Monday, March 2, 2015

ZIFAHAMU TOFAUTI YA ASALI YA NYUKI WADOGO NA ASALI YA NYUKI WAKUBWA

Asali za NYUKI WAKUBWA na WADOGO zina tofautiana katika mambo kadhaa na hvyo ni muhimu kujua tofauti hizo kabla hujanunua ili kua na uhakika.

NYUKI WADOGO
1. Ni nyepesi zaidi kwani ina kiwango cha maji kuanzia asilimia 24

2. Ina ladha ya UCHACHU ingawa ni tamu sana.
3. Mara nyingi ina rangi ya KAHAWIA ILIYOKOLEA inayoenda kwenye WEUSI

NYUKI WAKUBWA
1. Ni nzito kuliko ya nyuki wadogo kwani ina kiwango cha maji kuanzia asilimia 17 hadi 20.
2. Ni tamu moja kwa moja bila kua na ladha ya uchachu kama nyuki wadogo
3. Ina rangi nyingi kuanzia NYEUPE, NYANO, KAHAWIA ILIYOPOA, KAHAWIA ILIYOKOZA n.k

Hizo ni tofauti za muhimu kuzijua kwani zitakuwezesha kupata asali unayoitaka na kuepuka kuibiwa

No comments:

Post a Comment