Wednesday, February 25, 2015

Wawekezaji washauriwa kuwekeza kwenye kilimo

Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika STEPHEN WASSIRA
Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika STEPHEN WASSIRA ametoa wito kwa mashirika ya kimataifa na kampuni binafsi kuwekeza katika viwanda vya kuongeza thamani ya mazao ili kuendana na juhudi za serikali za kuwainua wakulima wadogo

Akizungumza baada ya kikao cha kufanya tathmini ya mfuko wa kimataifa wa maendeleo ya kilimo IFAD, WASIRA amesema asilimia 28.2 ya wakulima wadogo ni masikini hivyo serikali inawaboreshea mazingira ya ili wazalishe kwa tija na masoko yatakuwa ni viwanda vya ndani

Kwa upande wake Waziri wa Kilimo na Maliasili wa ZANZIBAR Dkt SINA UBWA MABWAYA amesema Wazanzibari wamefaidika na elimu waliyoipata kutoka IFAD jambo ambalo litaongeza uzalishaji wa mazao yao.

No comments:

Post a Comment