Tuesday, February 24, 2015

Waliokopeshwa zana za kilimo watakiwa kuzitumia kwa umakini.

Na Zacharia Mtigandi,
Manyara.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Uwekezaji na Uwezeshaji dokta Mary Nagu, amewataka wananchi waliokopeshwa zana mbalimbali za kilimo nchini, kuhakikisha wanaitumia mikopo hiyo kwa umakini ili iweze kuwa chachu ya kuinu hali zao za kiuchumi.

Aidha aliwataka kuhakikisha wanafanya marejesho ya mikopo hiyo kwa wakati kulingana na mikataba waliokubaliana na taasisi zilizowakopesha.

Zana za kilimo zilizokopeshwa kwa wingi kwa wakulima nchini msimu wa mwaka jana ni pamoja na matrekata makubwa na madogo yanii power tiller mbengu na mbolea.
Zana kama vile matreketa yamewanufaisha wakulima hasa wa wilayani Hanang mkoani Manyara ambao wameongeza uzalishaii wa mazao kutoka tani zaidi ya elfu 80 mwaka juzi hadi tani zaidi 120,000 kwa msimu wa mwaka jana.

Matrekta hayo hayawanufaishi wakulima waliokopa pekee bali hata wakulima wa kawaida wamekuwa wakikodi kwa gharama nafuu.

Akiongea na wakazi wa wilaya ya Hanang Waziri Nagu ambaye pia ni Mbunge wa jimbo hilo alisema kuwa serikali imetoa mkopo wa treketa kwa gaharama nafuu ili kuwawezesha wakulima kumudu.

Aidha aliwataka wananchi wa jimbo la Hanang kuanzisha vikundi vitakavyowasaidia kupata mikopo kwa urahisi kutoka taasisi za kifedha.

No comments:

Post a Comment