th9rlttKYbhPLD1kVs/s200/Dsc00005.jpg)
MATUMIZI
Majani yake huweza kupikwa kama mboga na kuliwa, pia yanaweza kuhifadhiwa kwa muda mrefu bila ya kuathiri ubora wake wa virutubisho (nutritional value) majani yake yanavirutubisho vingi kuliko vyakula vingi tulivyozoea mfano
Ina vitamin A nyingi zaidi ya karoti
Ina Calcium nyingi zaidi ya Maziwa
Ina madini ya chuma zaidi ya spinach
Ina vitamin C nyingi zaidi ya Machungwa
Ina madini na pottasium zaidi ya Ndizi
ina protein nyingi zaidi ya nyama na mayai
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEh50GA8oQOx8LU6vb40qm8DTe88Nk9Jt1jiEYKsf8xLrF3XOndRq_FiN2mB1PvHCA-9y74HHLfua4TZN_J-BxxaNb-vDlQIl50bBz3bydEpW-kPUm91MGZ2zM75WWO16vzADaQW6l5aL9I/s400/Dsc00020b.jpg)
MATUMIZI MENGINE
Maganda ya mbegu zake yanaweza kutumika kutibu maji(water treatment)unachukua maji yako ambayo unahisi si salama, unachanganya na maganda ya mbegu zilizopondwa pondwa kiasi, unayaacha kwa muda yatuame kisha unayachuja na yanakuwa salama kwa matumizi
Mbegu za milonge zinaweza kutumika kama dawa ya kupunguza sukari mwilini kwa wagonjwa wa kisukari, unachukua mbegu mbili au tatu unazipasua na kuchukua kokwa ya ndani na kutafuna mara 3 kwa siku, matumizi yanaweza kuongezeka au kuzidi kutegemeana na hali ya mgonjwa
Picha hapo chini inaonyesha mbegu za mlonge juu na kulia kwake ni baada ya kupasuliwa na kupata kokwa ya ndani (ambayo ni dawa ya kupunguza sukari mwilini), funguo imewekwa ili kujua ukubwa halisi wa mbegu
Sehemu yoyote ya mmea kama majani, magamba, mizizi, au maua yakipondwa pondwa na kupakwa kwenye sehemu yenye uvimbe ni dawa tosha ya kupunguza hali hiyo, pia dawa hii inauwezo mkubwa wa kupunguza sumu kama umeng'atwa na wadudu kama nyuki, manyigu/dondola, siafu, tandu, nge nk
Mbegu zake zinatoa mafuta (40%) yanayojulikana kama BEN OIL, ambayo hutumika kulainishia mitambo maalum kama saa za ukutani, pia mafuta haya ni dawa ya upele na harara
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgkzNfxbuXEJ-rVLJQWhONScealZUXY8vsTzBSV3lr7eIvvEr-gmmJnSr3byw5D4mhDKUd3Wsa6Alsw2iPA6GMZ2GWE5s1EiHkUi0hRbPz_RCEWc932N2P4jLN9d3lfYwMcy8x2-hKwanE/s400/Dsc00001b.jpg)
No comments:
Post a Comment