Tuesday, March 10, 2015

Wafugaji watakiwa kuacha kuweka alama za moto kwenye ngozi

Naibu waziri wa maendeleo ya mifugo na uvuvi KAIKA SANING’O TELELE
Naibu waziri wa maendeleo ya mifugo na uvuvi KAIKA SANING’O TELELE amezungumzia umuhimu wa wafugaji nchini kuacha tabia ya kuweka alama ya moto kwenye ngozi za mifugo yao ili kulinda ubora wa ngozi za mifugo hiyo. 
Akizindua kamati ya kitaifa ya ushauri wa ngozi jijini DSM , Telele amesema ngozi nyingi zinazozalishwa nchini hazina ubora unaotakiwa kwa sababu zimewekwa alama za moto. 
Nao baadhi ya washiriki wa semina hiyo wamewashauri wafugaji kuzingatia kanuni za ufugaji bora wa mifugo ili kuongeza thamani ya mazao mbalimbali yatokanayo na mifugo yao. 

No comments:

Post a Comment