Tuesday, February 24, 2015

Wajasiriamali waaswa kuendesha biashara zao kitaalamu.

Na Amina Saidi, Mbeya.
Wajasiriamali nchini wametakiwa kujifunza mbinu za kuendesha biashara zao kitaalamu ili kukuza mitaji.
Hatua hiyo itazijafanya biashara hizo kuwa endelevu na zenye tija.
Ni katika uzinduzi wa kitabu cha Mjasiriamali kinacholenga kutoa elimu itakayowasaidia wajasiriamali wadogo na wa kati kukuza mitaji ya biashara zao kitaalamu badala ya kuendesha biashara za kuiga ama kufuata mkumbo ambazo mara nyingi si endelevu.
Mtunzi wa kitabu hicho mjasiriamali mdogo anayejishughulisha na uuzaji wa viatu jijini Mbeya David Mbukwa anawaasa wajasiriamali wenzake kutokuogopa mikopo inayotolewa na taasisi za fedha na badala yake wakope na kuitumia mikopo hiyo kwa malengo mahususi.

No comments:

Post a Comment