Wednesday, February 19, 2014

KUTOKA OFISI YA MKUU WA MKOA MANYARA



FURUSA ZA UWEKEZAJI KATIKA MKOA WA MANYARA
Mkoa una fursa nyingi za uwekezaji hususani katika huduma za Kiuchumi (Kilimo na Mifugo, Viwanda, Biashara, Utalii na Madini); Kijamii (Elimu, Afya na Maji); na Kiutamaduni (Michezo na Utamaduni).
FURSA ZA UWEKEZAJI KATIKA HUDUMA ZA KIUCHUMI KILIMO
Kuna maeneo makubwa yanayofaa kwa shughuli za kilimo cha kwaida na kilimo cha umwagiliaji katika Mkoa. Mazao yanayozalishwa kwa wingi ni pamoja na Mahindi, Alizeti, Mbaazi, Mtama, Ngano, Maharage, Miwa, Vitunguu Maji, Vitunguu Saumu na Mpunga ambayo hutumika kama mazao ya Biashara na Chakula kwa wakazi wa Mkoa, Mikoa jirani na Nchi jirani za Kenya, Somalia, Ethiopia, Eritiria na Sudani. Hivyo wawekezaji wanakaribishwa kuwekeza katika sekta hii. MIFUGO
Mkoa una zaidi ya mifugo milioni 2. Wawekezaji wanakaribishwa kuwekeza katika sekta hii hususani katika uanzishaji wa ranchi na viwanda vikubwa na vidogo vya kusindika mazao ya mifugo ambayo ni nyama, maziwa na ngozi. Fursa nyingine ya kuwekeza katika sekta hii ni ujenzi wa majosho na mabwawa kwa ajili ya kuogesha na kunyweshea mifugo.

VIWANDA
Mkoa unawakaribisha wawekezaji ili waanzishe na kuwekeza katika viwanda Vikubwa, vya kati na Vidogo kwa ajili ya kusindika mazao ya kilimo, mifugo na sekta nyingine. Kwa sasa Mkoa una Kiwanda kikubwa cha Mbolea cha Minjingu ambacho husambaza mbolea yake ndani na nje ya Mkoa na Kiwanda cha kusindika nyama kilichopo Wilayani Simanjiro. Kadhalika, Mkoa unakadiriwa kuwa na viwanda vidogovidogo 4560 vinavyofanya kazi za: Kusindika Nyama na Maziwa, mafuta ya Alizeti, Kusaga na kukoboa nafaka na Kutengeneza Mkaa usiotoa moshi wenye athari.

BIASHARA
Tayari makampuni kadhaa kama vile Kampuni ya Usafirishaji ya Mtei ‘express’, kampuni za Simu za Vodacom, Airtel, Zantel na Tigo na taasisi za fedha kama Benki ya Posta Tanzania, NMB, NBC, CRDB, EXIM nk. wanaendelea na shughuli mbalimbali za biashara ndani ya Mkoa. Hata hivyo bado kuna fursa nyingi za kuwekeza hususani katika uanzishaji wa maduka makubwa yenye bidhaa mbalimbali, hoteli za kitalii, vituo vya utamaduni, huduma za usafirishaji, mawasiliano na shughuli za kibenki. UTALII Mkoa una maeneo mazuri ya vivutio vya utalii ambavyo ni Hifadhi ya Taifa ya Tarangire na Ziwa Manyara ambako hupatikana aina mbalimbali za wanyamapori kama Simba, Chui, Chita, Twiga, Pundamilia, Swala, Nyati, Pofu, Ngiri, Mbuni, Korongo nk. Eneo jingine la utalii ni Yaeda Chini ambako upatikana jamii ya Wahadzabe ambao huishi kwa kutegemea uwindaji, matunda, mizizi na asali. Hivyo, Mkoa unawakaribisha wawekezaji kuanzisha na kuwekeza katika hoteli na vituo vya utamaduni kwa ajili ya kutoa huduma muhimu kwa Watalii mbalimbali wanaotembelea Mkoa huu.

MISITU
Wawekezaji wanakaribishwa katika Mkoa kuwekeza katika shughuli za Ufugaji nyuki na uzalishaji Asali. Mkoa una eneo lenye ukubwa wa hekta 927,526 za hifadhi za Misitu zilizohifadhiwa kisheria ambamo shughuli za ufugaji nyuki na uzalishaji Asali zinaweza kufanyika. Tayari baadhi ya wananchi wanaendelea na shughuli hii katika misitu asili na binafsi iliyopo katika maeneo mbalimbali ya Mkoa.

MADINI
Mkoa una utajiri mkubwa wa madini ya Tanzanite ambayo yanathamani kubwa na hayapatikani mahali popote duniani isipokuwa Mkoani Manyara Wilaya ya Simanjiro eneo la Mirerani. Madini mengine yanayopatikana Mkoani hapa ni pamoja na: Ruby, Green Garnet, Green Tourmaline na Rhodilite. Ukiacha madini ya Tanzanite, hakuna uwekezaji katika aina nyingine ya madini tajwa hapo juu hivyo Wawekezaji wanakaribishwa kuwekeza katika Sekta ya Madini.

FURSA ZA UWEKEZAJI KATIKA HUDUMA ZA KIJAMII
Mkoa unawakaribisha wawekezaji kuwekeza katika Sekta za Elimu, Afya na Maji kwani huduma zinazoendelea kutolewa kupitia Sekta hizi bado hazitoshelezi na ni duni katika baadhi ya maeneo. Lengo kuu la Mkoa ni kuimarisha Sekta hizi ili kusaidia kuleta maendeleo ya haraka na kuondoa umaskini kwa Wananchi.

FURSA ZA UWEKEZAJI KATIKA HUDUMA ZA KITAMADUNI
Ili kudumisha tamaduni zilizopo, Mkoa kupitia Hospitali ya Rufaa ya Haydom iliyopo Wilayani Mbulu inajenga kituo cha Utamaduni (4corners) kitakachofanya utafiti wa mila na desturi za makabila 4 ya Mkoa wa Manyara ambayo ni Wahadzabe, Wanyaturu, Wairaqw na Wabarbaig. Vilevile, Mkoa unakituo cha Redio cha kijamii cha ORKENERI RADIO SERVICE 94.40RS FM kilichopo Wilayani Simanjiro kinachofanya kazi kubwa ya kutangaza utamaduni wa jamii ya Kimaasai. Hata hivyo Mkoa unawakaribisha wawekezaji kuanzisha vituo vingine vya Utamaduni katika maeneo mbalimbali kama vile Yaeda Chini ili kuwavutia zaidi Watalii. Aidha, Mkoa unawakaribisha wawekezaji kuwekeza katika Michezo ya aina mbalimbali kwani kwa Miaka mingi sasa Mkoa umekuwa chimbuko la Wanariadha maarufu nchini Tanzania ambao walipeperusha Bendera ya Tanzania katika mashindano mbalimbali ndani na nje na kuuletea sifa Mkoa na Nchi. Miongoni mwawanariadha hao ni; Gidamis Shahanga, Joh Bura, John Stephen Akhwari, Zakayo Malekwa na Simon Robert Naali.

MPYA KUHUSU MATIKITI MAJI - water melon



Ili kulima matikiti maji, inakubidi uwe na sehemu ya kutosha, yenye jua la kutosha, maji mengi na ardhi yenye rutuba ya kutosha, matikiti maji hukua haraka kama mimea mimgine ya jamii yake itambaayo mfano Matango, maboga na maskwash.
Kwa mtu ambaye anaanza kilimo yatampa tabu kidogo tofauti na Yule ambaye ana ujuzi kidogo na mambo ya kilimo kwa sababu yanahitaji umakini kiasi.

HALI YA HEWA
Mimea hii haihimili hali ya joto kali sana, mvua nyingi na udongo unaotuamisha maji, magonjwa ya fangasi na wadudu waharibifu, inastawi vizuri kwenye kuanda wa pwani na miinuko kidogo kama DSM,Tanga, Morogoro, Mtwara, lindi na Pwani ambapo kuna jua la kutosha. Muda mzuri wa kupanda ni kipindi cha kipupwe mwezi wa machi mpaka wa septemba .

UPANDAJI
Panda kwa kutumia Mbegu zinazouzwa madukani, ukitumia Mbegu kutoka kwenye tikiti ulilonunua linaweza likawa ni hybrid na matokeo yake matikiti yatakayozaliwa hayatakuwa bora kwa sababu yatakuwa ni kizazi cha pili (F2)
Panda Mbegu yako moja kwa moja kwenye shamba, usinunue miche au kupanda Mbegu kwenyemifuko ya plastiki halafu ndi uhamishie shambani, panda Mbegu mbili sentimeta 2 chini ya udongo kwa umbali wa sentimeta 30 kutoka shina hadi shina na mita 2 - 3 kutoka mstari hadi mstari, baada ya siku chache Mbegu zitaanza kuota, baada ya kama wiki 2 katika Mbegu mbili ulizopanda kata moja na uache ule mche wenye afya zaidi, angalizo using’oe mche bali ukate ili kuzuia kusumbua mizizi ya mche uliobaki.
Unaweza kupandishia udongo kwenye mashina na hii itasaidia kupunguza maji yasituame kwenye mimea yako, pia unaweza kuweka samadi badala ya kupandishia udongo ukiwa na nia ileile ya kuzuia maji yasituame na kuongeza rutuba.
Kama una sehemu ndogo ya shamba unaweza kuyawekea matikiti waya wa kutambalia, ila inabidi uwe imara kwa sababu ya kuhimili uzito wa matunda yenye, na wakati wa kuanza kutambaa kwenye waya ni lazima uifundishe mimea kwa kuielekezea kwenye waya na kufungia


MCHE ULIOCHIPUKA



UANGALIZI
Miche ikiwa imetambaa kiasi unaweza kuweka matandazo kwenye udongo ili kuzuia upotevu wa unyevu, unaweza kuweka samadi au mbolea za viwandani, mimea ikiwa midogo tumia zaidi mbolea zenye nitrojen na utumie zaidi mbolea za potasiam mara baada ya maua kutokeza hadi matunda kukomaa, matawi yakifikia urefu wa mita 2 kata mbele ilikuruhusu kutoa matawi na hivyo kupata maua mengi zaidi hatimaye mavuno zaidi

MAUA NA MATUNDA
Matikiti hutoa maua dume na jike kwenye tawi moja, maua dume ambayo ni madogo zadi hutoka kwanza yakifuatiwa na maua jike ambayo ni makubwa zaidi, usipoona maua dume na jike kuna tatizo mfano maji kidogo yalimwagiliwa, upungufu wa viritubisho kwenye udongo, hali ya hewa ni joto/baridi sana n.k
Uchavushaji kwenye matikiti hufanyika na wadudu, kama huwaoni wakifanya kazi yao unaweza kufanya mwenyewe, muda mzuri ni wa asubuhi, unakata maua dume kwa kisu na kufanya uchavushaji kwenye maua jike, maua jike ya mwanzo kwenye tawi ndiyo yenye ukuaji bora zaidi, unaweza kukata tawi lisiendelee kukua baada ya matunda kutokeza hii husababisha kuwa na matunda makubwa zaidi


UCHAVUSHAJI KWA MKONO



 UVUNAJI MATIKITI
Ili kujua matikiti yamekomaa inahitaji ujuzi kidogo, upande wa chini wa tunda huanza kuwa na rangi ya njano, pia kikonyo juu ya tunda hukauka kabisa na kuwa kijivu, ila njia nzuri ni kuyapiga kwa kiganja na kusikiliza mlio wake kama tunavyofanya kwenye mafenesi, hii nayo ni shule nyingine. Tumia kisu wakati wa kuvuna matikiti, yabebwe na kuhifadhiwa vizuri kwenye makasha tayari kuuzwa au kwa matumizi binafsi

MAGONJWA NA WADUDU
Wadudu wa matikiti wako wanaoshambulia majani na maua, na wengine hushambulia matunda , pia kuna magonjwa ya fangasi ambayo hushambulia mimea, ili kujua dawa za magonjwa ni vizuri kuchukua sampuli na kwenda nayo kwenye duka la dawa na pembejeo za kilimo ili kjupata dawa sahii, dawa aina ya KARATE itasaidia kuua wadudu wa majani, maua na matunda na FUNGICIDE itasaidia kwa mashambulizi ya fangasi

SOKO LA KATANI YA TANZANIA NCHINI MAREKANI LIMEDORORA





Soko la Katani ya Tanzania nchini Marekani limedorora kufuatia kuibuka ushindani mkali kutoka Brazil huku kimbilio la katani ya Tanzania likibaki nchi za Afrika na Asia.

WADAU WAOMBWA KUDHAMINI MAONYESHO YA KAZI ZA VIJANA WAJASIRIAMALI YATAKAYOFANYIKA DODOMA


Mkurugenzi wa Mtendaji wa Kampuni ya Aj It Development  Bw Jackson Audiface akizungumzia  kuhusu Maonyesho ya Tatu ya Kazi za Vijana wajasiriamali Yatakayofanyika Mkoani Dododma Mwezi Aprili mwaka huu.Maonyesho hayo ya kazi za Vijana wajasiriamali Hususani Vijana wanaosoma Vyuo Vikuu vya Dodoma. Lengo la Manonyesho hayo ni Kuzitangaza Kazi za Vijana wajasiriamali Wa Tanzania.Pili kuwapa Muda wadau Mbalimbali Kukutana na Vijana Wajasiriamali Ili kutatua Kero zote zinazowakabili vijana Katika Shuguli zao za Ujasiriamalia .




 Baadhi ya Bidhaa Ambazo zinazozalishwa na Vijana wajasiriamali Waliohitimu Vyuo vikuu Mbalimbali hapa Nchini Na Ambao Bado wako Vyuoni kuendelea na Masomo yaoamabzo zitaonyeshwa katika Maonyesho hayo Yatakayofanyika Mkoani Dodoma Yakiwa Ni ya Tatu kuafanyika hapa Nchini kwa Lengo la Kukuza soko la Kazi za Vijana wajasirimali pia Kuzitangaza na Kuatatua Ngangamoto Mbalimbali Zinazowakabili Vijana wa Kitanzania Kama Vile Vibali vya Kufanya Biashara Kutoka Mamlaka Mbalimbali hapa Nchi.Wadau Mbalimbali wa Vijana Mnaombwa Kujitokeza Kudhamini Maonyesho hayo. Bidhaa mbali mbali za kilimo zinazo zalishwa na
Vijana wa Mkoani Dodoma Ambao watazionyesha kwa Wakazi wa Mkoa wa Dodoma na Mikoa ya Jirani.






Jackson Audiface Akielezea Zaidi Kuhusu Maonyesho hayo Yatakayofanyika Mkoani Dodoma.Hapa Akiwa Ameshika Mafuta yanayozalishwa na Vijana wajasirimali wa Mkoani Dodoma jana Wakati wajasiriamali hao walipotembelea Ofisi za Kampuni ya Aj It Development Kwajili ya Kujisajili ili kushiriki Katika Maonyesho ya Kazi za Vijana wajasiriamali Yatakayofanyika Mkoani Dodoma


KUPE WEKUNDU KWENYE MASIKIO YA NG'OMBE


Ugonjwa huu hushambulia wanyama kama ng'ombe, mbuzi na kondoo na husababishwa na vimelea vijulikanavyo kama Theileria parva ambavyo vusambazwa na kupe wekundu wa kwenye masikio wajulikanavyo kama Rhepicephalus Appendiculatus, ugonjwa huu usipodhibitiwa unaweza kusababisha vifo vya wanyama wengi sana na pia ni aghali kuutibu kulinganisha na magonjwa mengine




DALILI ZA UGONJWA HUU
Homa kali, mnyama kushindwa kupumua vizuri,  kukohoa pamoja na kutoa makamasi, kuharisha na kuvimba matezi

MATIBABU
Mnyama inabidi apigwe sindano ya dawa za  PARVAQUONE au BUTALEX kiasi cha ml 20 (soma kimbatanisho cha dawa kwa maelezo zaidi) na kurudia baada  ya siku moja kupita, yaani ukuchoma leo unarudia dozi kesho kutwa, pia mnyama achomwe dawa ya OTC20% kipindi chote cha matibabu





KINGA
Kinga kubwa ya ugonjwa huu ni kuhakikisha kwamba mifugo yako inaoga mara kwa mara kwenye majosho au kwa kuwanyunyuzia dawa za kuua wadudu wa mifugo


NG'OMBE WAKIOGESHWA KWENYE DAWA 
 
 


KILIMO CHA KUTUMIA MAHEMA CHAINUA UZALISHAJI WA KILIMO NCHINI KENYA



 




Wakikabiliwa na eneo dogo la kulima kutokana na kukua kwa idadi ya watu na hali za hewa zisizotabirika, wakulima wengi wa Kenya wamegeukia teknolojia ya kilimo cha mahema kama njia ya kuongeza uzalishaji na kunyanyua kipato chao.
Kukua kwa umaarufu wa kilimo wa mahema kulioneshwa katika Maonesho ya Biashara ya Kimataifa ya kila mwaka mjini Nairobi mwezi wa Oktoba ambapo waoneshaji wa kilimo cha kutumia mahema walisema kuwa waliona kuinuka kwa hamu ya umma katika kilimo hicho.
"Wakenya wengi wameanza kufuata kilimo cha kutumia mahema kwa sababu kinahitaji mtaji mdogo ili kuanzisha na wakulima wanaweza kuzalisha zaidi katika shamba dogo," alisema Moses Khaemba wa Kampuni ya Hortipro Limited, iliyoko Nairobi ambayo inatengeneza mahema ya kilimo kwa gharama ndogo.
Pamoja na kuwa inakuwa ya gharama ndogo na rahisi kuyaweka, mahema ya kilimo pia gharama ndogo ya ushughulikiaji, yantumia maji kwa ufanisi na yanaweza kuhamishwa baina ya vitalu, alisema, na kuongeza kuwa wakulima wanaweza kuona faida yake kuanzia mavuno ya kwanza
"Kilimo cha kutumia mahema ya plastiki kina faida nyingi," Khaemba aliiambia Sabahi. "Faida hizi ni pamoja na uzalishaji wa juu zaidi na wa kuendelea kwa kila ekari moja, jambo lenye maana ya kupata faida kubwa zaidi, kujikinga na masuala ya hali ya hewa kama vile ukungu na upepo, kutokuwepo na hatari ya wadudu waharibifu, kupata mwanga asilia na upitishaji wa hewa, miongo mirefu ya upandaji na matumizi madogo ya maji, hasa katika maeneo yenye ukame."
Ukubwa wa mahema ya kilimo unategemea na uwezo wa mkulima wa kuyashughulikia na ukubwa wa shamba, alisema. Wastani wa kila hema moja ni upana wa mita 8 na urefu wa mita 30 na hugharimu shilingi 150,000 (dola 1,800). Kampuni imepokea zaidi ya maombi 1,000 ya mahitaji kutoka kwa wakulima mwaka huu -- ongezeko la asilimia 25 ikilinganishwa na 2011 -- vivyo hivyo na ongezeko la mahema mengi katika shamba hilo hilo, Khaemba alisema.
Mahema ya kulimia yanaweza kuwa ama katika muundo wa jadi kama nyumba au muundo wa upenyo - marefu yakiwa yamefunikwa kwa plastiki juu ya mazao. Wakulima wasema kwa kutumia mahema yenye umbo la upenyo, wanaweza kuzalisha zaidi kuliko katika ardhi ya wazi.
"Mimi ninayo mahema mawili katika shamba langu la ekari tatu huko Karen Estate mjini Nairobi ambako nimepanda nyanya," Margaret Wanjiku, mweny umri wa miaka 54, aliiambia Sabahi.
Wanjiku, ambaye alistaafu miaka mitano iliyopita kutoka shirika moja la kimataifa la msaada, alisema kuwa mmea wa nyanya unaweza kuzalisha kilo 16 hadi 20 za nyanya.
Ingawa bei hubadilikabadilika kutokana na upatikanaji wa bidhaa na mahitaji, alisema kuwa kila mita mraba moja ya nyanya humuingizia kiasi cha shilingi 3,000 (dola 35). "Ninauza nyanya zangu kwenye duka kubwa iliopo karibu na nyingine kwa majirani zangu," alisema.
Amos Karanja ametenga sehemu ya shamba lake la robo ekari huko Kitengela, Jimbo la Kajiado, kwa ajili ya kulima nyanya ndani ya mahema. "Ingawa ninayo kazi ya mchana, ninajaribu aina hii ya kilimo kama njia ya kupata mapato ya ziada ili kuisadia familia yangu," aliiambia Sabahi.
Dan Wanjohi kutoka kampuni Daner Greenhouse Limited huko Ongata Rongai, eneo la makazi ya watu katika Mkoa wa Bonde la Ufa, alisema kuwa kimwonekano aina yoyote ya mboga inaweza kulimwa katika mahema ya kilimo, ikiwa ni pamoja na matango, vitunguu na kabichi.
"Wakulima wengi nchini Kenya wanapendelea kulima nyanya kwa sababu ni mmea unaotoa mazao mengi na mtu hupata faida ndani ya miezi mitatu baada ya kuotesha," aliiambia Sabahi.
Alisema kuwa kampuni yake inatumia chuma cha pua katika ujenzi wa hema la ukubwa wa mita 8 kwa 30 na huuzwa kwa shilingi 200,000 (dola 2,300) kwa moja. Gharama ni pamoja na kulaza bomba kwa ajili ya umwagiliaji maji kwa matone.
Hata hivyo, wakulima ambao hawawezi kumudu gharama za majengo ya chuma cha pua, bado wanaweza kutumia mahema ya vipenyo kwa kutumia mbao kwa gharama ya chini zaidi. "Nililipa shilingi 70,000 (dola 818) kwa kujenga hema langu," Karanja aliiambia Sabahi.

Tuesday, February 18, 2014

MZEE MWINYI AZINDUA MPANGO ENDELEVU KWA WAKULIMA


Rais Mstaafu wa awamu ya pili Ali Hassan Mwinyi, akizindua  mpango maalumu  na  endelevu wa kumuwezesha mkulima yeyote hapa nchi  kupata trekta  kwa bei nafuu kupitia ushirikiano wa benki ya KCB Tanzania,anaeshuhudia kulia ni Diwani wa Kwadelo wilaya ya kondoa mkoani Dodoma,Bw.Omary Kariati aliefanyikisha mradi huo na kununua trekta(15)kwaajili ya wakulima nchini.Hafla hiyo ilifanyika Mikocheni jijini Dar es Salaam jana.
 
 
 


Rais Mstaafu wa awamu ya pili Ali Hassan Mwinyi, akiwasha Trekta ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa  mpango maalumu  na  endelevu wa kumuwezesha mkulima yeyote hapa nchi  kupata trekta  kwa bei nafuu kupitia ushirikiano wa benki ya KCB Tanzania, Hafla hiyo ilifanyika nyumbani kwake Mikocheni jijini Dar es Salaam.Anaeshuhudia kulia ni Diwani wa Kwadelo wilaya ya kondoa mkoani Dodoma,Bw.Omary Kariati aliefanyikisha mradi huo na kununua trekta(15)kwaajili ya wakulima  nchini.




Rais Mstaafu wa awamu ya pili Ali Hassan Mwinyi, akiangalia moja ya  Trekta  kati ya(15) kabla  ya kuzindua mradi endelevu wa kumuwezesha mkulima yeyote hapa nchi  kupata trekta  kwa bei nafuu kwa ushirikiano na benki ya KCB Tanzania na Diwani wa kata ya Kwadelo Bw.Omary Kariati.Hafla hiyo ilifanyika nyumbani kwake Mikocheni jijini Dar es Salaam.
 
 


Rais Mstaafu wa awamu ya pili Ali Hassan Mwinyi, akiongea wakati wa hafla ya uzinduzi wa  mpango maalumu  na  endelevu wa kumuwezesha mkulima yeyote hapa nchi  kupata trekta  kwa bei nafuu kupitia ushirikiano wa benki ya KCB Tanzania na Diwani wa kata ya kwadelo wilaya ya kondoa mkoani Dodoma, Bw.Omary Kariati wapili kushoto. Hafla hiyo ilifanyika nyumbani kwake Mikocheni jijini Dar es Salaam.



Baadhi ya wakuliama wa kata ya Kwadelo wilaya ya kondoa mkoani Dodoma wakimsikiliza Rais Mstaafu wa awamu ya pili Ali Hassan Mwinyi,(hayupo pichani)akiongea wakati wa makabidhiano rasmi wa Trekta(15)kuzindua mradi endelevu wa kumuwezesha mkulima yeyote hapa nchi  kupata trekta  kwa bei nafuu kwa ushirikiano na benki ya KCB Tanzania na Diwani wa kata ya Kwadelo Bw.Omary Kariati.
 
 
 
Rais Mstaafu wa awamu ya pili Ali Hassan Mwinyi, akisalimiana na Mkurugenzi wa ushirikiano wa kibenki wa benki ya KCB Tanzania,Bw.Frank Nyabundege(kushoto)wakati wa hafla ya uzinduzi wa  mpango maalumu  na  endelevu wa kumuwezesha mkulima yeyote hapa nchi  kupata trekta  kwa bei nafuu kupitia ushirikiano wa benki ya KCB Tanzania na Diwani wa kata ya kwadelo wilaya ya kondoa mkoani Dodoma, Bw.Omary Kariati(kulia). Hafla hiyo ilifanyika nyumbani kwake Mikocheni jijini Dar es Salaam.

WIZARA KUNUNUA MAZAO YA NAFAKA NCHINI






Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika imetangaza nia yake ya kutaka kununua mazao ya nafaka ili kumwekea mkulima wa hali ya chini soko la uhakika.
Miongoni mwa mazao yatakayonunuliwa kupitia Bodi  ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko  ni mpunga,maharagwe,karanga,choroko,ulezi,ufuta na mahindi,na yatanunuliwa kwa bei ya ushindani ya soko mwaka huu.
Hayo ni kwa mujibu wa Mchumi wa bodi hiyo Bw. Edwin Mkwenda  katika maonesho ya wakulima yaliyofanyika kitaifa katika Viwanja vya Nzuguni Manispaa ya  Dodoma.
Bw. Mkwenda alisema tayari Serikali imeikabidhi bodi hiyo maghala yote yaliyokuwa ya Shirika la Usagishaji la Taifa (NMC),ambayo hayakubinafsishwa zilizoko  kwenye kanda saba  ili kutunza mazao yatakayonunuliwa.
Kuundwa kwa bodi hiyo ni ukombozi kwa wakulima kwani watakuwa na uhakika wa kupata soko la mazao husika.



UMWAGILIAJI WA MATONE KUONGEZA UZALISHAJI



Serikali imepanga kuendeleza teknolojia ya Umwagiliaji wa Matone ili kuongeza kiwango cha uzalishaji wa mazao kwa wakulima.
Akizungumza katika kilele cha maonesho ya sikukuu ya wakulima ya Nane Nane katika Viwanja vya Nzuguni mkoani Dodoma, Makamu wa Rais wa pili wa Zanzibar, Balozi Seif Ally Iddy alisema kuwa umwagiliaji kwa njia ya matone utasaidia katika kukuza  uzalishaji wa mazao ya nafaka na bustani.
“Kutokana na teknolojia hii mpya ya umwagiliaji wa matone serikali imeweza kuvuna tani 16,510 za mazao kwa mwaka’’, alisema Balozi Seif.
Aliendelea kueleza kuwa teknolojia ya umwagiliaji ni lazima ipewe kipaumbele na kutekelezwa nchi nzima ili wakulima waweze kuzalisha mazao kwa wingi na kuuza ndani na nje ya nchi.
Aidha Balozi Seif aliwataka waandaaji na waendeshaji wa maonesho ya Nane Nane (TASO)  waweke utaratibu mzuri wa maonesho hayo ili wakulima waweze kuhamasika na kuhudhuria kwa wingi ili wapate mafunzo ya kilimo na ufugaji

WAZIRI WA KILIMO CHAKULA NA USHIRIKA AMESEMA HAPENDI KUONA TASNIA YA SUKARI IKIKOSA MWELEKEO





"Mhe. Eng. Christopher Kajoro Chiza Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika akitoa hotuba kwa Wadau wa Sukari katika Mkutano uliofanyika Mjini Morogoro Mwanzoni mwa Januari 2014.

Mhe. Eng. Christopher Kajoro Chiza (Mb) Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika ameonya kuwa kuwa Serikali haitapenda kuona Tasinia ya Sukari ikikosa mweleleo kutokana na matakwa ya kundi fulani. Alisisitiza kuwa, Tasnia ya sukari ni moja ya tasnia kubwa nchini ikijumuisha wadau muhimu wakiwamo walaji, wakulima, wafanyabiashara na wazalishaji. Kila mdau katika jumuisho hili ana maslahi ambayo kwa namna moja au nyingine yanaweza kukinzana na ya mdau mwenzake. Mkulima angependa kuona anauza miwa yake kwa bei ya juu, hali kadhalika mzalishaji kuuza sukari anayozalisha kwa bei yenye faida ya kutosha. Aidha mfanyabiashara angependa kupata faida maradufu na panapokuwa na mwanya kuingiza sukari kutoka nje kwa njia sizizo halali. Lakini kwa upande mwingine mlaji naye angependa kununua sukari kwa bei nafuu.
Serikali haipo tayari kuona tasnia kubwa na muhimu kama hii ya sukari ikipoteza mwelekeo, aidha ingependa kuwepo kwa mazingira mazuri (win - win situation) kwa kila mdau. Kwa maana hiyo nimeona ni jambo jema na muhimu sana kuwakutanisha ninyi wadau ili tuweze kujadili kwa pamoja changamoto zilizopo mbele yetu juu ya sekta hii. Ni matarajio yangu kwamba, mkutano huu utaweka misingi ya kufikia utatuzi wa chamngamoto hizi kwa manufaa ya pande zote
Mhe. Waziri ameyasema hayo katika mkutano wa Wadau wa Sukari uliofanyika Mjini Morogoro mwanzoni wa mwezi Januari
Akitoa picha halisi ya uzalishaji na mahitaji ya sukari hapa nchini Waziri Chiza alisema kuwa, Wakati viwanda vyetu vinabinafsishwa vilikuwa vinazalisha wastani wa tani 120,000 kwa mwaka. Sasa uzalishaji umefikia wastani wa tani 300,000 kwa mwaka.
Aidha uzalishaji wa miwa (siyo sukari) katika mashamba ya wakulima wadogo nao umeongezeka kwa asilimia 61 (hii ni kutoka wastani wa uzalishaji wa tani 439,122 hadi tani 705,176 kwa mwaka). Uzalishaji katika mashamba ya wenye viwanda umeongezeka kutoka wastani wa tani 1,083,738 na kufikia tani 2,229,274 kwa mwaka (ongezeko la asilimia 105).
Pamoja na mafanikio haya bado tasnia ya sukari imegubikwa na changamoto mbali mbali kubwa zaidi ikiwa uzalishaji usiokidhi mahitaji. Mahitaji yetu ni wastani wa tani 590,000 za sukari kwa matumizi ya kawaida na ya viwandani. Viwanda vya sukari nchini huzalisha takribani asilimia sabini tano (75%) ya mahitaji ya sukari ya matumizi ya kawaida. Wastani wa tani 290,000 ni nakisi inayojazwa na uagizaji sukari kutoka nje. Nakisi hii inajumuisha sukari ya matumizi ya kawaida (gap sugar) ya wastani wa tani 120,000 na sukari ya matumizi ya viwandani ya wastani wa tani 170,000 kwa mwaka. Kiasi chote cha sukari ya matumizi ya viwandani kinaingizwa nchini kutoka nje. Aidha uagizaji wa sukari ya matumizi ya kawaida unategemea hali halisi ya soko kwa kipindi husika na kwa hiyo uagizaji halisi unaweza kuwa juu au chini ya nakisi hiyo. Hata hivyo, Kamati ya Ufundi ya Ushauri ya Uagizaji Sukari iliyokutana tarehe 24/12/2013 kujadili hali ya sukari nchini imependekeza kuwa mwaka huu 2013/2014 kusiwe na uagizaji wa sukari kwa sababu kiasi tha tani 257,000 kitapatikana kwa matumizi ya kawaida kuanzia sasa hadi mwishoni mwa 2013/2014.

UKULIMA WA VITUNGUU





 ndugu zangu ambao mnabweteka na kutafuta kazi kuna kilimo cha vitunguu, two years unakuwa mtu mwingine kabisa na huta penda kuajiriwa na kama utakuwa kwenye ajira unaweza acha kabisa na kuamua kuwa mkulima. Tusiwaze kuajiriwa tu tutakufa maskin mwisho wa siku. Mimi nimejaribu na sasa nataka niache kazi na kuwa moja ya wakulima na wafanyabiashara wakubwa wa vitunguu na mazao yote ya shamba kwa ujumla ila pamoja na hilo bado nahitaji muongozo mkubwa kwa watu waliobobea kwenye ukulima pamoja na biashara ya mazao ya shambani ili waweze kunishauri zaidi. Mimi napatikana moshi pamoja na arusha ndiko napofanyia biashara zangu. Please kwa yoyote ambaye amebobea kwenye biashara hii zaidi naomba ani PM ili tuweze kupeana contact ili mkukuza network na bidae kuweza kuanzisha kitu flani kwa manufaa yetu asanteni sana na wakilisha.

MABADILIKO YA HALI YA KIBIASHARA TANZANIA



MABADILIKO YA HALI YA KIBIASHARA TANZANIA







Kama ukiangalia vizuri nchi yetu ya Tanzania inatengeneza mabadiliko fulani ya kibiashara na kiuchumi na mabadiliko haya yatakuwa na athari na faida zake.

1. Kwa sasa serikali imeamua kutengeneza vitambulisho vya utaifa hii ni ili kupata taarifa muhimu za kila mtanzania kuanzia
alikozaliwa hadi aliposasahivi.
2. Wanapitisha dodoso kwa kila nyumba na eneo ili kutambua ni nyumba ngapi zinatumika kama nyumba na sehemu ya
biashara na ngapi zinatumika kama nyumba peke yake au sehemu ya biashara peke yake ( hapa ni lazima uandike na jina
la biashara na biashara unayoifanya katika ofisi yako.
3.Tra kusisitiza matumizi ya EFD
4. TBS kusisistiza matumizi ya nembo zao katika bidhaa.

ukiangalia hivyo ni baadhi tu ya mabadiliko tuliyonayo kwa hivi sasa kitu kikubwa kinachoatafutwa hapo ni kodi na ubora wa biashara,asilimia kubwa ya wanaofanya biashara na wajasiriamali wamekuwa inspired na wajasiriamali wakubwa kutoka nje ya nchi na wengi wametumia baadhi ya njia walizotumia na kuweza kuyaona mafanikio lakini sasa serikali imebadilika inahitaji kila kitu kiwe perfect kama ambavyo ilivyo katika nchi tunazokopi kwao.

kuna watu wengi hufanya vitu bila hata kujua vina umuhimu gani kuna wanaotengeneza Logo kwa kuwa wanajua ili biashara iitwe biashara ni lazima uwe na logo, kuna wanaoprint fliers,posters, nakadhalika bila kujua zina faida gani na zinatoa majibu baada ya muda gani na unaziweka kwa mpango wa muda gani watu hufanya tu kwa mazoea ndio maana hata ukiangalia mabango ya kampuni zetu ni tofauti na mabango ya kampuni za nje.tunafanya vitu kiholela lakini serikali imeamua kututoa huko bila kutuambia kama tunahama kwenye mazoea tunaenda kwenye uhalisia.

kiukweli uhalisia ni mgumu kwa sababu bado watu hawajui faida na hasara au sababu na maana ya kufanya hivyo, lakini Tanzania inageuka kuwa nchi ya uwekezaji siku sio nyingi makampuni mengi yanakuja na kufungua matawi nchini kwetu hivyo tunahamishwa kwa sababu maalum, na kwa kuliona hilo Legacy Impresion Company inatoa ofa kwa wale wote wamiliki wa biashara na ambao wanatarajia kufungua biashara kuja kupata semina ya utambuzi wa matumizi na umuhimua wa vifaa vya kuitambulisha biashara yako kwenye jamii. ( Logo, Fliers,Brochure,Business card, nk) semina hii inatolewa bure kwa kila mfanyabiashara atakaefanya (Branding package) kutoka Legacy amabapo package hii inajumuisha dizaini tofauti tofauti za vifaa vinavyokutambulisha kwenye jamii na mteja unaemtarajia.

Muda wa kufanya kazi kwa mazoea unahesabika badilika sasa, badilika na Legacy,tunapatika Kijitonyama,Dar es salaam,na tunashughulika na kufanya Graphic design, Printing,Webtech,stationery na Brand Consult, mawasiliano ni 0713603699 au info@legacytz.com,website ni .:LEGACY TANZANIA:.



BAADHI YA NJIA UNAZO WEZA KUTUMIA KUPATA WAZO BORA LA BIASHARA



IDEA ya Biashara ni moja ya mambo yanayo waumiza watu wengi sana, Na mara nyingi wazo la biashara linahitaji utafiti wa kina ili kuja na wazo lenye tija kwako na kwa jamii nzima,

HIZI NI MOJA YA NJIA ZA KUPATA WAZO LA BIASHARA


1. TUMIA UJUZI ULIONAO
Ujuzi ulionao ndo sehemu ya kwanza kabisa ya kupata wazo la Biashara, Mfano kama wewe umejiliwa na ni Fundi wa kushona Nguo, why usianze na wewe kuwa na biashara ya aina hiyo? Kama wewe ni fundi magari why usianzishe gereji yako?
Ujuzi ulianao ndo hazina ya kwanza nay a kipekee ya kupata wazo na mara nyingi wajasirimali wengi waliofanikiwa waliacha kazi wanazo fanya na kwenda kuanzisha za aina hiyo na kuzimiliki wenyewe


2. BADILISHA HOBY YAKO KUWA PESA

Hobby ni moja ya maeneo ambayo watu huja kutajilikia, kama wewe hobby yako ni kufuga mbwa kwa nini usianze hiyo biashara ya kufuga mbwa?
Kama Hobby yako ni Kuogelea, kwa nini usinzishe mabwawa ya kuogelea na wengine wakawa wankuja huko kuogelea?
Kam unapenda gardening unaweza anza biashara ya kufanya landscape gardening


3. NUNUA BIASHARA AMBAYO TIYALI IPO
Ukishindwa kabisa kupa wazo mwanana unaweza nunua biashara ya mtu mwingine na kuindeleza, siku hizu kuna biashara kibao zinauzwa kwa sababu mbalimbali so unaweza nunua nu kuendelea nayo


4. Kununua Franchise
Hii ni moja ya njiza zinazo tumika kwa sasa na sehemu nyingi sana, Unaweza nunua Popular Brand na kuifanyia kazi, Ingawa mara nyingi kuna mashariti ya kuambatana ikiwemo kuhakikisha unatoa huduma sawa na Brandi yenyewe, nah ii ni popular sana katika MAHOTELI/MIGAHAWA, MASUPERMARKET NA MADUKA MENGINE
Na usijalibu kutumia Brand ya Kampuni Fulani bila kuwapa Taarifa make inaweza kula kwako na ukajikuta unafilisiwa,
Na ilisha wahi kutokea kwa Kampuni ya Mabasi ya SABENA baada ya kutimia jina la Shirika la Ndege la Ubeligiji, Ila sijui walimalizana vipi, make jamaa bado wanalitumia


5. TUMIA PERSONALITY YAKO
Kuna watu unakuta either ni Mrembo sana, Handsome na kazalika, unaweza utumia huo urembo na uhendsaamu kufanya biashara, either za marketing na kazalika

.
6. NINI KINAKOSEKANA MTAANI?
Tazama ni kitu gani hakipo hapo mtaani and then geuza kuwa opportunity, inaweza isiwe ni mtaani ikawa ni kazini kwako, Kijijini kwenum au maeneo unayo enda kustalehe
-Ni kitu gani huwa kinaleta usumbufu kwako na kukuchukulia muda mwingi na pesa nyingi?
- Ni huduma zipi hazipo kabisa mtaani kwako? Na ambazo ni za muhimu?
-Ni bidhaa zipi ambazo ni vigumu kuzipata mtaani kwenu?
-Ni kitu gani, wewe, Ndugu, Majirini huwa wanakilalamikia sana mtaani hapo?


7. UTALII KATIKA MAENEO YAKO
Hii nayo ni moja ya wazo, so unaweza angalia furusa za utalii kwenye maeneo uliyopo au hata kwingine na kuyafanyia kazi.


8. TUMIA TECHINOLOGIA MPYA KUANZISHA BIASHARA
Angalia mfumo wa maisha wa sasa ulivyo, vitu vinavyo tumika kwa sasa na vinavyo tumiwa na watu wengi, so mfumo wa maisha wa watu kwa sasa unaweza kukuongoza kuja na wazo la Biashara


9. ANGALIA MAKAMPUNI MAKUBWA NA TAASISI ZINGINE WANAHITAJI NINI
Unaweza tumia uwepo wa makampuni Fulani au taasisi Fulani maeneo yako kutengeneza wazo la biashara, taasisi kama Shule, vyuo, Hospitali, Makampuni kama Viwanda Migodi na kazalika, angalia ni kipi hawa watu wanaweza kuwa wanahitaji kwa wingi


10. UNAWEZA KUANGALIA KUHUSU KUUZA BIDHAA ZA WENGINE
Unaweza ukawa unauza bidhaa za watu wengine, unachukua na kuuza


11. ANAGALIA NEWS NA MAKALA MBALIMBALI
Kunachaneli huwa zina makala mazuri sana ya kiuchumi na biashara, hata TBC huwa inamakala Fulani nzuri sana, na kuna chaneli za kimataifa siku huzi kazi yao ni hiyo tu, ni kuonyesja ubunifu wa wajasirimali, so TV, radio na magazeti yanaweza toa mchango w akutosha kwa wewe kupata wazo la biashara


12. CPY BUSINESS AIDEA AMBAYO IMEFANIKIWA KWINGINEKO
Hii ni moja ya njia zinazo tumika kwa sasa, unaweza copya aidea kutoka hata India, China, na kwingineko na ukaja kuifanyia kazi huku kwa kufanya marekebisho madogo kulingana na mahitaji ya eneo husika


13. TUMIA NJIZA ZOTE ZA KIUTAFITI KUPATA WAZO LA biashara- maonyesho ya biashara
-Magazeti,
- Kwenye taasisi za uma zinazo husika na biashara
-Kwa marafiki


14. UNAWEZA GUNDUA KITU?Unaweza ukaja na ugunduzi wako kama walivyo fanya wakina Thomas Edson Michael Dell na wengineo, na ikawa ndo mwanzo wa mafanikoa kwako







Wednesday, January 29, 2014



VIDEO YA MTENDAJI MKUU WA SAGCOT AZUNGUMZIA HALI YA UZALISHAJI WA CHAKULA NCHINI


BONYEZA HAPA KUONA


Kenya yapiga jeki kilimo



 Kenya imezindua mradi mwengine tena ambao ikiwa utafanikiwa utapiga jeki na kuleta maendeleo makubwa katika sekta ya kilimo nchini humo.

Mradi huo 'Galana Kulalu' katika mkoa wa pwani unanuiwa kuziweka katika mpango wa unyunyiziaji maji ekari zaidi ya millioni moja za kilimo hasa cha mahindi na miwa.
Mradi huu unakadiriwa kwamba katika kipindi cha miaka 5 ijayo utagharimu zaidi ya shilingi billioni 250 za Kenya.
Tangu kale maeneo ya bara ya Kenya ndio yamejulikana kuwa na kilimo kinacholisha nchi kutokana na hali nzuri ya hewa na kupata mvua ya kutosha , lakini mpango huu wa Galana Kalula unasemekana utaifanya Kenya kuwa na uwezo wa kujitosheleza kwa chakula na hata kuweka kukiuza nje.
Kila ekari kwa mfano itatarajiwa kuzalisha kati ya magunia 40 na hamsini kutokana na rutuba ya ardhi hiyo na kunyunyiziwa maji kwa kipimo kinachohitajika.
Eneo hilo liko katika majimbo ya Kilifi na Tana river ambayo kwa miaka mingi yamekumbwa na umaskini na yameachwa nyuma kimaendeleo licha ya kuwa na ardhi nzuri ya kilimo.
Hii ilitokana na sera mbovu, ukosefu wa usalama na hivi majuzi kukumbwa na vita kati ya wakulima na wafugaji vilivyochochewa zaidi kisiasa.
Hadi sasa bado kuna hofu miongoni mwa wenyeji kwamba licha ya kuahidi mengi mazuri , huenda wasitendewe haki. Hata hivyo wadadisi wanasema iwapo mradi huo , utatekelezwa kwa haki na uwazi ni fursa nzuri ya kutatua matatizo yanayoilemea kaunti hiyo.