Tuesday, March 10, 2015

Wakulima mkoani DODOMA waiomba serikali miradi ya umwagiliaji

Katibu Mkuu wa chama cha mapinduzi, ABDULRAHAMN KINANA
Kufuatia Mkoa wa DODOMA kukabiliwa na ukame katika maeneo mmbalimbali, baadhi ya wananchi wilayani CHAMWINO mkoani humo, wameiomba Serikali kuwasadia wakulima miradi ya umwagiliaji, hali ambayo itaongeza tija ya mazao mbalimbali yatokanayo na kilimo ndani na nje ya wilaya ya hiyo.

Wakizungumza mara baada ya Katibu Mkuu wa chama cha Mapinduzi kutembelea wilayani humo, wananchi hao wamsema wakulima wengi wa zabibu wamekuwa wakikabiliwa na changamoto hiyo na kusababisha uzalishaji za zabibu kutokuwa na tija kama ilivyokusudiwa.

ziara ya Katibu Mkuu wa chama cha mapinduzi, ABDULRAHAMN KINANA hapo jana alitembelea katika shamba la zabibu linalomilikiwa na ushirika wa kikundi cha baadhi ya wananchi wa wilaya ya CHAMWINO.

Kisha KINANA akashiriki kupuliza dawa ya kuua wadudu wanaoshambulia zabibu akionyesha kuunga mkono jitihada za kilimo hicho.

Kwa upande wake KINANA, hakusita kutilia mkazo suala la kilimo cha umwagiliaji na uhifadhi wa mazingira kwa wakulima hao

No comments:

Post a Comment