Monday, February 23, 2015

Kilimo cha chai Morogoro chaonesha tija.

Pamoja na changamoto nyingi zinazowakabili wakulima wa zao la chai Tanzania ikiwemo kuyumba kwa  bei ya zao hilo kwenye soko la dunia lakini limeweza  kuzitoa  kwenye lindi la  umaskini kaya  zipatazo  30,000 zilizoko katika wilaya 6 nchini zinazozalisha zao hilo.

Katika mkutano wa uzinduzi  wa mradi wa utetezi  wa wakulima wadogo  wa chai  nchini  ulifanyika mjini Morogoro  inabainishwa kuwa  pamoja na zao hili kuuzwa bei ndogo kwa kilo  katika soko la dunia, lakini bado limeonesha kuondoa umaskini kwa wakulima wadogo kwani chai huvunwa kila mwezi tofauti na mazao mengine ambayo  huvunwa kwa msimu.

Ujio wa sera ya uchumi wa soko katika kuendesha biashara ya chai hapa nchini umeshuhudia changamoto ikwemo bei duni ya majani mabichi ya chai  kwa wakulima nchini.
Tangu mwaka 2004 hadi 2013 bei ya majani  mabichi ya chai   kwa kilo moja imeongozeka kutoka sh.86 hadi sh.206, ongezeko hilo ni dogo sana ikilinganishwa na gharama na uzalishaji wa zao hilo, hata hivyo bado limeonesha kuondoa umaskini kwa wakulima .
Kumeanzishwa mfuko wa  wakfu  wa maendeleo ya  wakulima  wadogo wa chai  Tanzania  , ambao unatakiwa kutatua changamoto za wakulima  huku wataalamu wa mfuko huu wakipewa changamoto.
Kutokana na  asilimia 80 ya chai ya hapa nchini kuuzwa nje ya nchi  moja kwa moja  na kupitia mnada wa  Mombasa ,Tanzania inaingiza  dola  za kimarekani milioni 56 kwa mwaka,tofauti na nchi  jirani ya  Kenya ambayo imekuwa ikijizolea dola za kimarekani milioni 1328.

No comments:

Post a Comment