Sunday, March 8, 2015

UFUGAJI WA KISASA VIJIJINI UNAWEZEKANA


IMG_0754
Kuna wafugaji wengi tu wenye imani/dhana kwamba ufugaji wa kisasa vijini hauwezekani kulingana na utunzaji wake. Mfano huu wa Bwana Aidan Paulus wa huko Mbinga utatupa fundisho zuri tu wafugaji wenye imani ya aina hii. Kikubwa ni kuweka jitihada na moyo wa kuthubutu. Yeye amethubutu na ameweza, wewe je?
Ni ndani ya shamba ambalo kiukweli ni msitu wa ukweli ambao ni takribani kilomita za mraba 50 na humo anaishi mwenye shamba Bw. Aidan Paulus Kenyero katika kijiji cha Liganga, wilaya ya Mbinga.
Bwana huyu pamoja na kujihusisha na kilimo cha mazao lakini pia anafuga mifugo…ngómbe zaidi ya 70 na vitu vingine. Nimejifunza namna ya kuhudumia kuku wa mayai na kuepusha mayai kuvunjika pindi yakishatagwa.
Bwana huyu ana nyumba ya ghorofa moja ilojengwa humo msituni mwaka 1989 na anatumia umeme wa gesi (Biogas) ambapo ana mitambo 2. Anacho pia kiwanda cha sukari lakini hakifanyi kazi kutokana na ukiritimba wa serikali hivo amekifunga na mitambo ipo tu imelala
IMG_0755
Kuku wa mayai…anao pia kuku wa kienyeji
IMG_0757
Baadaye kwenye ‘drowa’/saraka ya chini mayai hayo hufichwa
IMG_0758
Kuku akipanda juu akienda kushusha mzigo

No comments:

Post a Comment